Kwenu madaktari-hivi Tanzania ugonjwa ni malaria tu?

Joined
Mar 15, 2013
Posts
17
Reaction score
7
Nilichogundua ni kwamba kwenye hospitali nyingi za mikoa, kushuka chini asilimia kubwa ya wagonjwa wakifika tu kwa madaktari wanapatiwa dawa za malaria hata kabla ya vipimo, na hata vipimo visipoonyesha uwepo wa wadudu hao, bado utapatiwa dawa. Hivi nyie madaktari wetu kwani ugonjwa ni malaria tu mnaoujua? hamna magonjwa mengine mnayoweza kutibu?
 
A negative blood smear for malaria parasites does not rule out malaria.Ndio maana madaktari wameenda shule.Ukitaka kuelewa zaidi na wewe nenda darasani ukafundishwe kama hao madaktari.
Tatizo siku hizi kila mtu anajifanya anajua kutibu, hatufuati ushauri wa wataalamu hawa.Wewe unaijua life cycle ya malaria parasites?kuna kipindi hivi vijidudu vinakuwa kwenye ini na havipatikani kwenye peripheral blood smear, daktari anaelewa anachofanya dalili za malaria zinaweza kumsaidia kuanzisha tiba hata kama majibu ya damu hayaonyeshi vidudu.Msiingilie kazi za wataalamu.
 
its tricky!

matibabu ya mgonjwa yanategemea historia, upimaji wa mwili na majibu ya maabara.
majibu ya maabara yana mchango mdogo katika kuamua matibabu ya mgonjwa.
kwa mazingira ya kwetu (ambapo wagonjwa wengi hawana family dr) dr. hana uwezo wa kumfuatilia mgonjwa kwa ukaribu anaweza kutibu hata kama malaria haijaonekana. kama mgonjwa anakuwa na family dr, akizidiwa anaweza kumpigia family dr wake akampatia matibabu.
 
kuna mshkaji miaka ya zamani kidogo alipewa dozi ya malaria akawa hapati nafuu, kumbe alikuwa na typhoid, baada ya wiki moja akatokea jamaa ambaye alishawahi kuugua typhoid akamshauri akapime typhoid kwa daktari mwingine, akakutwa na typhoid na ilibaki kidogo ifikie stage mbaya. jamaa akatumia dozi ya typhoid akapona kabisa.

NB: hao madaktari ambao unawaita madaktari ukienda deep utakuta wengi wao sio madaktari wa ukwelii.
 

sijaenda shule ya udaktari lakini nimeenda shule zingine na najua kutumia common sense na pia nasoma sana hata vitabu vyenu, kama sio malaria kali, hakuna haja ya kutoa dawa mpaka ithibitishwe kwa kuwa mnatengeneza usugu wa madawa
 

dalili zamalaria mara nyingi ni sawa na za magonjwa mengine kama typhoid, kwa hiyo dr unataka kusema kwamba ukifikiria tu ugonjwa basi uutibu? kama ni hivyo sina haja ya kuja kwako kwa sababu dalili za malaria nazijua na ntanunua dawa dukani
 
Siku hizi kuna evidence based medicine. sijui kama unajua hilo.Hatusomi medicine kwa vitabu tu.na hakuna kitu kama usugu wa dawa.haijawahi kutokea dawa ikawa sugu.Is that how you use your common sense?
sijaenda shule ya udaktari lakini nimeenda shule zingine na najua kutumia common sense na pia nasoma sana hata vitabu vyenu, kama sio malaria kali, hakuna haja ya kutoa dawa mpaka ithibitishwe kwa kuwa mnatengeneza usugu wa madawa
 
Afadhali umezungumzia hili.nadhani kibiasharazaidi amekupata
 
Last edited by a moderator:
Mkuu unayo haki ya kuhoji hivyo lakini linapokuja suala la tiba,weledi na kipaji,wito na kujitoa ni vitu muhimu sana!wakati mwingine ni muhimu kwenda nje ya miongozo rasmi iwapo unadhani ni muhimu kuokoa maisha ya mgonjwa!Sijui iwapo umewahi kujiuliza pia accuracy ya vipimo vya malaria maabara?kwani inatokea sana mtu anacheki asubuhi anakuta hana malaria parasites halafu hapewi dawa za malaria ingawa ana kila dalili!sasa unakuta analazimika kurudi hospitalini usiku wa manane akiwa kazidiwa sana na ukicheki tena malaria unakuta inaonekana!Wataalam wa maabara watwambie ukweli ni kwa nini hutokea hii?Hii inakuwa mbaya kwa mtoto.Nimewahi kuona mtoto kazidiwa sana na walivyocheki malaria hawakuona hivyo alipewa antibiotic tu na painkillers!lakini homa haikwisha na walikuwepo madaktari wenye imani kuwa usipoona majibu ya kuwa na malaria basi is muhimu kutoa dawa za malalia!Yule mtoto hatimaye alianza kupata degedege na alifariki wakijaribu kumpa dawa za kuzuia degedege!Ninavyojua ujuzi wa kugundua tatizo kwa 75% inapaswa kufanywa na daktari na 25% iliyobaki ni support ya vipimo ili ku confirm alichokuwa anafikiria daktari.Sasa naona siku hizi hata wananchi wa kawaida wanaamini vipimo vya maabara ni zaidi ya uwezo wa daktari kugundua tatizo.Hiyo inaweza kuwa Ndio kwa baadhi ya magonjwa ila sio malaria kwani malaria ni deadly disease!Ukichelewa kuitibu inaweza kugharimu muda,raslimali na hata maisha ya mgonjwa.Acha wenye taaluma yao watumie ujuzi wao kutoa huduma kutokana na mazingira yetu!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Mgonjwa mwenye homa kama vipimo vimeonyesha sio malaria basi anatakiwa kupimwa vitu vingine vinavyoweza kusababisha homa.

Wakati vipimo vinaendelea anaweza kupewa dawa ya kutuliza homa na dalili nyingine za ugonjwa wake.

Kama daktari hana vipimo anatibia "emperically" kwa kutoa dawa ya ugonjwa anaodhani una uwezekano mkubwa kumuathiri mgonjwa.

Tafiti zinaonyesha kiwango cha malaria ni kidogo sana Tanzania. Homa nyingi Tanzania husababishwa na magonjwa ya bacteria na virus. Tatizo ni kwamba wapo madaktari ambao hawasomi taarifa mpya na wanaendelea utaratibu wa zamani wa kutoa dawa ya malaria kwa wagonjwa wenye homa. Utaratibu huu hutumika sehemu zenye maambukizo mengi, ambayo Tanzania sasa hivi sehemu nyingi haziko hivyo, ingawa kuna wilaya kama Karagwe ambako maambukizi ni mengi.

Dar es Salaam maambukizi ya malaria ni machache sana. Kwahiyo kutoa dawa za malaria kwa kila homa tusiyojua sababu yake Dar es Salaam si sahihi whereas kwa Karagwe inaweza kuwa sahihi.
 
dalili zamalaria mara nyingi ni sawa na za magonjwa mengine kama typhoid, kwa hiyo dr unataka kusema kwamba ukifikiria tu ugonjwa basi uutibu? kama ni hivyo sina haja ya kuja kwako kwa sababu dalili za malaria nazijua na ntanunua dawa dukani


UNAJUA POSITIVE PREDICTIVE VALUE NA NEGATIVE PREDICTIVE VALUE YA KIPIMO CHA MALARIA (BS) NA WIDAL TEST?
unajua prevalence ya typhoid hapa Dar?
UNAJUA TAFSIRI YA KIPIMO CHA TYPHOID (WIDAL TEST) KUWA POSITIVE MAANA YAKE NI NINI?
JE UNAJUA NI MUDA GANI UNAPITA MTU ALIYEKUWA POSITIVE KUWA NEGATIVE?
tatizo la watanzania kila kitu wanajua wao.
ngoja siku mtoto wako awe na homa ulete kujua kwako; ndio utajua majuto ni mjukuu.
 
Mara nyingi ukienda hospitali za mikoa, utakutana na madaktari wa aina nne tofauti, japokuwa wote wanaitwa madaktari, na sio rahisi mgonjwa wa kawaida kuwatofautisha hawa.kuna clinical officer, Assistant medical officer, medical officer na Physician( kama ni medical case).Sasa huduma yako inategemea unakutana na nani.Ukikutana na physician orodha ya vipimo atakavyokuandikia, mgonjwaasiyeelewa ataona kama ameonewa na lazima atalalamika.Physician ndiyo think tank wa all medical cases in the hospital.It is a good idea to have a family doctor, ambaye muda mwingi atakushauri uende wapi na upate huduma ya aina gani.na infact a good family doctor akiwa hajui kitu atakuambia na atakuelekeza kwa senior wake.wanaoelewa umuhimu wa kuwa na daktari wa familia, wameshafanya hivyo katika baadhi ya mikoa kama kilimanjaro, dar na mwanza.
 
Nadhani Mpigania Uhuru ameweka wazi hapa.mie nilifikiri unatafuta maoni ya kitaalamu kumbe uko kwenye ligi!endelea kujinywea dawa kwa kusoma vitabu mbalimbali.ipo siku utahitaji maelekezo ya kitaalamu, kwa kuwa haujui pharmacodynamics na pharmacokinetics ya hizo dawa unazomeza.
dalili zamalaria mara nyingi ni sawa na za magonjwa mengine kama typhoid, kwa hiyo dr unataka kusema kwamba ukifikiria tu ugonjwa basi uutibu? kama ni hivyo sina haja ya kuja kwako kwa sababu dalili za malaria nazijua na ntanunua dawa dukani
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ulichosema ni kweli kabisa,ila kifanyike kwenye malaria kali tu! ninachohoji hapa ni sisi tunaoenda hospitali kwa vidalili vya kichwa kuuma, kizunguzungu, maumivu ya viungo n.k
 

Mkuu hili ni jukwaa huru, hata kama sijui hivyo ulivyoviandika hapo juu wewe unatakiwa ujibu (kama unataka) hoja iliyopo mezani. Na mimi nikikuuliza vitu nilivyosoma mimi kwa muda wote niliokuwa shule hutavijua. Cha msingi jibu hoja Dr.na kuwa tayari kupokea challenges! Suala la mtoto wangu kuugua homa kali halina uhusiano na hoja iliyo mezani
 

Sounds professional! ahsante
 

We ni daktari, na inaonesha huelewani na madaktari wenzako kazini. Umeleta mvutano tu ndo kusudi lako (Histrionic disorder)
 
Dr. Maubero na mwenzio Mpigania uhuru, nawashauri muangalie ITV malumbano ya Hoja usiku huu ndo mjue kwamba sisi wananchi tunafikiria nini kuhusu nyie!
Suala la kuniambia nikikuambia dalili zangu bila kunipima wewe utajua kama ni malaria na unipe dawa tu nakufananisha na mganga wa kienyeji aliyepiga ramli na kwa nini nije kwako kama hizo dalili na mimi nazijua na dawa ziko dukani? nadhani ZeMarcopolo- nadhani ni mwalimu wenu ametoa majibu yenye akili

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…