Kwanini Watendaji na wenyeviti wa mitaa/Kijiji huuza huduma za kiutawala kwa wananchi?

Kwanini Watendaji na wenyeviti wa mitaa/Kijiji huuza huduma za kiutawala kwa wananchi?

Wakati anaanza kuandika nilihisi atashuka na nondo za maana sana! Mpaka mwisho ndo nikajua kuwa alikuwa hajui aendako! Tangu mwanzo alishapitiliza kwao na akaendelea kupuyanga mpaka nje kabisa ya dunia hii!
Uchawa unaua uwezo wa kufikiri"
Hawa masisiemu ni mas nge Sana yaani
 
Ni wizi na rushwa na kwa kuwa imekuwa hivyo kwa muda mrefu, basi imekuwa kama sheria!
Siku nyingine ukiwa na issue ya kawaida, komaa mpaka kieleweke - saa nyingine ni sisi tunawalemaza
 
Mwenyekiti



Huwezi kubishana kwa hoja hadi uongee maneno ya kukera eeh? Ushawahi hata siku moja kushiriki mkutano wa kijiji/mtaa? Au unahisi vitu virahisi tu, yani utoke kwako na kitambi chako kama tikiti bovu, uje kwenye ofisi ya mtendaji/mwenyekiti na mikaratasi yako ya mkopo, ujichekeshe chekeshe ugongewe muhuri na barua ya utambulisho harafu unafuta makalio yako unaondoka, we unahisi hayo makaratasi yamejileta tu ofisini, pen, ink pad viti vyote watu wamechangia, wewe elfu mbili yako unakuja kuitolea malalamiko huku.
Zipo sheria ndogondogo hutungwa kwenye mikutano ya mtaa mfano ada za ulinzi shirikishi na maendeleo ya mtaa mfano ujenzi wa ofisi za mitaa na mengineyo sasa ukute wewe na ujuaji wako hushiriki harafu yakikukuta unalalama,
Usituchoshe muulize aliyekwambia utoe hela hiyo sheria kaitoa wapi kifaruhande wewe
Yote hayo no ushenzi mtupu mwananchi wa kawaida ni haki yake kupatiwa huduma na sio viongozi kutia tia huruma serikali ndogo ndogo za mitaa hadi serikali kuu Wana vyanzo vingi vya mapato kumuongezea mzigo mwananchi kwenye huduma muhimu za kiutawala ni upumbavu
 
Wadau mtakubaliana na Mimi haya mazoea yamekuwa Kama uhalali na Sheria kwamba ukiingia kwenye ofisi ya afisa mtendaji au mwenyekiti lazima uandae sh 2000-5000-20000 kwa ajili ya kupata huduma (mara nyingi huwa muhuri tu wa ofisi)

Miaka nenda miaka rudi haya mazoea hutendeka sijui imeidhinishwa au ni utashi wa watu, na mara nyingi inapotokea madogo wakitaka kuomba mkopo ya elimu ya juu kwenye kuidhinisha taarifa za muombaji hukumbwa na kadhia hiyo wengine ni hawa vijana wanaoenda JKT yaani lazima watozwe hela sijui kwanini ( sio wote ila ni wengi)

Mamlaka tunaomba mtutolee ufafanuzi
Mimi nadhani tukitaka mambo haya ya kutoa pesa Kwa wenyeviti yakomeshwe wawe wanapewa mishahara Kwa mwezi pamoja na wajumbe wao, hivi ni halali kweli mtu atoe muda wake afanye kazi bure? Ana familia na majukumu yake pia .
 
Ni wizi na rushwa na kwa kuwa imekuwa hivyo kwa muda mrefu, basi imekuwa kama sheria!
Siku nyingine ukiwa na issue ya kawaida, komaa mpaka kieleweke - saa nyingine ni sisi tunawalemaza
Unakuta unaomba upewe hiduma fulani halafu mtu anakuambia bila aibu kabisa "leta 3000"
 
Mimi nadhani tukitaka mambo haya ya kutoa pesa Kwa wenyeviti yakomeshwe wawe wanapewa mishahara Kwa mwezi pamoja na wajumbe wao, hivi ni halali kweli mtu atoe muda wake afanye kazi bure? Ana familia na majukumu yake pia .
Lakini hawa watu hawalazimishwi kuchukua hizo nafasi
 
Huduma zipi wananchi tunapaswa kulipia kisheria
Watendaji hairuhusiwi kulipia.

Wenyeviti baadhi ya huduma na baadhi ya Halmashauri. Hivyo inategemeana na Halmashauri ulipo.

Ukitaka kujua fika ofisi ya Mkurugenzi ya Halmashauri uliyopo watakupa orodha ya huduma ambazo wamezipitisha kisheria kulipia Kwa wenyeviti.
 
Wakuu mimi ndio kiranja mkuu huku kuzimu yote yaliyosemwa sio kweli. Narudia tena ni uwongo mtupu.

Kunyweni bia sana imbeni na fanyeni ibada kujifurahisha mwili. Huku hakuna mambo ya duniani kwa hiyo fanyeni mpaka mzeekee.

Huku ni kuzuri ila sio kama duniani. Kuna shida na karaha kuliko duniani. Sio sehemu ya kufikiria kuja ukiwa na nguvu. Ni bora ukae gerezani kuliko kuzimu huku haina vitu vya duniani.
 
Back
Top Bottom