Kwasasa UTRAFIKI uko juu halafu TRA na Bandari zinafuata.

ukiona mtu anatamani kuwa traffick police ujue kapigika kweli kweli , yaani nchi imekua ya hovyo sana hiyo, kuna watu wana deals zao za halali na za maana wanapiga hela vibaya , sasa wengine mnawaza kubet tu na kunywa energy maisha yatabadilika lini? vijana wa hovyo wanaongezeka kila uchao.
 
Pale mwandege kila daladala inatoa buku tatu huku temeke kilwa road kila daladala inatoa buku mbili hapo bado malori ya mizigo na canter.......
Hizo daladala njia hiyo hata 100 hazifiki. Na sio kila wakipita wanalipa ni mara moja tu kwa siku labda akakamatwe njia nyingine. Na sio kila lori wanakamata ni za kuotea pia, wangekua wanakamata kila lori kwanza hiyo jam yake ingeleta ugomvi traffic wenyewe watajikuta lupango. Watu wanafikia hadi hatua ya kujidanganya eti traffic analaza milioni kwa siku 😂😂😂😂
 
Njoo pm nikupe info kamili.
Nikikupa code hapa wanoko watasanukia viwanja.
 
Niko ilala kwaiyo katikati ya mji Kuna barabara magari hayipiti ili yamkimbie trafiki upo Dar sehemu gani mkuu?
Katikati ya mji trafiki kusimamisha gari ni labda uzingue kwenye taa au kwenye zebra. Ni nadra sana kukuta wamejazana kukusanya maokoto kama njia za pembezoni kama za kinyerezi,goba etc. Hapa Dar unaweza endesha gari 2 years na usiwahi simamishwa na traffic kwa maeneo ya town unless uzingue kwenye taa au zebra wakakuotea, tofauti na mikoani..ndio maana nikahisi upo mkoa
 
Sasa na utuambie nawe kama mla kwa urefu wa kamba😁
 
NI VYEMA TUKAJIFUNZA TABIA NJEMA KIMAADILI NA TUWE NA HAMU YA KUONA TAIFA LETU LINANYANYUKA KIMAENDELEO KWA KUKWEPA KUTAKA KUJINUFAISHA WENYEWE PALE TU UNAPOAMINIKA MAHALI JITAHIDI KUWA MUADILIFU,.PIA SIO SAHIHI KUZIORODHESHA TAASISI KAMA HIZO HAPA, KAMA UNA USHAHIDI WA HAYO ULIYOYASEMA NENDA KASHTAKI KWENYE VYOMBO HUSIKA #KATAARUSHWA
 
Hili jambo siyo sahihi. Tujitahidi kutoa taarifa sahihi na changamoto sahihi ili tuweze kutatua.

Sent from my SM-A235F using JamiiForums mobile app
 
kwa maelezo yako tra kuko vizur
kama unaweza kutoka na 10m per day hiyo namba moja kabisa
afu hao tpa namba 9 namba 10 trafiki



ila tu nikwambie kwa sasa mfumo wa kodi ambao hatukabidhi mkononi
10m ni uingo wa karne

control number zimeharibu sana

hiyo 10 labda kama utakuwa unaongelea wale matop huko juu ila sio mikoani na vituo vya kodi mtu wa kawaida hakunaaaaaaaaaaaaaaa
 
vijana muache tamaa kuna watumishi katavi wa uhasibu wapo rumande toka mwaka jana mwezi 7 kwa kosa la wizi wa pesa ya selikal


mpaka sasa na wengine mateso wanayopitia sio ishu kabisa ni mabaya

madeal haya selikal skuiz inaona sana mifumo imekuwa mingi
 
NI VYEMA TUKAJIFUNZA TABIA NJEMA KIMAADILI NA TUWE NA HAMU YA KUONA TAIFA LETU LINANYANYUKA KIMAENDELEO KWA KUKWEPA KUTAKA KUJINUFAISHA MWENYEWE PALE TU UNAPOAMINIKA MAHALI JITAHIDI KUWA MUADILIFU,. #KATAARUSHWA
Huko PCCB kwenyewe watu wanatembeza rushwa ili mafile yao yazimwe.
Ukishindwa kupigana nao jiunge nao .
 
Halmashauri njaa kali ukiibila laki 5 tu mpaka baraza la madiwani watajua
 
They're finding short term pleasure for long term painful hao ndio vijana wa Tanzania wanaoamini kwamba ukicheza buku kwenye mchongo pesa basi unapata million 10 na friji na tv.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…