Pre GE2025 Kwanini Wateule wa Hayati Magufuli wanarejeshwa na Wale aliwatumbua na kurejeshwa na Rais Samia wanatumbuliwa tena?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Na Raisi , anaona shida kuwakaripia watu waliomzidi umri
Alafu Kabudi na Lukuvi aliwaaga kabisa tena akawapamba kwamba ameaacha si kwamba hawana uwezo Bali anahitaji vijana ila atawatumia kama washauri ktk mambo mbalimbali ya serikali na atakuwa anaibuka nao sehemu mbalimbali.

Naona tena amewarudisha meaning that aliowateua hawajaendana nae hivyo amewarudisha wale wale aliowapumzisha Kwa maana ya kutoa ushauri
 

Rais Samia Suluhu Hassan anafanya maamuzi yanayozingatia matokeo kuendekeza kile wakichoanzisha pamoja.

Mungu ibariki Tanzania

Kazi iendelee
 
Nadhani ile kauli ya mtanikumbuka tena kwa mazuri ina siri kubwa sana. Hili pia ni katika kukumbukwa
 
shujaa wa familia yako , wew na mke wako na watoto wako
 
Wale walifikuzwa kwa hasira lakini wamerudishwa kwa sababu the government is sinking.
Jambo hili ni political disaster, political mistake,na sasa hivi tunakaribia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa,hili jambo ni political embarrassment.
It was a big government project,ambapo hela nyingi zilitolewa to move detainees across the country.
We do not the right of the government to enforce discipline,we do not enforce the right of anyone who has the task of enforcing discipline to enforce discipline.
Lakini when people are being punished viciously,we always want to ask,"Why such a punishment? What have they done?"
 
Ni mbinu ya kutafuta uungwaji mkono zaidi kuelekea uchaguzi. Kundi lake pekee ameona haliwezi kumpa kura zote. Amewapumzisha watu wa kundi lake kwa muda kwa makubaliano maalum. Watu wake amewapeleka kwenye maandalizi ya kuiba kura ambako anajua wana uzoefu mkubwa. Anataka alitumie kundi la marehemu. Halafu akishafanikiwa kulitumua, atawarudisha watu wake. Ndiyo maana mzee Makamba alisema, watakaporudishwa msiseme kwa nini wamerudishwa"
 
Yaani JPM alikuwa na akili na mtu wa haki? Kazi ipo
Wewe si umekaririshwa na Team za mchongo. Akili umekabidhi watu na hataki kufkir kabsa. Watu wakisema Flani mbaya na wewe unafuata mkumbo tu.
 
Changamoto kubwa, wabunge wa ccm hawana credibility kwenye masuala ya leadership anakosa amweke nani anaona afadhali ya Jana , inasikitisha sana kuwa na wabunge zaidi ya mia tatu halafu walio na credibility ya leadership hawazidi kumi
 
Ngoja tuone Hatima ya Bashiru pia Kabla ya 2025
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…