mwaka jana tulimfanyia KP wifi yangu. mchumba hakuwa na hela sana, huku kwetu kulikuwa na uafadhali. tukiwa tunajadili cha kumpa binti kwa kp na sendoff nikashauri wakwe kuwa huu sio wakati wa kujionyesha, hebu tumpe binti muda wa kwenda kukaa na mwenzie wajue wanataka nini.
Orodha waliyotupa karibu yooote ilikuwa vitu vya jikoni, huyo kaka alikuwa kapanga tu vyumba 2, na walikuwa na vitanda vyao 2 etc, wakaona vinawatosha kwa kuanzia maisha. wakaomba kama kutakuwa na hela ya ziada, kuliko kuwanunulia vitu ambavyo kwa sasa vitakaa tu bora tuwape hizo hela ziwasaidie.
badala ya kwenda china kufunga kontena la vitu ambavyo hawana hata nyumba ya kuviweka, tuliwapa zawadi ya 25M. Imewasaidia kuongezea, nasasa karibia watahamia nyumbani kwao na hayo masofa watanunua wakiwa na pa kuyaweka