Kwanini watu huogopa kurudi kwao wasipofanikiwa?

Kimwakaleli

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2018
Posts
7,755
Reaction score
11,737
Habari zanu wanaJf,

Kufuatana na kichwa cha habari hapo juu, nimeona niombe ufafanuzi zaidi wa jambo hili.

Nimeona watu wengi baada ya kutoka kwao na kuenda kutafuta maisha sehemu nyingine na kukosa kile walichokusudia, huamua kukaa huko bila kukumbuka hata kurudi kwa asili yao! Nawasilisha wanajamii na kazi iendelee.

Ahsanteni.
 
Tatizo kubwa hapo huwa ni aibu, ukiangalia uliondoka miaka zaidi ya kumi iliyopita, hujafanikiwa vile ulivyotaraji, ukipiga picha home kwenu (kijijini) wale ulowaacha wamejenga nyumba, wanamikiki mifugo ya kutosha, wanamikiki familia zao. Sasa wewe ukijicheck kwanza unaenda kufikia kwa wazazi pili mtonyo ulonao ni wa nauli tu. Na ukifika inabidi ushinde siku 2 tu ukipitiliza utakula nauli na hautakuwa na ubavu wa kupata nauli nyingine[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] mojawapo ya sababu ni hizo
 
Mm ndio nipo huku nyumbni kabisa nlipozaliwa picha ya kuwa nilikulia dar since 1987 na shule nkasomea huko

Kurudi kijiin ukiwa hujajipanga hata kama umekuja kutembea tu jitahidi uje na pesa zako za kula bia na kuzungusha round kadhaa

Na hizo pesa zikiisha uondoke chaap!
-
Hasa huku moshi ukiwa huna nyumba wala pesa ndio usitie pua yako huku
 
kongole sana mkuu
 
Ili mtucheke?
 
Changamoto hiyo ipo sana kwa waliotoka mkoa, ila Mimi nimezaliwa kinondoni nimeenda kuanza maisha tabata mambo yakiwa magumu kwanini nisirudi kwetu?
 
Masimango!Wanaanza kusema si bora ungebaki hukuhuku na kukutolea mifano ya waliofanikiwa,uliowaacha wakati unaondoka!
Kama mgawa rizki hajakutembelea ??kwanin wakulinganishe na mtu mwingine binadamu hapo ndipo tunapokosea jaman kila mtu na bahati yake au walitaka uwe jamabazi maana ndio kazi inayoleta mafanikio kwa haraka
Ukiisha kwa kuogopa kuonekana vipi katika jamii kisa hujafanikiwa utakufa kwa presha
Cha msingi pambana hataukijatoboa uzeen shida iko wapi alimradi huja iba cha mtu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…