Kwanini watu wengi tuliobahatika kulelewa na wazazi / ndugu tunadharau watoto wa mitaani ?

Kwanini watu wengi tuliobahatika kulelewa na wazazi / ndugu tunadharau watoto wa mitaani ?

R-K-O

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2023
Posts
482
Reaction score
2,178
Nami wala nisiwe mnafki sitaki nijifiche kwamba ni mwema kwamba niwakemee wengine

Watu wengi tumepata bahati ya kuweza kuja hapa duniani tukiwa na bahati kubwa sana ya kupata malezi ya kulishwa, kuvishwa, kuishi nyumbani na kulelewa na wazazi ama ndugu walioweza kujitwika hayo majukumu.

kuna hawa wenzetu ambao hawakuipata hio bahati, aidha wazazi walifariki bila kuwajua ndugu, waliishi na wazazi / ndugu wanaowatesa wakaamua kutoroka, kupotea mitaani wakiwa watoto, kutekelezwa mitaani, n.k.

Sasa unakuta sisi ambao tuliweza walau kupata hizo bahati za kipekee huwa hatujiongezi, tunakutana na hawa wattoto ila tunawapuuza na hata tukifatwa mtu anaweza jifanya yupo bize kumbe anakwepa maksudi kwa kuona ni kero, wengine hudiriki kuwafukuza kabisa.

Binafsi nimewahi kusaidia saidia hawa watoto ila misaada yote jumla ni kama elf 40 tu, nafsi inanisuta kamba sijawahi hata hii misaada haifikii hata asilimia 0.01 ya bahati niliyopata ya kuwakuta wazazi wangu walionilea na kunipa mahitaji kadri ya uwezo wao,

nimejikuta najiona nina ubinafsi mkubwa sana, pengine hii ndio mitihani tunayopewa pindi tukizaliwa, haijalisgi hata uende kanisani / msikitini bila kuwazingatia wenzako wa kundi hili, bado huwezi kupata idhini yale Muumba.
 
Mna dharau sana sio tu watoto wa mtaani hata watu wa kawaida ambao pengine hawakupata malezi ya wazazi wao wenyewe wakalelewa na bibi yao huwa mnawadharau sana sijui kwanin wakat pengne hata akili zote nakuzidi [emoji19]
 
Mna dharau sana sio tu watoto wa mtaani hata watu wa kawaida ambao pengine hawakupata malezi ya wazazi wao wenyewe wakalelewa na bibi yao huwa mnawadharau sana sijui kwanin wakat pengne hata akili zote nakuzidi [emoji19]
Watoto wa bibi wana nafuu mara 100 zaidi na wana mlezi, wapo kundi la waliopata malezi.

Watoto wa mtaani ni tofauti kabisa
 
Mimi ndo mana huwa nawakumbukaga na kuwazingatia.

Zile sadaka zangu za kwenye nyumba za Ibadan huwa nawapatia hawa vijana.

Kila weekend lazma nihakikishe mamfuraisha mtoto mmoja au wawili Kwa chakula na pesa.
 
Watoto wa bibi wana nafuu mara 100 zaidi na wana mlezi, wapo kundi la waliopata malezi.

Watoto wa mtaani ni tofauti kabisa
Sijasema hawana malez nimesema nao mnawaona kama sio watu yani kisa tu hakupata malez ya wazaz wake
 
Sijasema hawana malez nimesema nao mnawaona kama sio watu yani kisa tu hakupata malez ya wazaz wake


Watoto hata wakilelewa na bibi huwezi kuwafananisha na wa mitaani wanaotafuta vyakula vilivyobakizwa kwenye migahawa, kuwakuta hawajaoga wiki, wanaishi kwa magenge, n.k.
 
Watoto hata wakilelewa na bibi huwezi kuwafananisha na wa mitaani wanaotafuta vyakula vilivyobakizwa kwenye migahawa, kuwakuta hawajaoga wiki, wanaishi kwa magenge, n.k.
Broh sisemei kufananisha malezi wala sisemei watoto wa mtaani ingawa mada ni moja ila nasemea dharau wanazoonesha wale waliobahatika kupata malezi ya wazazi wote wawili kamavile wao ndo binadamu tu hope tuko pamoja now
 
wanawaita mishangazi.mishangazi nayo inawaita vijana Serengeti Boyz.

images (1).jpeg
 
Back
Top Bottom