Kweli tunapiga vita ugaidi au ni vita dhidi ya uislam?

Kweli tunapiga vita ugaidi au ni vita dhidi ya uislam?

Status
Not open for further replies.
[
QUOTE=zomba;8200550]
relviolence.jpg
[/QUOTE]
Pamoja na Data hizi eti kuna Waislamu wanatishia kuanzisha Vita.Chondechote ndugu zanguni vita sio lelemama,Wenzenu wanauzoefu wa kutosha kivita,mtakwisha.Wote tushirikiane kuutokomeza Ugaidi na Magaidi ili Dunia iwe sehemu salama ya kuishi.
 
Kumbe mmepewa Nyenzo za kujikomboa,kwa nini hamzitumii?Lianzisheni ili mtutawale.Ila kumbukeni wenzenu akina AL QUIDA,BOKO HARAM,AL SHABAB,HEZBOLLAH n.k.wanataabika.


Mkuu samahani! Ebu Tujaribu Kua na kuvumiliana kidogo!
 
Hizo ni Hadithi ndugu yangu,Hata Wakristo ukiwauliza watakwambia Mbingu na Dunia zitapita lakini NENO Litasimama.Wakristo walishaona Mapungufu ya Nyuma na wakawekeza kwenye ELIMU.Sasa nyie na kachuo kenu Kamoja mlikopewa na Mkristo mnategemea kushinda?Kama ni Historia ya Vita usianze 622AD,anza kuanzia mwanzo wa Ulimwengu uone YEHOVA anavyojiita kwamba yeye ni BWANA WA VITA.Wakristo hushindwa vita pale tu wanapomuhasi MUNGU(YEHOVA) na si vinginevyo.Wameshawahi kushindwa vita vingi sana na sio hiyo tu unayoijua wewe.Kitu pekee unachotakiwa ujue ni kwamba Mungu wa kweli(YEHOVA) hashindwi na hapiganiwi
The crusade were a series of Roman catholic holywar to wrest control of the holyland from muslim.They produced some of the bloodiest battles in history.

They are called the christian crusade but that label itself is a deception.they were primarily catholic crusade.
In 622AD,catholic fought and WERE DEFEATED IN A CRUSADE AGAISNT PERSIA AND THE JEWS.some 60,000 catholic were killed and 35000 enslaved.
The fall of Jerusalem left the catholic SHOCKED AND MOURNING.
Some historian consider this the first crusade.
endelea.
https://www.thetrumpet.com/article/1153.27033.68.0/world/war/the-coming-war-between-catholicism-and-islam
 
Hizo ni Hadithi ndugu yangu,Hata Wakristo ukiwauliza watakwambia Mbingu na Dunia zitapita lakini NENO Litasimama.Wakristo walishaona Mapungufu ya Nyuma na wakawekeza kwenye ELIMU.Sasa nyie na kachuo kenu Kamoja mlikopewa na Mkristo mnategemea kushinda?Kama ni Historia ya Vita usianze 622AD,anza kuanzia mwanzo wa Ulimwengu uone YEHOVA anavyojiita kwamba yeye ni BWANA WA VITA.Wakristo hushindwa vita pale tu wanapomuhasi MUNGU(YEHOVA) na si vinginevyo.Wameshawahi kushindwa vita vingi sana na sio hiyo tu unayoijua wewe.Kitu pekee unachotakiwa ujue ni kwamba Mungu wa kweli(YEHOVA) hashindwi na hapiganiwi
yehova is nothing but a murderous pagan god,he was a cold blooded killer and it is all well documented in the bible.
 
[
QUOTE=zomba;8200550]
relviolence.jpg
Pamoja na Data hizi eti kuna Waislamu wanatishia kuanzisha Vita.Chondechote ndugu zanguni vita sio lelemama,Wenzenu wanauzoefu wa kutosha kivita,mtakwisha.Wote tushirikiane kuutokomeza Ugaidi na Magaidi ili Dunia iwe sehemu salama ya kuishi.[/QUOTE]
wana uzoefu kina nani,au wakristo?.sasa kama ni kweli si mkawasaidie ndugu zenu kule syria mbona kila siku wanachinjwa?.au pale irag mbona jana tu wameuawa karibu 50,huo uzoefu wenu wa kivita uko wapi?.au ndo ule wa kuogopa kupigana na kutuma drone zisizo rubani kwenda kuua watu kwenye mikusanyiko ya harusi?
 
Ndio maana ninasema elimu inaitaji ili watu wenye fahamu kama za kwako waelewe maana hasa ya aya kama hizo na vipi zinapaswa kufanyiwa kazi.

Hapa kwenye ELIMU tupo pamoja.Elimu itawasaidia kujua Adui sahihi wa Waislamu na Kupambana naye.Hili swala la kuilaumu Serikali ya CCM inakumbatia MFUMO KRISTO na wakati huohuo mnaendelea kuipigia Kampeni Misikitini iendelee kutawala inaonyesha jinsi gani mnavyotumika na Msivyokuwa makini na Malengo yenu.
 
yehova is nothing but a murderous pagan god,he was a cold blooded killer and it is all well documented in the bible.

Mkuu nakuomba tafadhali Kwani usipomjibu Huyu mtu utapungukiwa nini?

Turudi kwenye mada!
 

Hii umeitoa wapi?

Lakini kibaya zaidi haieleweki

HiviWar maana yake nini?
Political violence ni kitu gani?

Nimekuuliza hayo maswali kwa kuwa umeweka hiyo kitu yako halafu umeandika kufuatia rangi za kwenye mduara wako kuwa "Killed by Christian" "Killed by Muslims"!

Inawezekanaje jambo liwe political halafu wakati huohuo liwe la kidini?
 
The crusade were a series of Roman catholic holywar to wrest control of the holyland from muslim.They produced some of the bloodiest battles in history.

They are called the christian crusade but that label itself is a deception.they were primarily catholic crusade.
In 622AD,catholic fought and WERE DEFEATED IN A CRUSADE AGAISNT PERSIA AND THE JEWS.some 60,000 catholic were killed and 35000 enslaved.
The fall of Jerusalem left the catholic SHOCKED AND MOURNING.
Some historian consider this the first crusade.
endelea.
https://www.thetrumpet.com/article/.../the-coming-war-between-catholicism-and-islam

Wewe hujui Mbinu mbalimbali za Kivita.Kurudi Nyuma na kujipanga inakubalika Vitani.Wenzenu sasa wana Drones,wakati nyie bado mnafundisha Watoto JIHAD kwa kutumia Majambia.
 
Tofauti na wafuasi wa dini zingine waislaam wengi hua tayari kutetea lolote linalofanywa na watu chini ya bendera ya uislaam. Ni vigumu kukuta muislaam akiwapinga watu wa dini yake wenye harakati za kuvunja amani ya nchi eti tu kwa kuwa wamevaa kanzu/vilemba na kufuga midevu.
 
Mkuu nakuomba tafadhali Kwani usipomjibu Huyu mtu utapungukiwa nini?

Turudi kwenye mada!
sikujibu kwahisi ndo reality..ntaleta dondoo toka ndani ya bible nikipata mda.
 
Wewe hujui Mbinu mbalimbali za Kivita.Kurudi Nyuma na kujipanga inakubalika Vitani.Wenzenu sasa wana Drones,wakati nyie bado mnafundisha Watoto JIHAD kwa kutumia Majambia.
by drone una maana wakristo wa marekani...okay,si wao peke yao wenye nazo.nakwambia hii game sio ya kitoto,weka ushabiki pembeni.

Then jiulize kwanini sharia inaanza kutumika United kingdom?.maanake ni kuwa islam is gaining power in the westchristian nations while dying in middle east.
 
Wewe hujui Mbinu mbalimbali za Kivita.Kurudi Nyuma na kujipanga inakubalika Vitani.Wenzenu sasa wana Drones,wakati nyie bado mnafundisha Watoto JIHAD kwa kutumia Majambia.


Mkuu kuna vitu vingi Tunataka kujifunza toka Kwa wenzetu! Ebu Jaribu kuweka uvumilivu mbele!

Samahani!
 
sikujibu kwahisi ndo reality..ntaleta dondoo toka ndani ya bible nikipata mda.

Mkuu hii ligi yote ya nini!?

Kuna vitu muhimu tunasubiri Kutoka Kwa Mwalimu CHAMVIGA na Bilal bin Rabah! Sasa Kwa mnavyoelekea hivi mnaturudisha Kule nyuma tuliko toka ambako tumeshaweka sawa!

Tafadhali Mkuu nakuomba!
 
Sio kweli kwamba kule kilindi Tanga kulikua au kuna al shabab. Ukitaka kujua anza kutafuta nini ilikua sababu ya operation ile hatamu.
Chanzo cha vurugu ni ugomvi wa mgambo na wakulima na wafanya biashara wa hiliki.mgambo walikua wanalazimisha kwa kutumia nguvu ulipaji wa kodi haramu kwa mazao.na inaonekana ni mazoea yao kutumia mwanya wa kuvaa magwanda yao na kuwaonea raia wasi na hatia. Wananchi kwa pamoja walikataa uonevu ule hali iliyopelekea mapambano na kusababisha kifo cha mgambo mmoja na wananchi kadhaa kujeruhiwa.
Tukio lile likafika polisi nao badala ya kufanya uchunguzi wa tukio walikwenda ki operation na ilawa ni hali ya mapambano baina yao na raia watu wengi wakajeruhiwa na akiwamo polisi.
Polisi wakaongezewa nguvu na ndipo walipo fanya collective punishment. Na raia wakajificha kwenye misikiti lakini hio haikua dawa kijiji kizima kilikua katika kushambuliwa wanawake wakakimbia mapolisi wakaacha watoto wao. Wanaume wengi wakakimbilia maporini.
Kutokana na uhalifu ulofanyika kuwa mkubwa ndio kama kawaida afande masawe akatangaza kuwa ilikuwa operation ya kupigana na alshabab.
Yote kujaribu ku cover up uhalifu waliowafanyia raia.
Wakati yeye akitangaza anapambana na alshabab mkuu wa mkoa bibi chiku anasema hakuna gaidi ni wavunja sheria tu.
Hivyo tukirudi kwenye suala la mada kuu jibu ni kuwa vita ya ugaidi inatumiwa kama mwanya wa kuubamiza uislam. Waloathirika ni waislam .misikiti yao ilivamia na maimam ndio walokamatwa.
Kutoka vurugu za kuuza hiliki mpaka ikageuzwa kuwa ugaidi...

it's more than that.Ni zaidi ya uislam pekee.Vita dhidi ya ugaidi imelenga kuondoa ibada kwa Mwenyezi Mungu duniani.Masalia yote ya imani ya Ibrahim(judaism,christianity and islam) ni lazima yafutike ili kumpisha Maitreya(Dajjal).Tunachokiona hivi sasa ni mkakati maalum wenye kutumia akili za hali ya juu toka kwa malaika Hallel(mnamuita shetani) na wafuasi wake,kutengeneza chaos against each other ndani ya imani hizi,ili chaos hizo zitumike kuhalalisha vitendo vya hujuma dhidi ya dini hizi na kuziangamiza at the same time taking economical advantage juu ya watu wa imani hizo.September 11 marked the beginning of war agains terrorism,do you know who are the real "terrorist"?Wote wale wanaopinga sera za "wakubwa" hao kwa haki na kwa haramu ndio terrorist.Hata mie na wewe kesho tukiamua kuandamana kukataa uwekezaji wa wamarekani kwenye mafuta yetu kule Mtwara tutaitwa terrorist na tutashughulikiwa na serikali yetu wenyewe iliyojaa vibaraka wa "wakubwa" hao.Someni historia za nyuma muone jinsi dini hizi zilivyowatikisa wakubwa hadi wakaziundia mkakati wa kuzifuta.Ni dini hizi ziliangusha Roman empire na kuleta ustaarabu wa sovereign states hadi mie na wewe leo tunajiita watanzania huko nyuma hali ilikuwa mbaya sana tunafichwa tu.War on terror ni excuse inayotumika na wakubwa kupiga kila nchi,kikundi wanachoona ni threat kwao.At the same time wapo magaidi wanaotengenezwa na wakubwa ili kutekeleza matakwa yao kwa kificho.Nendeni mkasome muone uhusiano wa siri kati ya U.S na akina Osama,Taleban etc.Ugaidi unatumika kudhoofisha all sovereign states duniani ili huko mbele iwe rahisi kuwa na serikali moja,dini moja na sarafu moja.Angalieni Misri,Iraq na kwingineko,ugomvi ni wa jamii na serikali lakini watu wanalipua makanisa,misikiti ya madhehebu mengine,why?hiki ndicho wanachotaka wakubwa,kuwapandikizeni roho ya chuki mtwangane hadi mmalizane,baadae mkichoka magomvi haya mkaambiwa dini hazifai wajinga watakubali.Na hata humu jamvini hatuoni baadhi yetu wameanza kutoa kauli hizo na kuziita "dini za meli"?mbona dawa hadi leo zinakuja na meli hatuzisemi?au kwa vile zinatuponya?no,ni kwa vile hazileti magomvi.Dini watu wanazichoka,wanafanywa wazichoke.Ndio maana nikauliza,tunafanyaje ili kuzitengamanisha dini zetu na kesi za kubambikiwa?nina maana kubwa kuuliza hivyo?huko mbele mtapigwa marufuku kwa kuitwa magaidi na haya yalishatokea.Dark ages warumi walichoma moto maneno ya Mungu(scrolls),waliua mamilioni ya wakristo na wayahudi duniani(hasa ulaya) na hata Yerusalem iliposhikwa na akina Caliphate Omar,Saladin na majeshi ya uislam mayahudi waliruhusiwa kuabudu na kukaa Jerusalem(wayahudi na waarabu walielewana,majeshi ya uislam yaliheshimu wayahudi na dini yao),lakini mji uliposhikwa na crusaders wayahudi waliuawa na kufukuzwa Yerusalem,why?leo tunaongea kinyume kwamba myahudi na mwarabu hawaelewani,mkristo na muislam hawapatani,Hallel kafanikiwa,kilichobaki mpigane,mlete vita kubwa duniani,muitwe wafanya fujo,muwe banned!ndio hayo ya Tanga(kama ni kweli),ndio hayo ya Arusha,etc.Kuelewana myahudi na mwarabu na mkristo na muislam kutakuwa failure mbaya ya wakubwa na kutofautiana kwao kutakuwa ushindi mkubwa kwa wakubwa.Ugomvi hapa unamuhusu Ibrahim na Mungu wake,na Nimrod na Mungu wake Hallel,nothing new,it's all about "ancient war".Cha msingi tusikae kimya,tuiulize serikali,tena tukiwa pamoja wakristo kwa waislam,tuwaulize wakubwa,nini kimetokea Tanga?wakituona pamoja watashtuka sana!
 
HABRUHI YA NIPASHE KUTOKA KWA MAJERUHI NA MASHUHUDA ILIKUA KAMA IFIATAVO...

25th October 13
Wananchi waasi

Lulu George
Askari mgambo wa kijiji cha Lwande Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga, Salum Mgonje, ameuawa kwa kucharangwa mapanga na Mkuu wa Kituo cha Polisi cha wilayani hapa, Inspekta Lusekelo Edward, kujeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi baada ya kuibuka vurugu kubwa kijijini hapo.

Vurugu hizo zinadaiwa kusababishwa na kundi la watu ambao walikuwa wakipinga kitendo cha mwenzao kulipishwa ushuru wa ununuzi wa hiliki na serikali ya kijiji.
Kufuatia vurugu hizo, askari kadhaa wakiongozwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Kilindi, Inspekta Edward, walikwenda katika kijiji hicho kwa lengo la kuwakamata watu waliohusika na mauaji ya askari mgambo, na ndipo alipopigwa risasi tumboni na mkononi.

Inspekta Edward akizungumza na NIPASHE jana katika Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo, alikolazwa kwa matibabu, alisema alipigwa risasi alipofika katika Msikiti wa Answaar Suna uliopo kwenye eneo la Kibirashi wilayani Kilindi muda mfupi baada ya kuwatangazia watu hao ambao baadhi yao wanadaiwa kuwa waumini wa msikiti huo kuwa wako chini ya ulinzi.

Alisema chanzo cha tukio hilo ni kutokana na vurugu zilizotokea Oktoba 22, mwaka huu saa 6:00 mchana, baada ya waumini hao kutakiwa kulipa ushuru wa mazao waliyonunua, lakini waligoma na kusema kuwa ni kinyume cha sheria za dini yao.

Alisema kutokana na hali hiyo, watu hao walianzisha vurugu na kusababisha kifo cha mgambo huyo kwa kumshambulia kwa mapanga.
Hali hiyo iliwalazimisha polisi kuwakamata viongozi wao wawili na kusababisha wengine kuandamana kupinga hatua hiyo.

"Baada ya vurugu hizo ambazo zilisababisha kifo cha mgambo, ndipo tulipoamua kuwafuata waumini hawa kwenye msikiti wao, tulipofika pale walikuwa wakitoka na ndipo tulipowatangazia kuwa wapo chini ya ulinzi. Cha kushangaza walirudi na bunduki mkononi na kuanza kuwafyatulia askari risasi ovyo," alisema Edward.

Alisema pamoja na kushambuliwa na waumini hao, hadi kufikia juzi watu watatu walikuwa wamekamatwa na kwamba msako unaendelea.

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Selemani Liwowa, alisema chanzo cha mapigano hayo ni mfanyabiashara mmoja ambaye jina lake halijafahamika, mkazi wa kijiji cha Lulago, Kata ya Lwande alipokwenda kijiji cha Lwande kununua hiliki na kukaidi kulipa ushuru wa mazao.

Alifafanua kuwa mfanyabiashara huyo baada ya kukataa kulipa ushuru huo, ndipo askari mgambo (marehemu), alipokwenda kumtia msukosuko ili alipe kama taratibu na sheria za kijiji zinavyoelekeza.

Liwowa alisema baada ya kutokea mabishano makubwa baina ya mgambo na wafanyabiashara, ndipo wenzake walipoingilia suala hilo kwa kuanza kumshambulia kwa mapanga mgambo huyo hadi kusababisha kifo chake.

Aliongeza kuwa taarifa za mauaji ya mgambo zilipofika kituo cha polisi, ilimlazimu Mkuu wa Kituo kuongoza kikosi cha askari kilichokwenda kijiji cha Lwande kwa ajili ya kuwasaka waliohusika na mauaji hayo na ndipo lilipojitokeza kundi la watu wenye silaha na kuanzisha mapigano dhidi ya askari hao.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Juma Ndaki, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa polisi inaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo halisi cha vurugu hizo.

Kamanda Ndaki alisema kundi hilo lilianzisha vurugu baada ya kuona wenzao wamekamatwa na kukimbilia msituni na kwamba msako mkali unaendelea ili kuwatia nguvuni.

"Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constatine Massawe, yupo eneo la tukio kwa ajili ya kuona hali halisi ilivyo na operesheni maalum ya kuwasaka watu hao imeanza kutekelezwa," alisema Kamanda Ndaki.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo, Dk. Jumanne Karia, alisema majeruhi huyo, Mkuu wa Kituo cha Polisi alipokelewa hospitalini hapo juzi saa 10:30 usiku akitokea wilayani Kilindi.

Dk. Kariya alisema hali yake kwa sasa inaanza kuimarika na kwamba utaratibu wa kumwondoa risasi moja iliyopo tumboni unaendelea.

Tukio hilo limetokea Kilindi wakati kukiwa na taarifa za tukio linalofanana na hilo kutokea katika Wilaya ya Lushoto ambako Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wilayani humo (OCCID), Ufoo Maanga, alicharangwa mapanga na wananchi baada ya askari kwenda kumkamata mtuhumiwa wa mgogoro wa ardhi katika kijiji cha Viti, Kata ya Shume wilayani Lushoto.


NIPASHE

Utaona vurugu hizi ni kama ilivo tajwa katika habari hiii. LAKINI pia usome habari kama ilivomkariri juu polisi majeruhi ni kuwa baada ya vurugu zile za wafanya biashara walikwenda msikitini !!!!! kuwataka waumini wajisaliimishe...
tuseme ukweli polisi walivurunda na kukitia adabu kijiji kizima na wanawake na watoto ...na ili kuficha ouvu wao basi wakatangaza wanapambana na magaidi wapo msikitini na lashabaab.....
waislam ndio wamekua punching bag na kichaka cha uovu

lakini kuna masuala tujiulize kuhusu hili:


  • kwanini polisi walizuia waandishi kufika kule kujua kinachoendelea?
  • masheikh wa mJINI Tanga walipopata taarifa hizi walikutana na kutaka kwenda kujua kina cho jiri lakini hawakukubaliwa
  • sheikh chambuso na wenzake wanao kaa mjini Tanga walifika kuwaona majeruhi hospital kwa nini wakamatwe na kusingiziwa?
  • kwa nini waislam wa Tanga mjini kwa muda wa wiki mbili walikua wakizingirwa siku za ijumaa misikitini?
  • polisi walikua wanaficha nini?
kuna haja ya kuunda tume huru kulifanyia uchunguzi jambo hili....
 
Baada ya kukonect dots kilichofanyika kilindi haukuwa ugaidi ni riots tu za kawaida,issue hi kwamba wanakijiji waliua mgambo na polisi walikuja kuli restore order sasa tuwe wakweli uhalifu unapotokea na mhalifu akajificha msikitini au kanisani polisi hawana haki ya kumkamata???wanakijiji hawa inavyoonekana walibishana na dola pamoja na kupambana nayo baadhi wakakimbilia msikitini je haikuwa sahihi kuwafuata humuhumo???refer kesi ya mwembechai
 
it's more than that.Ni zaidi ya uislam pekee.Vita dhidi ya ugaidi imelenga kuondoa ibada kwa Mwenyezi Mungu duniani.Masalia yote ya imani ya Ibrahim(judaism,christianity and islam) ni lazima yafutike ili kumpisha Maitreya(Dajjal).Tunachokiona hivi sasa ni mkakati maalum wenye kutumia akili za hali ya juu toka kwa malaika Hallel(mnamuita shetani) na wafuasi wake,kutengeneza chaos against each other ndani ya imani hizi,ili chaos hizo zitumike kuhalalisha vitendo vya hujuma dhidi ya dini hizi na kuziangamiza at the same time taking economical advantage juu ya watu wa imani hizo.September 11 marked the beginning of war agains terrorism,do you know who are the real "terrorist"?Wote wale wanaopinga sera za "wakubwa" hao kwa haki na kwa haramu ndio terrorist.Hata mie na wewe kesho tukiamua kuandamana kukataa uwekezaji wa wamarekani kwenye mafuta yetu kule Mtwara tutaitwa terrorist na tutashughulikiwa na serikali yetu wenyewe iliyojaa vibaraka wa "wakubwa" hao.Someni historia za nyuma muone jinsi dini hizi zilivyowatikisa wakubwa hadi wakaziundia mkakati wa kuzifuta.Ni dini hizi ziliangusha Roman empire na kuleta ustaarabu wa sovereign states hadi mie na wewe leo tunajiita watanzania huko nyuma hali ilikuwa mbaya sana tunafichwa tu.War on terror ni excuse inayotumika na wakubwa kupiga kila nchi,kikundi wanachoona ni threat kwao.At the same time wapo magaidi wanaotengenezwa na wakubwa ili kutekeleza matakwa yao kwa kificho.Nendeni mkasome muone uhusiano wa siri kati ya U.S na akina Osama,Taleban etc.Ugaidi unatumika kudhoofisha all sovereign states duniani ili huko mbele iwe rahisi kuwa na serikali moja,dini moja na sarafu moja.Angalieni Misri,Iraq na kwingineko,ugomvi ni wa jamii na serikali lakini watu wanalipua makanisa,misikiti ya madhehebu mengine,why?hiki ndicho wanachotaka wakubwa,kuwapandikizeni roho ya chuki mtwangane hadi mmalizane,baadae mkichoka magomvi haya mkaambiwa dini hazifai wajinga watakubali.Na hata humu jamvini hatuoni baadhi yetu wameanza kutoa kauli hizo na kuziita "dini za meli"?mbona dawa hadi leo zinakuja na meli hatuzisemi?au kwa vile zinatuponya?no,ni kwa vile hazileti magomvi.Dini watu wanazichoka,wanafanywa wazichoke.Ndio maana nikauliza,tunafanyaje ili kuzitengamanisha dini zetu na kesi za kubambikiwa?nina maana kubwa kuuliza hivyo?huko mbele mtapigwa marufuku kwa kuitwa magaidi na haya yalishatokea.Dark ages warumi walichoma moto maneno ya Mungu(scrolls),waliua mamilioni ya wakristo na wayahudi duniani(hasa ulaya) na hata Yerusalem iliposhikwa na akina Caliphate Omar,Saladin na majeshi ya uislam mayahudi waliruhusiwa kuabudu na kukaa Jerusalem(wayahudi na waarabu walielewana,majeshi ya uislam yaliheshimu wayahudi na dini yao),lakini mji uliposhikwa na crusaders wayahudi waliuawa na kufukuzwa Yerusalem,why?leo tunaongea kinyume kwamba myahudi na mwarabu hawaelewani,mkristo na muislam hawapatani,Hallel kafanikiwa,kilichobaki mpigane,mlete vita kubwa duniani,muitwe wafanya fujo,muwe banned!ndio hayo ya Tanga(kama ni kweli),ndio hayo ya Arusha,etc.Kuelewana myahudi na mwarabu na mkristo na muislam kutakuwa failure mbaya ya wakubwa na kutofautiana kwao kutakuwa ushindi mkubwa kwa wakubwa.Ugomvi hapa unamuhusu Ibrahim na Mungu wake,na Nimrod na Mungu wake Hallel,nothing new,it's all about "ancient war".Cha msingi tusikae kimya,tuiulize serikali,tena tukiwa pamoja wakristo kwa waislam,tuwaulize wakubwa,nini kimetokea Tanga?wakituona pamoja watashtuka sana!

Mkuu
Hayo yote Mimi nimeyasema na kuwauliza ndugu zangu Wote Humu baadhi wamenipa majibu mazuri na Mimi nimewambia hii Dhana Hakuna atakae pona! Awe mkristo Au Muislam!

Nilichokugundua kuna baadhi ya Watu Humu hawaelewi kabisa hii kitu!

Nakushukuru Kwa kuweka sawa haya mambo na Kwa maelezo marefu na mazuri!

Mungu ahimidiwe!
 
TANGA: Mji wenye tamaduni nyingi za Kiislamu


MJI wa Tanga ni moja kati ya miji iliopo katika ukanda wa Pwani wa Afrika ya Mashariki wenye Waislamu wengi. Inakadiriwa kuwa karibu asilimia 80 ya wenyeji wa mji huo ni Waislamu jambo lililofanya mji huo kuwa na tamaduni nyingi za Kiislamu. Kwa miaka mingi mji wa Tanga umekuwa moja ya miji ya Afrika ya Mashariki ambao umekuwa ukiheshimiwa miongoni mwa Waislamu wa Afrika Mashariki.
WENYEJI wa mji huo ni Wadigo na Wasegeju ambapo ukichukuliwa kimkoa una mchanganyiko wa Wazigua, Wabondei na Wasambaa. Katika sehemu zote za mji huo ambazo utatembea utakuta madrasa ndogo ndogo za watoto zisizo na idadi, Misikiti na pia kuna vyuo vikuu vitatu vinavyotoa elimu ya dini ya Kiislamu. Vyuo hivyo ni TAMTA, ZAHRAU na MAA-WA.
Chuo cha TAMTA ambacho ni cha kwanza na cha muda mrefu zaidi kilichopo eneo la Gatundu kiliasisiwa na Sheikh maarufu Afrika Mashariki, marehemu Sheikh Mohammed bin Ayoub, aliyefariki mwaka juzi na kuacha uongozi kwa mwanafunzi wake mkuu Sheikh Mohammed Bakar.
Chuo hiki huchukua wanafunzi mbalimbali kutoka nje ya mkoa na nje ya nchi na kina matawi yake katika wilaya za mkoa huo na nje ya mkoa. Wanazuoni wengi wenye madrasa kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini walipata elimu zao kutoka chuo hiki.
Aidha, Chuo cha ZAHRAU ambacho kiliasisiwa na marehemu Sheikh Selemani kilichopo eneo la Madina, pia huchukua wanafunzi kutoka nje ya mkoa na kina matawi yake kadhaa hapa nchini. Hivi sasa kinaongozwa na Sheikh Mohammed Selemani ambaye ni mtoto wa kwanza wa Sheikh Selemani.
Chuo cha MAA-WAL kipo eneo la Mwakizaro na kimejenga shule ya sekondari katika eneo la Ngamiani. Chuo hiki kilianzishwa na marehemu Sheikh Shabani na hivi sasa kinaongozwa na Sheikh Mohammed Hariri.
Miongoni mwa Misikiti mikubwa ya Ijumaa iliopo katika mji huo ni Msikiti wa Riyadha uliopo katika eneo la Ngamiani ambao ndio mkubwa kuliko yote uliojengwa tangu enzi za wakoloni ambapo katika miaka ya karibuni uliongezwa tena.
Pia kuna taasisi ya Kiislamu ya Answar Sunna ambayo imeendeleza zaidi maendeleo ya Uislamu ya mji huo kwa kuanzisha shule ya chekechea ya Kiislamu na shule ya msingi ambayo pia hutoa mafunzo ya kidini na kufundisha Kiarabu. Shule hii ipo eneo la Msambweni.
Taasisi hii pia imejenga kituo cha watoto yatima kilichopo eneo la Makorora na ina mpango wa kujenga shule ya sekondari katika eneo la Pongwe.
Kwa vile asilimia kubwa ya wenyeji wa mji huo ni Waislamu, Uislamu unaonekana kuwa na nguvu kuliko dini nyingine na hivyo mji mzima kutawaliwa na mazingira ya Kiislamu.
Tukiacha Misikiti inayoonekana katika mitaa mbalimbali pamoja na madrasa za watoto, mavazi rasmi ya wazee wa mji huo ni kanzu, kofia na bakora. Kwa upande wa wanawake, mabaibui hutumika kama vazi maalum la kutokea. Mavazi ya hijabu na kujitanda khanga mbili ni ya ada sana kwa wasichana waliofikia umri wa kuolewa.

Miongoni mwa mambo yanayodhihirisha kutopea kwa tamaduni za Kiislamu katika mji huo ni salamu wanayopeana watu wanapokutana bila kujali ni wa dini gani. Salamu kubwa inayotumika katika mji huo ni Salaam Alaikum. Hata Wakristo wachache wa mji huo wameizoea salaam hii na kupeana hata wenyewe kwa wenyewe. Ni jambo la kawaida pia kumsikia mtu akishukuru kwa tamshi la Alhamdulillahi au akitumia neno IshaAllah hata kama si Muislamu.
Katika mji huo kunakuwa na mabadiliko makubwa katika miezi ya kawaida na mwezi wa Ramadhani. Pamoja na kuwepo na watu wa dini nyingine lakini anaweza kuhisi kuwa kila mtu anafunga katika mwezi huo kwa sababu unaheshimiwa na hata wasiokuwa Waislamu.
Huduma za chakula wakati wa mchana zinakuwa adimu. Unaweza kuzunguka mji mzima bila kukuta mgahawa ulio wazi na pale unapobahatika kukuta sehemu inayouza chakula utakuta pazia kwenye mlango ili kuficha waliomo ndani. Biashara ndogondogo kwenye mitaa kama vile kahawa, tangawizi, maji baridi na nyinginezo huachwa na kuonekana wakati wa magharibi.
Katika kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhani kunakuwa na makundimakundi ya kina baba na kina mama kwenye maduka kutafuta nguo mpya za watoto wao kwa ajili ya sikukuu ya Idd el Fitr inayoadhimishwa kila baada ya mfungo wa Ramadhani.
Ni katika kipindi hiki ambapo wenye maduka ya nguo katika mji huo huneemeka na kufanya biashara zao kwa uhakika zaidi. Kuna maduka ambayo hufufuka katika kipindi hiki tu na baada ya sikukuu kupita hufa na kusubiri mfungo mwingine.
Tanga ni mji unaongoza Tanzania kwa ustahamilivu wa kidini.hakujawahi kuwa na misuguano kati ya wakristo na waislam. Nimeishi Tanga kwa miaka mitatu.zile Big November Crusade kila mwaka zilikuwapo Tanga, wala haijawahi kutokea rabsha yoyote ingawa waislam ni wengi na mikutano ile ikifanywa katika maeneo yao.kwa tanga msuguano kati ya Zaharau na Tamta ni mkubwa sana kwenye mambo ya Maulid na mengineo , ni msuguano wa kitaalam zaidi kila mmoja akishandana na mwenzie kuhusu lipi sahihi na lipi si sawa katika iman.
Ushabiki huu wa TAMTA NA ZAHARAU umeenea maeneo yote ya mkoa wa Tanga ikiwamo Kilindi.
Iliripotiwa hivi kwenye sherehe za Tamta mwaka jana:
ZAHARAU DAY SIKU MOJA NA TAMTA
Sherehe za mwaka huu za taasisi kongwe nchini katika hali nadra sana zimeanza na kumalizika kwa siku moja.mahudhurio nayo yalionekana kugawanyika kisawa sawa.muda wote sherehe za siku tatu waumini walionekana wakikatiza kutoka barabara itokayo TAMTA kuja Zaharau.Kwa vile sherehe za Tamta zilimaliza mapema saa sita usiku makundi ya watu walikatiza kuelekea Zaharau kuendelea kusikiliza mawaidha.
Hawa ndio watu wa TANGA.


Jee TAMTA NA ZAHARAU KUNA MSUGUANO GANI ?
Msuguano huu sio wa kupigana bali kama wa simba na yanga naweza kuuita.Lakini mahusiano kati ya waislam na wakristo yapo shwari kabisa hakuna msuguano hata wa kimawazo kama huu wa ndugu zao Tamta na zahrau.

Lakini Leo wanapangwa viongozi kuwatumikia wananchi lakini wanakuja na fitna za kutaka kuwagombanisha kwa kuja na agenda za watu wengine.
sheikh Mohamed said atanirekebisha maana yeye mjuzi zaidi wa huko Tanga
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom