Kwanini watoto wa Kiafrika ni Wajinga.?

Kwanini watoto wa Kiafrika ni Wajinga.?

Mwananchi wa chini

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2013
Posts
227
Reaction score
599
Thread Hii kwa Hisani ya DK YAHYA MSANGI (PHD)-WEST AFRIKA.

Ukiishi na wazungu utabaini jinsi vitoto vina uelewa. Na ndio maana wengi hupata digrii ya kwanza kabla hajavuka Miaka 18. Miaka 25 tayari wana PhD!

Watoto wa kiafrika digrii ya kwanza sio chini ya Miaka 25! PhD inasomwa uzeeni. Unakuta zee kama nanii anajivunia kuoata PhD Akiwa na miaka 50 tena ya kubumba! Sasa upate PhD na miaka 50 utaitumia umestaafu? Ni Waafrika wachache kama Sisi wapare tunapata PhD Sawa na wazungu. Wachaga mburaa!

Tuangalie sababu.
Sio kwamba mungu katuumba na akili ndogo kuliko wazungu. Tatizo ni jinsi tusivyojali afya zetu.

Kuna kemikali inaitwa LEAD (kiswahili = risasi). Kemikali hii unahusika mno na ujinga ! Inadhuru watoto na watu wazima lakini madhara kwa watoto ni makubwa. Kemikali hii husabanisha "IQ" ishuke. Ikimuatjiri Mtoto sana IQ inashuka mpaka mshale unasoma "Mafuta yameisha"!! Mtoto au mtu anakuwa "100% mjinga"!!!

Mitoto ya namna hii ukiituma dukani Lazima uandike kikaratasi akampe mwenye duka (kama atafikisha).

Watu wazima aina hiii utaikuta Iko mahakamani kutwa na haina kesi. Au inashiriki jambo ambalo unashangaa ni akili yakeee au kavuta cha Arusha?! Mfano unawezaje kulipa nauli kwenda kudai watoto wa nanii? Yaani hukuona umuhimu kwenda kudai wawekeze kulima michikichi mawese yaongezeke wee na Mimba!

Jamani msione watoto au watu wazima wanafanya ya ajabu! Wengi ni madini ya risasi yamejaa kwenye ubongo. Ni risasi zinazotembea!

Je ni Wapi au njia zipo Mtoto au MTU mzima anaathirika?

1. Kwa kitoto tumboni kinaweza kushiba madini ya risasi kupitia mama mjinga. Mama jinga ni lile linajipaka vipodozi vyenye madini ya Leads aka risasi. Badhi ya vipodozi hutengenezwa kwa kuongezwa lead ili kuongeza "upenyevu" (penetration) kwenye ngozi. Basi mama jinga na lenye kitumbo linapenyeza lead mpaka kwenye fuko la uzazi. Lenyewe linajiona limependezaaaa kumbe linamlisha sumu malaika! Unakuta linafakamia chips kuku kumbe shetani!

2. Lead imetumika miaka mingi kuwekwa kwenye rangi (paints). Rangi za nyumba, magari, n.k. Watoto huathirika wanapolamba ukuta au gari au chombo chenye rangi. Watoto na Watu wazima huathirika wanapopita sehemu inapopulizwa rangi. Gereji, majengo, n.k. Wapaka rangi haswaa gereji na majengo ni waathirika wakubwa! Unakuta mpaka rangi kalowa rangi na anajiona fundiiii! Lead huongezwa kwenye rangi kusaidia rangi ipenye kwenye kuta au bodi ya gari. Badala yake inapenya kwenye mwili na kuenda kwenye ubongo! Utakuta nyumba inapigwa rangi familia imo ndani na inapika au inakula! Mijinga tupu!

3. Mafuta ya petroli na dizeli. Lead huongezwa kwenye Mafuta kuongeza uwezo wa kupokea joto na kuendesha injini (kuzungusha piston). Sasa ukivuta Moshi wa gari, ukijipaka dizeli au petroli unajipaka lead! Ushaona tabia za mafundi gereji? Unajisikiaje ukivuta moshi wa gari?

4. Vigae vyao kuezekea au mabati ya Lead. Uliezeka nyumba na vigae au mabati haya vikichoka vichembe vyao lead vinaanza kusambazwa na upepo. Utavivuta na vitaingia kwenye mapafu. Ukijifanya unakinga maji ya mvua unywe basi hapo Utakuwa juna tofauti na mwehu aliyelala chini ya transfoma.

Hizi ndio njia Kuu za lead aka risasi kuingia mwilini.

Lead imeshapigwa marufuku kutumika kwenye vipodozi, Mafuta, rangi na vifaa vyao kuezekea.Lakini Waafrika watajua saa ngapi? Wako busy kujua wachezaji mpira vilabu vyote ulaya, wanamuziki wooote marekani, aina zoote za magari ya kifahari huku hâta guta hana!

Je, u-miongoni mwa huu ujinga?

Je, unajipaka marangi kwa kujifanya mshabiki sana wa mpira ? Hivi yule Yamungu wa reli morogoro nani alimpima?

Una uhakika gani mirangi unayojisiriba haina risasi? Wee jinga unajua
💄
yako kama haina risasi? Tena unalamba utadhani ice cream? Hebu acha uzungu pori. Mama yako alipaka? Mbona baba hajamuacha?

Vipodozi unavyotumia ushavisoma kujua havina risasi?

Unanunua rangi za nyumba na gari zisizo na risasi? Mafuta ya dizeli au petroli yasiyo na risasi?

Unavaa kinga unapolazimika kutumia bidhaa yenye lead?

Unapaka vipodozi vyenye risasi huku una kitumbo? Pambaaaf
 
Umeandika pumba tu, hakuna kitu kama hicho. Ubongo ni sawa na program ya computer, ukilijaza toto lako kwa program za kijinga lazima liwe jinga tu.
Mfumo wetu wa elimu unawajaza program za kutokuwa na uelewa. Na muda hausubiri. Utakuta memory nzima imejazwa pumba tu.
Hapo issue ni
Poor leadership
Corruption
Selfishness
 
Sababu zipo nyingi ya kwanza lishe!
We mtu asubuhi kala wanga tena kiporo,mchana wanga tena ugali la sembe,usiku wanga miwali ya laboratory!.
Pili umaskini
Hiyo lishe duni inatokana na umaskini mtu hawezi kula balance diet na huohuo umaskini u achangia pia watu kusoma shule za kajamba nani!.
Tatu mazingira!
Mazingira yamekuwa magumu aidha kwa kusababishwa na wenyewe ama umaskini ama ndo nature yetu humo Kuna maswala ya imani n.k

Ni kweli tunaishi ktk jamii pana kifikra n.k ndio tunatakiwa kubadilika ila sio kwa mambo yote baadhi hatutakiwi kuiga kabisa just imagine unakuwa na PhD halafu mwanaume anaoa mwanaume mwenzio huu ujinga sio wa kuachia hovyo!. Ikiwa ni PhD iwe ni PhD ya kuelimika haswa sio upuuzi.
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Walimu wenyewe hawaijaielewa elimu ya msingi wala ya secondary , unategemea nini kitatokea?
 
Labda ungesema kwanini waafrika elimu yao haiwasaidii kama baadhi ya wasio waafrika.

Hapo uzi wako angalau ungeleta maana.
 
Huo ujinga uliosemwa haujaanza kwa watoto Bali wakubwa wao ndo wamewarithisha huo ujinga, watoto nao watawarithisha watoto wao ujinga then ni mnyororo wa ujinga Hadi siku ya mwisho duniani...
 
Umeandika pumba tu, hakuna kitu kama hicho. Ubongo ni sawa na program ya computer, ukilijaza toto lako kwa program za kijinga lazima liwe jinga tu.
Mfumo wetu wa elimu unawajaza program za kutokuwa na uelewa. Na muda hausubiri. Utakuta memory nzima imejazwa pumba tu.
Hapo issue ni
Poor leadership
Corruption
Selfishness
Respect 🔥
 
Back
Top Bottom