Kwanini wazee wa zamani waliweza kuishi na ndugu wengi nyumbani, lakini kizazi hiki ni ngumu kuishi na ndugu?

Kwanini wazee wa zamani waliweza kuishi na ndugu wengi nyumbani, lakini kizazi hiki ni ngumu kuishi na ndugu?

Prakatatumba abaabaabaa

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2022
Posts
1,842
Reaction score
6,087
Nimefikiria sana mpaka nimekosea majibu, tulizaliwa watoto saba nyumbani, na ndugu waliokuja kuishi nyumbani kipindi tunakua wanafika 6, hao waliosomeshwa na mzee, japo wengine walikua wanakuja na kuondoka, mabinti wengine walikua wanakuja kujifunza cherehani na kuondoka, na sio kwamba mzee alikua na maisha mazuri hapana ya kawaida tu wala hakua mtumishi wa serikali, japo ndugu kutoka kijijini walikua hawakatiki pale nyumbani kiukweli tulikua na familia kubwa yenye upendo, mpaka sasa mzee ameshazeeka na tumeshakua watu wazima, lakini bado ndugu wapo huko nyumbani pamoja na wajukuu kutoka sehemu mbalimbali.

Nikipiga mahesabu yangu na nina watoto wawili wako primary lakini maisha yananiendesha, yaani nawaza hapa wakiongezeka ndugu wengine nitaweza kuiendesha hii familia? Sasahivi vijana wengi wanavipato lakini ni ngumu sana kumsomesha ndugu yake ukiachana na ndugu wadamu, lakini mtoto wa baba mkubwa sijui mama mkubwa upendo haupo kabisa.

Hapa nawaza wazazi walikua na upendo sana au walikua na uwezo? Au maisha yalikua cheap miaka hiyo?
 
Zamani chakula hakikuwa cha kununua.. Sehemu kubwa kilitoka kwenye mashamba na bustani za familia
Lakini tulizaliwa mjini sio vijijini, ndugu ndio walitoka vijijini kuja kutafuta maisha mjini, sema utakua sahihi kwa maana nakumbuka magunia ya mahindi na mihogo yalikua yanatoka kijijini, maramoja moja.
 
Lakini tulizaliwa mjini sio vijijini, ndugu ndio walitoka vijijini kuja kutafuta maisha mjini, sema utakua sahihi kwa maana nakumbuka magunia ya mahindi na mihogo yalikua yanatoka kijijini, maramoja moja.
Mjini huwa wanaenda kutafuta hela, na ujinga wa vijana kuendana na dunia, kijijini hakuna mzunguko mkubwa wa pesa.
 
Zamani chakula hakikuwa cha kununua.. Sehemu kubwa kilitoka kwenye mashamba na bustani za familia
Lakini tulizaliwa mjini sio vijijini, ndugu ndio walitoka vijijini kuja kutafuta maisha mjini, sema utakua sahihi kwa maana nakumbuka magunia ya mahindi na mihogo yalikua yanatoka kijijini, maramoja moja.
Wa mijini walikuwa wanatumiwa chakula cha kutosha toka kijijini na kililetwa kwa upendo mkubwa
 
Zamani chakula hakikuwa cha kununua.. Sehemu kubwa kilitoka kwenye mashamba na bustani za familia

Wa mijini walikuwa wanatumiwa chakula cha kutosha toka kijijini na kililetwa kwa upendo mkubwa
Hapo nimekuelewa, mboga yenyewe ilikua ni dagaa, shule za kata kwahiyo ilikua ni rahisi kwake kuendesha familia kubwa.
 
Watu wa zamani waliamini katika Mungu.
Watu wa sasa hawaamini katika Mungu, wamejawa na hofu ya maisha ingawa watu wa sasa ni wapenda ibada sana.
Kama maisha yamekupiga yatakuchakaza tu hata ukiwa single.
Jamani tumwamini Mungu, hawezi kumleta mtu duniani akashindwa kumpa ridhiki.
Ni mambo 2 .
1. Roho mbaya na uchawi
2. Pepo la hofu ya maisha, hili mpaka matajiri wamepigwa nalo. Mtu ana ghorofa la Billioni mbili lakini ndani ana katoto kake ka moja tu. Hata ndugu haruhusiwi kuingia kiholela
 
Back
Top Bottom