Kwanza Online TV yafungiwa miezi 11, kwa kuchapisha taarifa ya Marekani

Kwanza Online TV yafungiwa miezi 11, kwa kuchapisha taarifa ya Marekani

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Ni kwa kukiuka Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta 2018 kwa kuchapisha taarifa ya Ubalozi wa Marekani

TCRA imesema taarifa hiyo ilijaa upotoshaji na Kwanza TV waliichapisha bila kuzingatia mizania
11.jpg
12.jpg
 
Nawapongeza Kwanza Tv wametoa maeleza mazuri

Taarifa imetolewa na Ubalozi na ipo kwenye tovuti yao, wao kuitangaza ina shida gani?

Ninachokiona hapo ni kwamba wana hasira na Ubalozi ila wameshindwa cha kuwafanya sasa hasira wanamalizia kwa wengine
 
Vifungu viko wazi kwanini waandike habari za kutia hofu watanzania.
 
Duh, tuzidi kuiombea nchi yetu. Huko inakoelekea siko kabisa.
 
Leo TCRA wametangaza kuwafungia Kwanza online tv eti kwa kosa la kuripoti tahadhari iliyotolewa na Ubalozi wa Marekani kwa raia wake kuhusu mwenendo wa COVID 19 nchini. Wamefungiwa miezi 11 kwa kosa hilo walilofanya julai mosi mwaka huu. Kitendo hiki kamwe hakikubaliki.

Taarifa za Kwanza online tv siyo za kigaidi, hazihamasishi chuki wala kumtukana mtu. Kwa TCRA kufanya hivi ni kukosa uadilifu na kushindwa kusimamia misingi yake. Wamegeuka chombo cha kufanya kazi kwa kumuogopa fulani na kuabudu. Huu ni upuuzi wa kiwango chake.

Aidha lipo gazeti ambalo limekuwa likiwatukana wapinzani kila leo na juzi lilienda mbali na kumuita Lissu kuwa ni balozi wa ushoga chini. Hakuna hatua yoyote lililochukuliwa. Habari kama hizi zinahamasisha chuki na hasa ikizingatiwa jinsi TCRA walivyozifumbia macho.

Yapo mambo ambayo mtu au watu kuyafanya waone aibu, wazingatie maadili ya wao kupewa usimamizi na siyo kumuabudu mtu na kuegemea upande!
 
Tunamulikwa na taa ya dunia lakiiniviongozi wetu hawalioni hilo. Hii inaweza kuwa sababu ya wakubwa kutuingilia zaidi.Sympathy ya kwanza itatoka ubalozi wa Marekani na sijui Pompeo atasemaje.
 
Tunamulikwa na taa ya dunia lakiiniviongozi wetu hawalioni hilo.Hii inaweza kuwa sababu ya wakubwa kutuingilia zaidi.Sympathy ya kwanza itatoka ubalozi wa Marekani na sijui Pompeo atasemaje.
Hawa watawala wanakera kupita kiasi.
 
Viongozi wetu wamemua kwa makusudi kushupaza shingo zao. Kwa sasa hata hawataki kabisa kuusikia ukweli ukinukuliwa na vyombo makini vya habari hapa nchini.

Habari kama hizo zikitolewa na vyombo vya habari vya nje, hapo hugeuka kuwa balaa zaidi. Huzipuuzia pia kwa kuziita kuwa ni propaganda za mabeberu wenye kutuonea wivu, hasa kutokana na hatua kubwa za maendeleo tuliyoyafikia tangu kuingia kwa awamu ya tano.
 
Dah!..hata habari za uchaguzi hawataripoti, hii adhabu kubwa mno.
 
Mambo kama haya yanatia aibu sana...eti miezi kumi ma moja ili wajirekebishe aisee .....mbona ni vitu vya kijinga sana hivi ..
Poor TCRA
 
Back
Top Bottom