Kwanini wenye nyumba wanalazimisha wapangaji walipe Kodi kwanzia miezi 6?

Kwanini wenye nyumba wanalazimisha wapangaji walipe Kodi kwanzia miezi 6?

Nikupangishe mwezi mmoja kwa 150,000 au 300,000 ukitoka ushaharibu vitu kadhaa,mwingine akiingia lazima ufanye marrkebisho madogo.

Hio 150k yako si itaishia kwenye marekebisho? Sasa hio si biashara kichaa?

Sheria ya serikali haitakiwi kuzidi miezi mitatu, miezi 6+ inaleta utulivu kwa mpangaji na mwenye nyumba.
Kuna wengine hawatakii miez 3, unalipa miez 6 au zaidi afu unapata dharura, harudishi pesa iliyobaki.

Na ukisema utafute mtu wee mwenyewe ili ukate chako anakataa, sasa huu c utapeliii kabisaa.
 
Bora tz unalipia 6months unarelax, nchi zingine ambazo wanalipa kila mwezi lazima mwanzo kuna safety deposit depending na finishing ya nyumba unaweza lipia deposit kodi ya 6months halafu ndo unaanza mmoja mmoja. Hii yetu ni nzuri na ukifikiria mwenye nyumba ndo anabeba risk kubwa kwa system ya kodi miezi 6.
Hawapigii mahesabu uharibifu wa miundombinu wanaoufanya kwenye hizo nyumba , kuna majitu mashenzi yanaharibu mpaka rangi za kuta za ndani , yaani jitu mpaka sink za chooni linavunja ,shower , pipes ,vioo unakuta vimevunjwa ili kukomoa tu , yaani unakaa na kujiuliza hivi huyu ni mtu mwenye akili timamu au mwendawazimu ?
Na hapo ni lijitu ambalo lilikuwa linasumbua kwenye malipo ya kodi ,kila siku longolongo za nina matatizo ya kifamilia,mara nimekwama mara sijui upuuzi gani ,na anakufanyia hilo kama fadhila .
Kwa wenzetu wenye huo mfumo wa kodi kila mwezi kuna deposit ya pesa ndefu tu inafanyika kabla ya kupanga kama pesa ya uharibifu na kodi ni sharti ilipwe kila mwezi ,hamna cha nimekwama wala nina matatizo ya kifamilia , huna kodi ,wanaitwa police unafurushwa nje
 
Hawapigii mahesabu uharibifu wa miundombinu wanaoufanya kwenye hizo nyumba , kuna majitu mashenzi yanaharibu mpaka rangi za kuta za ndani , yaani jitu mpaka sink za chooni linavunja ,shower , pipes ,vioo unakuta vimevunjwa ili kukomoa tu , yaani unakaa na kujiuliza hivi huyu ni mtu mwenye akili timamu au mwendawazimu ?
Na hapo ni lijitu ambalo lilikuwa linasumbua kwenye malipo ya kodi ,kila siku longolongo za nina matatizo ya kifamilia,mara nimekwama mara sijui upuuzi gani ,na anakufanyia hilo kama fadhila .
Kwa wenzetu wenye huo mfumo wa kodi kila mwezi kuna deposit ya pesa ndefu tu inafanyika kabla ya kupanga kama pesa ya uharibifu na kodi ni sharti ilipwe kila mwezi ,hamna cha nimekwama wala nina matatizo ya kifamilia , huna kodi ,wanaitwa police unafurushwa nje
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaah
 
Mkuu mara nyinyi wenye nyumba hufanya hivo ili wasisumbuane na mpangaji kila mwezi kodi kodi hata wew kuna unafuu ukishalipa kodi una relax kdg kufatilia mambo mengne
Pamoja na hayo, mpangaji anapohama anamuachia mwenye nyumba gharama nyingi za marekebisho, sasa kama analipa kodi ya mwezi mmoja na kuhama hapo mwenye nyumba ataingia gharama kubwa ya matengenezo ilihali amepokea kodi ya mwezi mmoja.

Vv
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaah
Hamna cha nimekwama wala nina matatizo ya kifamilia kwa Landlord WA nchi za wenzetu ,nenda Kenya tu hapo ukaone moto .
Huwezi nenda Marekani ukapanga house ukamwambia Landlord " Nimekwama / Nina umwa bawasiri Nivumilie "
Ni kodi ikifika tu tarehe na hamna longolongo , la sivyo 911 inakuwa activated na landlord na polisi wanakuja kukufurusha nje kwa nguvu na unakuwa blacklisted kwenye mfumo ,Yaani inakuwa ngumu kwako kupata nyumba tena ,maana Kwa wenzetu kila kitu kiko kwenye mfumo , na wana social security number mfano pale USA ,yaani ni kama Namba ya NIDA hapa ni Bongo ila kwao ndio kila kitu , mpaka kwenye kupanga huwezi pangishwa bila hiyo number , Landlord lazima umpe hiyo number na akufanyie background check kama una historia ya usumbufu wa malipo au kero / delinquency behaviour Kwa mwenye nyumba
So kama ulimvuruga Landlord huko ulipotoka , utakuwa umeyatimba , maana taarifa zako zishaingizwa kwenye Data base na landlord wako wa zamani na polisi pia .
Kiufupi unakuwa umeyatimba na imekwisha , officially homeless
Utaishi maisha ya shida mno
 
Bora tz unalipia 6months unarelax, nchi zingine ambazo wanalipa kila mwezi lazima mwanzo kuna safety deposit depending na finishing ya nyumba unaweza lipia deposit kodi ya 6months halafu ndo unaanza mmoja mmoja. Hii yetu ni nzuri na ukifikiria mwenye nyumba ndo anabeba risk kubwa kwa system ya kodi miezi 6.
Hii ndio nzuri, mimi nime deposit ya miez 2 kodi, halafu hapo kila mwezi nampata kodi yake siku ya kuhama yeye aje kukagua nyumba yake kama kiko poa anipe yangu ya miez 2 aliyenayo nikalipie sehemu nyingine.

Nampango wakuanzia huu mfumo nitakapoanza ujenzi wa nyumba zakupangisha
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaah
Inabidi mshukuru tu hawa na landlord wenu akina mwajuma ndalafupi na mfumo huu uliopo , huu mfumo unampa unafuu sana mpangaji / tenant ni vile tu kuna ule usemi ukiwa na kitu huwezi ona umuhimu mpaka kitu hicho kiondoke
 
Wabongo tubadilike , tuheshimu biashara za watu , yaani unamvyompangisha foreigner na mbongo kuna tofauti kubwa kabisa unaona .
 
Hamna cha nimekwama wala nina matatizo ya kifamilia kwa Landlord WA nchi za wenzetu ,nenda Kenya tu hapo ukaone moto .
Huwezi nenda Marekani ukapanga house ukamwambia Landlord " Nimekwama / Nina umwa bawasiri Nivumilie "
Ni kodi ikifika tu tarehe na hamna longolongo , la sivyo 911 inakuwa activated na landlord na polisi wanakuja kukufurusha nje kwa nguvu na unakuwa blacklisted kwenye mfumo ,Yaani inakuwa ngumu kwako kupata nyumba tena ,maana Kwa wenzetu kila kitu kiko kwenye mfumo , na wana social security number mfano pale USA ,yaani ni kama Namba ya NIDA hapa ni Bongo ila kwao ndio kila kitu , mpaka kwenye kupanga huwezi pangishwa bila hiyo number , Landlord lazima umpe hiyo number na akufanyie background check kama una historia ya usumbufu wa malipo au kero / delinquency behaviour Kwa mwenye nyumba
So kama ulimvuruga Landlord huko ulipotoka , utakuwa umeyatimba , maana taarifa zako zishaingizwa kwenye Data base na landlord wako wa zamani na polisi pia .
Kiufupi unakuwa umeyatimba na imekwisha , officially homeless
Utaishi maisha ya shida mno
Kheeeeh mbna huko ni kisangaa sasa, woiiiiiih
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kumetokea wimbi la wenye nyumba kutaka Kodi ya miezi 6 kwa mkupuo wengine wanataka hadi ya mwaka mzima

Mfano Mimi nalipia Kodi 150,000 mwenye nyumba huaa hapokei Kodi ya mwezi mmoja anasema Kodi lazima nilipe miezi 6 au mwaka mmoja

Ukiangalia ulipwaji WA fedha/Kodi haumpi mpangaji guarantee ya fedha Anayolipa

Mfano mpangaji akipata dharura akitaka Kuhama mkoa hakuna kipengele Cha kurudisha Kodi.

Mpangaji akifariki kama hakua na MTU WA Karibu wakati WA kusain mikataba hizo fedha zinapotea .

Nishauri Wenye nyumba waruhusu wapangaji waamue ulipwaji wakodi ili haki itendeke.

Uliweza kujiridhisha TRA na wafanya biashara nayo Iko Je?
 
Kuna wengine hawatakii miez 3, unalipa miez 6 au zaidi afu unapata dharura, harudishi pesa iliyobaki.

Na ukisema utafute mtu wee mwenyewe ili ukate chako anakataa, sasa huu c utapeliii kabisaa.
Huyu asiyetaka maelewano ya kupata mpangaji mwingine arudishe pesa ya miezi iliyobaki ni tapeli kama matapeli wengine.
 
Hii ndio nzuri, mimi nime deposit ya miez 2 kodi, halafu hapo kila mwezi nampata kodi yake siku ya kuhama yeye aje kukagua nyumba yake kama kiko poa anipe yangu ya miez 2 aliyenayo nikalipie sehemu nyingine.

Nampango wakuanzia huu mfumo nitakapoanza ujenzi wa nyumba zakupangisha
Sema tz wapangaji wa kila mwezi lazima mpasuane vichwa, mtu anaweza kuishi miezi miwili anakupiga kiswahili kumbe anampango wa kuhama, unakuja kushtuka mtu anahama, deposit ashatumia kwenye kodi na nyumba mbovu na analia shida kama zote.
Pia kwa vipato vyetu uhakika wa tar fulani kila mwezi bila kumiss labda uanze kuomba introduction letter kutoka ofisini na slip zake za mshahara ukague kama mtoa mkopo.
Wabongo tuna utu sana, ile ya kufukuza mpangaji kama tunayoona kwa wakenya sisi bado.
 
Sema tz wapangaji wa kila mwezi lazima mpasuane vichwa, mtu anaweza kuishi miezi miwili anakupiga kiswahili kumbe anampango wa kuhama, unakuja kushtuka mtu anahama, deposit ashatumia kwenye kodi na nyumba mbovu na analia shida kama zote.
Pia kwa vipato vyetu uhakika wa tar fulani kila mwezi bila kumiss labda uanze kuomba introduction letter kutoka ofisini na slip zake za mshahara ukague kama mtoa mkopo.
Wabongo tuna utu sana, ile ya kufukuza mpangaji kama tunayoona kwa wakenya sisi bado.
Huwezi jenga nyumba yakupangisha upasue kichwa wakati wakujenga, alafu uje opasuliwe kichwa na mpangaji tena,

Jinsi mtu alivyo ndio wapangaji wake walivyo.

Usipangishie mtu nyumba ambaye hayupo kwenye ajira rasmi, one month deposit muhimu kama kishindwa kulipia kodi baada ya tareha 30 ile deposit ndio itatumika kulipia kodi huku akifanya utaratibu wakuondoka mwezi huohuo
 
Anailipa kwa kuwanunulia umeme kivipi?,hebu fafanua hapa!
ukinunua umeme mwanzo wa mwezi automatic wanakata 1500 yao ya kodi, mwaka juzi huko mpaka jana katikati ilikuwa ni 1200.

Sasa wao wakikata hiyo 1500 maana yake umeme wenu utapungua. So mwenye nyumba yake anatakia kufidia hayo makato kwa kuwanunulia umeme wa 1500 mara miezi 12.

Wa kwetu ikifika tu january anaununua kabisa wa mwaka mzima anatupa token tunaweka. Huku sisi wanaendelea kukata kodi yao kama kawaida.
 
Huwezi jenga nyumba yakupangisha upasue kichwa wakati wakujenga, alafu uje opasuliwe kichwa na mpangaji tena,

Jinsi mtu alivyo ndio wapangaji wake walivyo.

Usipangishie mtu nyumba ambaye hayupo kwenye ajira rasmi, one month deposit muhimu kama kishindwa kulipia kodi baada ya tareha 30 ile deposit ndio itatumika kulipia kodi huku akifanya utaratibu wakuondoka mwezi huohuo
Bongo ajira rasmi ni serikalini tu mkuu, hizi zingine anytym inapeperuka, mtu ana stress ya kupoteza kazi na mwezi ujao kodi hajui analipaje, daah utaua watu kwa stress.
Pia wapangaji unaowatafuta wenye ajira rasmi wengi wamejenga.
 
Kwa sababu ya njaa, anakuwa anategemea kodi ili aweze kuishi
 
Mkitaka utaratibu wa kulipa kodi kila mwezi basi wenye hela zao wataacha kujenga nyumba za kupanga muanze kulala kwenye mabanda. Hizo nyumba chache zilizopo mtazigombania sana na zitapanda bei hata kama mnalipia kwa mwezi. Nchi itapata housing crisis, viwanja vitapanda bei, nyumba zitapanda bei na uchumi utaporomoka.

Au mtalipa kwa mwezi ila kutakuwepo na security deposit, nchi kadhaa (zilizostaarabika, sio warugaruga kama bongo) huwa na mfumo huu ambapo mara nyingi security deposit inakuwa kodi ya mwezi mmoja. Mwenye nyumba ana haki ya kuzuia vitu vyako kutoka kama kuna mgogoro mahakamani. Ni mfumo wa kupoteza sana muda kama kuna mgogoro hasa kwa mifumo yetu ya kisheria.

Hakuna mwendawazimu atatoa hela yake kujenga nyumba ili awe anakimbizana na waswahili kila mwisho wa mwezi.
 
ukinunua umeme mwanzo wa mwezi automatic wanakata 1500 yao ya kodi, mwaka juzi huko mpaka jana katikati ilikuwa ni 1200.

Sasa wao wakikata hiyo 1500 maana yake umeme wenu utapungua. So mwenye nyumba yake anatakia kufidia hayo makato kwa kuwanunulia umeme wa 1500 mara miezi 12.

Wa kwetu ikifika tu january anaununua kabisa wa mwaka mzima anatupa token tunaweka. Huku sisi wanaendelea kukata kodi yao kama kawaida.

Hongera sana
 
Back
Top Bottom