Kweli biashara ya ndege ngumu, Kenya Airways na ukubwa wote wamechemka. Ruto kuiuza kwa Wamarekani. ATCL vipi?

Kweli biashara ya ndege ngumu, Kenya Airways na ukubwa wote wamechemka. Ruto kuiuza kwa Wamarekani. ATCL vipi?

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Rais wa Kenya, William Ruto amekutana na viongozi wakuu wa shirika la ndege la kimarekani la Delta katika mpango wa kuwauzia hisa zote 48.9% zinazomilikiwa na Serikali ya Kenya kwenye shirika hilo.

Kenya Airways imekuwa ikitegemea hazina ya Kenya kuweza kujiendesha huku kipindi cha Januari-Juni ikiwa imerekodi hasara ya dola milioni 82 na kipindi kama hicho 2021 kikitoa hasara dola milioni 95.8.

Kwa upande wa Tanzania, ripoti ya mwisho inayopatikana inasema ATCL imepata hasara ya TZS bilioni 36 mwaka 2020/21 kutoka bilioni 60 mwaka 2019/20. Kwasasa shirika hilo ndege zake kubwa inazoziendesha zimepumzishwa huku moja ikishikiliwa kwa madeni.

Serikali chini ya Rais Magufuli iliamua kulifufua shirika la ndege la Tanzania lililokuwa hoi bin taaban kwa kununua ndege mpya na kuliazima shirika hilo.
 
Kwa upande wa Tanzania, ripoti ya mwisho inayopatikana inasema ATCL imepata hasara ya TZS bilioni 36 mwaka 2020/21 kutoka bilioni 60 mwaka 2019/20. Kwasasa shirika hilo ndege zake kubwa inazoziendesha zimepumzishwa huku moja ikishikiliwa kwa madeni.[emoji2827]
 
Hayo mambo ya biashara ya ndege waachiwe sekta binafsi, fastjet ilikuwa imekuja juu na kuufanya usafiri wa ndege kuanza kutumiwa na watu wengi kwani nauli ilifika hadi elf 40, kama Serikali inaona sifa kumiliki ndege wauzie sura hiyo ndege ya Rais iliyonunuliwa kwa watu kula majani enzi zileee.....
 
Ni Habari njema, huoni kuwa ni Maendeleo? Delta waki-invest Kenya Airways how big the airline will be? More revenue for Kenya, bigger worforce guaranteed by first World Economy growth! Stop your communist Thinking! The biggest investor in China is also US of America, what is your problem?

Fikra za mwenyekiti zimewaharibu bongo zenu, you need change, Serikali haiwezi kufanya biashara iwaachie wananchi!!!
 
ATCL imepata hasara ya TZS bilioni 36 mwaka 2020/21 kutoka bilioni 60 mwaka 2019/20. Kwasasa shirika hilo ndege zake kubwa inazoziendesha zimepumzishwa huku moja ikishikiliwa kwa madeni.
Mbona kuna moja inapita hapa mjini mara kwa mara hiyo yenyewe imekataa kupumzika?
 
MWENDAZAKE alifikiri biashara ya ndege ni kama Bodaboda jioni unaletewa hesabu...huku kwenye ndege kunahitaji uwekezaji wa muda mrefu
Unajua maana ya Ndege? kuwa na ndege ni "class"; unajua "Status" ya Pilots?
Ni vibwengo tu ndiyo hawajui.

Magu alikuwa katili, ila kwenye Vision ya Tanzania among the greatest Presidents: JKN, Mkapa!!
 
Ni Habari njema, huoni kuwa ni Maendeleo? Delta waki-invest Kenya Airways how big the airline will be? More revenue for Kenya, bigger worforce guaranteed by first World Economy growth! Stop your communist Thinking! The biggest investor in China is also US of America, what is your problem?

Fikra za mwenyekiti zimewaharibu bongo zenu, you need change, Serikali haiwezi kufanya biashara iwaachie wananchi!!!
Ila serikali ina takiwa ilete maendeleo kwa kodi na mikopo bila kusahau misaada??? Kufanya biashara hapana!

Tuna ambiwa tuna mali, serikali ina zifanyaje hizi mali? Tuwape wawekezaji, tuziache na serikali itapataje pesa??

Serikali ina nunua mahindi 2000/- kwa kilo na kuja kuya toa kama msaada au kuuza kwa 1000/- kwa wananchi wake... kesho hawana pesa ya kununua au kujiendesha na kuanza kutafuta pesa za kununua mahindi na kuhifadhi gharani...
 
Rais wa Kenya, William Ruto amekutana na viongozi wakuu wa shirika la ndege la kimarekani la Delta katika mpango wa kuwauzia hisa zote 48.9% zinazomilikiwa na Serikali ya Kenya kwenye shirika hilo...
Binafsi sipingi kununua ndege kwani nayo ni kama nembo ya Nchi ila cha muhimu
Kuendesha Shirika la ndege kunahitaji watu wa marketing ambao ni creative, aggressive na profit oriented na wanaofanya maamuzi ya haraka na sio kuendelea kupeleka ndege kwenye miji/viwanja vya ndege ili kufurahisha watu na sio kupata faida.

Tunahitaji watu ambao ni very creative na focused kwenye Biashara na sio hawa wa kucopy na kupaste
Muhimu zaidi; huwezi kuendesha Biashara ya ndege ya kimataifa bila kupata Wabia mathubuti (code share)
Yaani unapokea wageni wa ndege A unawapeka sehemu B. na ndicho kenya wamefanya (ila tofauti yake ni kuwauzia kabisa hisa?) Ukijifanya kusimama kivyako vyako, hutoboi.

ATC Ikiwashinda waipe private sector waone kama haitasimama ila wajue kwa Tanzania route zitabakia kama tatu tu ambazo zinafaida kubwa inayomezwa na route nyingine zisizokuwa na abiria/zinazoendeshwa kwa hasara kubwa. kwa mtazamo wangu, route zenye faida kubwa ni;
1. Kilimanjaro/Arusha to Dar, 2. Dar to Mwanza 3. Dar/Dodoma to Kigoma na pengine moja ya kusini.
 
Rais wa Kenya, William Ruto amekutana na viongozi wakuu wa shirika la ndege la kimarekani la Delta katika mpango wa kuwauzia hisa zote 48.9% zinazomilikiwa na Serikali ya Kenya kwenye shirika hilo.

Kenya Airways imekuwa ikitegemea hazina ya Kenya kuweza kujiendesha huku kipindi cha Januari-Juni ikiwa imerekodi hasara ya dola milioni 82 na kipindi kama hicho 2021 kikitoa hasara dola milioni 95.8.

Kwa upande wa Tanzania, ripoti ya mwisho inayopatikana inasema ATCL imepata hasara ya TZS bilioni 36 mwaka 2020/21 kutoka bilioni 60 mwaka 2019/20. Kwasasa shirika hilo ndege zake kubwa inazoziendesha zimepumzishwa huku moja ikishikiliwa kwa madeni.

Serikali chini ya Rais Magufuli iliamua kulifufua shirika la ndege la Tanzania lililokuwa hoi bin taaban kwa kununua ndege mpya na kuliazima shirika hilo.

tupe hasara ya ndege za emirates na utupe hasara za ndege ya Qatar air, kama kuendesha ndege ni hasara kampuni mbili hizi zingeuza ndege zake
 
Back
Top Bottom