Kweli Ndoa yataka Moyo.....

Kweli Ndoa yataka Moyo.....

Nakubaliana na hoja yako ninachotaka mimi sio kushindana na huyo ex wake kwenye manjonjo ama la,nataka heshima yangu irudi na ule upendo ulionidrag hapa uendelee kugrow....sitakata tamaa ntapambana tu ila naamini machozi yangu hayataenda bure kuna siku Mungu atanilipia tu.Mume wangu ntaongea nae kwa adabu na upole na kirafiki juu ya hili jambo na kama kuna kitu anaona siko swa ntamuomba anieleze wazi ili nijirekebishe na ntamuomba tuweke mikakati ya pamoja katika kuinusuru ndoa yetu ikiwa ni pamoja na kukata mawasiliano na huyo ex maadamu hayana faida kwetu zaidi ya kuharibu tu...Nakubali kuna ex wanaweza kuwa rafiki kwa maana ni wastaarabu na wanajua nyajibu zao ila wengine wako katika kuharibu tu furaha za wenzao na si vinginevyo,nitampa ushauri mzuri ambao naamini utakua na matokeo chanya baina yetu wawili
 
Pole sana dada,inaonekana huyo mumeo anshindwa kufanya uamuzi mgumu wa kumweleza huyo ex-wake juu ya kuheshimu ndoa yenu,pia huyo dada hana adabu,kwani kutembea na mume wa mtu ndo atoe siri,ina maana hata angekuwa na mume wake angekuwa anaanika yale yote wanayoyafanya kwenye mitandao?kwenye mitandao watu tunasaidiana tu kwa mawazo lkn huwezi anika siri za kitandani kwako kama wewe ni mtu una akili timamu.huyo mumeo angekuwa na akili nzuri leo leo angempiga chini kwani ipo siku atamdhalilisha kwa kumtoa picha za uchi ambazo atakuwa amempiga kwa kujua au kutokujua,kwani hapo anatembea na zuzu.
Wewe mpiganie mumeo kwa Mungu kwa maombi na kufunga hasa kipindi hiki cha kwaresma naye atakujibu.
Nashukuru kwa ushauri...utafanyiwa kazi
 
Huu upendo wenu wa kileo wa ma - twirra... na manini sijui, tupa kule......Huyo baba mwenye nyumba siamini kama kweli huyo bi mkubwa amebaki kama rafiki tu...mbona sioni mipaka mie?
 
Mkuu nakukubali kwa ushauri wako na naamini uko sahihi,nakiri kuwa nitaplay my part as a married wife na daima kuwa upande wa mume wangu but i wont allow tena huyo EX aitese ndoa yangu,naamini ntachukua hatua yakinifu katika kulitatua hili tatizo....

A good start! ...the change starts with you! kila la kheri, na mwenyezi mungu atakusaidia.
 
vishawishi vingi plus kufosiwa kufunga ndoa ndo usiseme
usikute huyo mwanamke alilazimisha ndoa na si mapenzi ya mwanaume mwenyewe

Labda useme hivyo. Eti true_diva ndoa yako ilikuwaje!??
 
Last edited by a moderator:
Pole mrembo,huyo mwanamke asikushughulishe sana mpaka ukakosa amani na ukaanza kugombana na mumeo unaempenda,
Kumbuka kua angekua anadhamani asingekuoa wewe yeye akamuacha,ila ukisikia wale adui hana sababu ndio huyo mwanamke, zidisha manjonjo kwa mumeo mpe mambo mapya kama unatokea pwani nadhani utanielewa,jengine wacha kabisa kupekura cm yake wala kutaka kujua nani katuma sms utashindwa kumeza mengine, Kumbwa zaidi Mtangulize mungu kabla ya chochote na zidisha sala za usiku amka usiku mwingi omba na ulie kutoka moyoni amini mungu atakusaidia...
 
Ndugu zanguni yamenikuta na naomba ushauri wenu,Mimi ninaishi na mume wangu yapata miaka miwili sasa,nina mpenda sana Mume wangu na ninaamini kuwa naye ananipenda pia.Ila kuna tatizo linanisumbua sana juu yake ambalo linanipa wasiwasi kiasi kwamba nashindwa kuelewa hatma ya mahusiano yetu ya ndoa kwa maana ya kwamba nahofia yasije yakaingia shubiri na ile imani nlionayo juu yake ikateteleka.Ni hivi kabla ya kunioa mimi aliwahi kuwa na mahusiano na wanawake wengine ila mwanamke wa mwisho ambaye aliachana nae amekua akiendelea kuwasiliana na mume wangu na kila ninapohoji juu ya hilo Mume wangu hunijibu kuwa hauna kitu kinachoendelea baina yetu ni rafiki yangu tu wakawaida na hana shida yoyote na sisi kwanza huwa anapiga simu na kutuma meseji za kutujulia hali,anyways nimejitahidi sana kuwa na mtizamo chanya na kuuambia moyo wangu uamini hivyo.Ila siku zinavyokwenda nikaona mazoea yanakua sio mazuri kwa maana wakati mwingine humpigia simu ana hutuma meseji humueleza mume wangu kuwa amemmiss sana na anataka kuonana nae na vitu kama hivyo.Nlimwambia mume wangu mawasiliano na huyo mpenzi wako wa zamani hayanibariki hata kidogo naomba uwe na mipaka na ikibidi uache kwa maana yananiumiza mimi zaidi,aliniahidi kufanya hivyo na kweli kwa kipindi fulani kazi ilipungua ila sasa leo ametuma tweets kuhusu mume wangu kwenye mtandao wa twitter kitu ambacho kimeniuma maana anaeleza jinsi anavyofurahia tendo la ndoa na mume wangu na baada ya kuliona hilo nkampigia mume waqngu kumweleza akaniambia atampigia simu kumsema juu ya hilo na kumuonya.Badala yake kilichotokea yule mwanamke alituma tweets za kunitukana na kunidhalilisha mimi kitu ambacho kinaniuma sana kwa maana mume wangu anasema yule mwanamke ni rafiki mzuri tu na hana shida hata kidogo.Nisaidieni ushauri ndugu zangu je niendelee kuvumilia hayo yote yanayojitokeza na kuamini maneno ya mume wangu kuwa huyo mwanamke hana shida na sisi ama nifanyenye?Naomba ushauri wenu katika hili.....

Ulimpate huyu mumeo? Si kwamba ulimpora kutoka kwa mdada mwingine? Auaye kwa upanga naye atauawa kwa upanga.
 
unatakiwa uwe na roho ngumu ya kuamua
usifanye hamaki isipokuwa umshauri Baba mwenye nyumba kuwa bora muwe wote pamoja awe na wake wawili
Ukimueleza hilo lazima ataruka kutaka kujua kulikoni ila wewe usioneshe kuterereka hapo lazima ajiulize maisha haya na wake wawili yatakuaje? akianza kukubali ujue unasaidiwa na mwenzio hapo itakuwa akili kichwani mwako,
Kwanza jaribu kuonesha upendo zaidi ili asahau huko nje inawezekana unashindwa na ujanja fulani ndio anakwenda nje kuutafuta,
Jaribu kuonesha upendo zaidi ili asahau nje hata akipigiwa simu huko nje wewe usipokee na usitazame simu yake jaribu kumpa vitu kila siku muekee maji ya kuoga na mengine, usafi wake uwe muhimu na wako pia usimpigie simu kila wakati muachie yeye apate mtihani
 
Kuvumilia...?yaani usilale mdogo wangu,hapo mtafute kwa hudi na uvumba,halafu mchape na kumtoa shoo yote usoni,hakuna kuremba hapo,ni kichapo tu..kama humwezi kodi watu...na hicho kidole anachotweet nacho kitie alama...akiona tu,atakumbukakichapo.wanawake wa mujini noma:crying:
 
hata mimi x wangu ni rafiki yangu saaanaaaa........
mwanzo hakuamini kama sitaweza kumpa kitu baadae kakubali matokeo, maana nilimwambia kabisa siwezi kwenda beyond stories...... kama anataka zaidi ni bora tusiwasiliane kabisaaaa, kila mtu aishi kwa amani nyumbani kwake. akiangalia hawezi kunipoteza, maana namsaidia sana kwa maushauri na kila kitu..... in fact hata kwenye kuijenga ndoa yake ambayo ilikuwa inayumba mara kadhaa...... tumebaki kuwa marafiki na hakuna feelings zozote (to me)

Walau, @fp
 
Muite mmeo na uwe na kikao nae serious umuulize nini zaidi anachokipata toka kwa huyo dada ambacho we haumpi.
It is very obvious that mmeo anafanya sana tendo hilo na huyo ex a.k.a kimada also known as concubine.
Sikatai kwamba prayer has a powerful way of resolving all the mysteries ila kumbuka sometime we tend to be spiritual in the areas where we are supposed to be natural and act wisely. Unaweza kuta huyo mmeo anapewa mapenzi extra kuliko unavyompa ndo maana labda kila napokumbuka kitu fulani ana resolve kwenda ng'ambo ya pili.
Be serious ukae na umuulize maswali magumu na akupe majibu thabiti. One to one on a serious note, what is he given by that concubine that you can not give and so on and on. When you learn to be open with your spouse even in little issues it will help you strengthen communications between you two.
Yawezekana ni tendo lenyewe au chakula au bashasha kadhaa za kimapenzi.
Ukishindwa tafuta wasimamizi wenu wa ndoa ukishindwa ipeleke kwa wazazi. Kwa msaada zaidi PM and I will try to hel as much as I can.
 
Walau, @fp
ha ha haaa, Kaizer naogopa sana kuusemea moyo, nisije nikajisemea hatuna mafeelings kumbe mwenzangu anakufa kiume, lol! ninachoshukuru tu anakubaliana na rules & regulations zangu..... mengine hayanihusu
 
Last edited by a moderator:
.....Kamanda TIMING big up sana kwa kuliona hili. Huyo ex- g'friend mpaka ana tweet mambo ya chumbani inajionyesha yupo desparate 'kuichokonoa' ndoa ya huyu mdada.

......mwanaume 'ustaarabu' wake kwenye case hii unaweza kumponza. Anayumbishwa na mkewe hapa!

......dada mwenye thread hii, hebu nawe uwe na busara.Unapomshinikiza mumeo amkanye ex wake, hujui unamsukumia upande ule pia?

Unachokozwa nawe unachokozeka? badala ya kuimarisha nyumba yako weye unaibomoa. Mumeo kakuchagua wewe na anataka utulivu bana.... Msaidie mumeo kwa kumuonyesha hajakosea kukuoa na hubabaishwi na huyo 'reject!'
Mwenye maskio na asikie, ukubwa dawa swahiba!
 
Huwa narefer story yako kila ninapokumbana na issue kama hizi; and l think, ilikutokea hiyo ili uweze kuwasaidia wengine wenye shida za namna hiyo.
Basi once again, nakuomba; nenda naye another stage further, akupe contacts zake uendelee kumjenga zaidi (simu etc). She seems to be somewhat naive and too nice (jinsi hata anavyojibu post "......nimekuelewa nitafanyiakazi...." sort of majibu) so she need a strong woman like you to mentor her.
Amina mpendwa ama hakika nitaweka maombi maalumu juu ya hii changamoto nliyonayo na kutoa sadaka kwa bidii na nina amini Mungu atakutana na haja ya moyo wangu hata katika kipindi hiki cha kwaresma...sina budi kumshukuru Mungu kwa kila jambo na kupiga moyo konde na kusonga mbele nikishika silaha za upendo,kusamehe na kuzidisha ibada kwa mwenyezi Mungu
 
ha ha haaa, Kaizer naogopa sana kuusemea moyo, nisije nikajisemea hatuna mafeelings kumbe mwenzangu anakufa kiume, lol! ninachoshukuru tu anakubaliana na rules & regulations zangu..... mengine hayanihusu

yeah @FP, thats why I was happy kuwa you were careful not to generalize. See, quite a number of relationships end in such a way that one side is still wanting.....and thats made even worse when you have regular communications, in a belief that there is 'no more chemistry'.....and alas, one side is burning inside lol!
 
Amina mpendwa ama hakika nitaweka maombi maalumu juu ya hii changamoto nliyonayo na kutoa sadaka kwa bidii na nina amini Mungu atakutana na haja ya moyo wangu hata katika kipindi hiki cha kwaresma...sina budi kumshukuru Mungu kwa kila jambo na kupiga moyo konde na kusonga mbele nikishika silaha za upendo,kusamehe na kuzidisha ibada kwa mwenyezi Mungu
true_diva,

Mosi, pole sana kwa mksa huu ulipo hivi sasa.
Pili, ningekushauri pia katika maombi yako, usome sana Zaburi, hasa ya 35, 64 na 91.
Tatu, naomba wewe mwenyewe ukae chini, ujichunguze,,,,jiweke mbele ya kioo ikibidi, ujiulize kwa uaminifu kabisa, kama binafsi hujachangia kwa namna yeyote katika hili linalokutokea? Jibu utalopata, litakuongoza nini cha kufanya pamoja na sala.
Nne, Kwa namna yeyote ile usifanye nguvu kwenye hili suala, yaani usitumie mabavu au lugha ya kejeli/dharau/ugomvi, kwani hii itazidi kulikuza tatizo na sio kulipunguza
Tano, Hili jambo ni la kwako na Mume wako, na sio mtu mwingine YEYOTE. That way, utalimalia kistaarabu na kulinda heshima ya ndoa yako.

Ni hayo tu kwa sasa
 
Last edited by a moderator:
yeah @FP, thats why I was happy kuwa you were careful not to generalize. See, quite a number of relationships end in such a way that one side is still wanting.....and thats made even worse when you have regular communications, in a belief that there is 'no more chemistry'.....and alas, one side is burning inside lol!
nalijua hilo Kaizer ndo maana sikutaka kumsemea.....
tulishaliongea sana na kufikia conclusion tuliyofikia for the sake of friendship. tumegundua kwamba we have so much to benefit from each other ukiondoa ....., ndo maana tukaona isiwe tabu, tuchukuliane tu hiyo mizigo na maisha yasonge mbele. ukizingatia kila mtu anapata hicho kingine huko aliko, lol!
 
Last edited by a moderator:
You are fine ila huyo mmeo ni cheater mzoefu wala hili halina ubishi. Issue ni je anaweza badirika? Cheating ni trait na ni tatizo sawa na wizi. Mwenye trait za uwizi hata awe tajiri ataiba tu. Na cheater hata umpe nini atacheat tu kwani yeye kitendo cha cheating ndo starehe kwake si aina ya penzi analopata! Mhh hata humu ndani bila shaka umeshawssikia sana watu wakisema eti penzi la wizi tamu! Hujasoma hiyo humu? Kuiba penzi ndo amachovutiwa nacho mmeo. Basi.
 
Usingekua twitter usingejua yote hayo. Ukimchunguza sana bata humli. Pole sana dada.
 
Back
Top Bottom