Kwanini Zitto Kabwe achambue ripoti ya CAG siku ambayo Freeman Mbowe amepanga kulihutubia Taifa?

Jamani tunaelewa maana ya kulihutubia taifa au tunapachika tu. Kuongea na waandishi wa habari au press conference kwenu ina maana gani!!
 
Ndiyo siku amepata wasaa
Sisi wana taifa tuna masikio mawilimawili, moja tutamsikiliza rais wa Chadema 'akilihutubia taifa’ na lingine tutamsikiliza huyo nani aaah Zitto akiichambua ripoti ya cag.
 
Mtawala wa kinazi Mbowe atakuwa mubashara kupitia channel gani
 
CHADEMA imejaa Vi.laza wenye hasira tu! Mbowe anataka Tume huru ya Uchaguzi na blah blah kibao ambazo tumezizoea na pia anaenda ku- justify kuwa HAJAFA.

Mimi nitamsikiliza ZITTO KABWE akichambuwa ripoti ya CAG!
CHADEMA msikilizeni kiongozi wenu kwani muda mrefu hakuwa hewani!
WATANZANIA tutamsikiliza MCHUMI ZITTO KABWE kwenye ripoti ya CAG.

Hata hivyo tusipangiane kwani kila MTU anatumia vyombo vyake kufuatilia taarifa anayotaka!
Kama unafuatilia blah blah za Mbowe sawa!
Kama unafuatilia MADINI ya ZItto KABWE sawa!
 
Kwa sababu hii ni nchi huru, na kila mtu ana uhuru wa kusikiliza anayotaka kusikiliza
 
Si huwa mnataka freedom of speech mbona mnalalamika wengine(akina zitto)wakitaka haki hio hio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…