Kwenu wasindikiza misiba na wafiwa mikoani

Kwenu wasindikiza misiba na wafiwa mikoani

let say unaishi dar, ukifa ukazikwa huko kuna ndugu zako wengi hawatakuja, hawataliona kaburi lako. Kuzikwa mbali na ndugu zako wengi ni sawa na kuzikwa kusikojulikana. Pale dar labda uwe na uwezo kifedha walau kaburi lako lijengewe ili lisipotee muda mrefu kuna ndugu watajikongoja kuja dar kuona ulikozikwa. Kuzikwa nyumbani unakotoka ni bora
Kuna faida gani ya kutunza kaburi?
 
Nilifiwa na ndugu yangu dar, msiba ukaletwa mkoani kwetu kuzikwa kijijini. Pale kijijini hatuna nyumba ila shamba tu ambako huwa tunazika wanafamilia. Jirani na eneo letu kuna vijumba vya slope vimechakaa japo majirani wanaishi ndani ya vijumba hivyo. Wasindikiza msiba toka dar na kwingine walianza kukandia eti inakuwaje marehemu alijenga jumba la kifahari dar lakini nyumbani kwao asijenge hata kibanda cha kufikia? Wasindikiza wafiwa walianza kuhusisha vijumba vile kuwa ndio nyumbani kwa marehemu ikabidi tuwaambie hapa tulihama kitambo sana enzi tukiwa wadogo na tuna mpango wa kujenga nyumba ya maana hapa ili tuwe na pa kufikia tukitoka mikoani kunako mishe zetu. Wasindikiza wafiwa wana tabia ya kuchunguza nyumbani kwao na marehemu kuna nini cha maana walinganishe na huko dar alivyonavyo
Umeshakutwa naa bwana Pepsi unajitetea nini. Kama mlihama toka zamani mmerudi kufanya nini..?? Hio aibu ibebeni. Ndo tulivyo binadam.. kujenga utakapozikwa ni muhimu sana huwez kuzuia binadam kuongea by then
 
Kuna kitu watu hwataki kukisema lakini ukweli ni kwamba maisha ya kijijini yamejaa chuki na zongo saana kuna jamii ukianza kujenga nyumba kijijini kama haujajipanga walahi hautoweza kuingia kwenye hiyo nyumba ukiwa mzima ni jeneza tu ndiyo litaingizwa na hii imepelekea wengi kutokujenga nyumba ya maana kwao.
Huku kujijini kipindi cha nyuma hata ukitaka kusafiri hauagi unamuaga mama baba na ndg wa karbu saana na kuondoka unaondoka kama unafika tu kijiji cha jiran kumbe ndiyo unasepa hivo.
Lakini pia kingine ni uwezo. Unakuta mtu amejikongoja saana mpk akajenga nyumba mjin mpka aje ajenge nyingine kijijin inamchukua tena miaka kadhaa
 
let say unaishi dar, ukifa ukazikwa huko kuna ndugu zako wengi hawatakuja, hawataliona kaburi lako. Kuzikwa mbali na ndugu zako wengi ni sawa na kuzikwa kusikojulikana. Pale dar labda uwe na uwezo kifedha walau kaburi lako lijengewe ili lisipotee muda mrefu kuna ndugu watajikongoja kuja dar kuona ulikozikwa. Kuzikwa nyumbani unakotoka ni bora
Hapana, huo ni uzamami, zikwa ulipo hukohuko
 
Ni vizuri ukifa ukazikwe na watu wako kwenu. Kuzikwa mbali na unakotoka ni sawa na ufe halafu mwili wako haujilikani umelala wapi, majini au majivuni? Makaburi ya mbali ni ya hovyo sana
 
Nilifiwa na ndugu yangu dar, msiba ukaletwa mkoani kwetu kuzikwa kijijini. Pale kijijini hatuna nyumba ila shamba tu ambako huwa tunazika wanafamilia. Jirani na eneo letu kuna vijumba vya slope vimechakaa japo majirani wanaishi ndani ya vijumba hivyo. Wasindikiza msiba toka dar na kwingine walianza kukandia eti inakuwaje marehemu alijenga jumba la kifahari dar lakini nyumbani kwao asijenge hata kibanda cha kufikia? Wasindikiza wafiwa walianza kuhusisha vijumba vile kuwa ndio nyumbani kwa marehemu ikabidi tuwaambie hapa tulihama kitambo sana enzi tukiwa wadogo na tuna mpango wa kujenga nyumba ya maana hapa ili tuwe na pa kufikia tukitoka mikoani kunako mishe zetu. Wasindikiza wafiwa wana tabia ya kuchunguza nyumbani kwao na marehemu kuna nini cha maana walinganishe na huko dar alivyonavyo
Tanga?
 
Kinachotuhukumu ni back ground zetu wakati tukiwa wazima,unakuta mshkaji nilikuwa nakesha bar nabadili wanawake gari kali japo za mkopo sometimes nakula pombe na washkaji huku nagombania ku-clear bills za vinywaji.

Ktk mazingira kama haya hata ninaotumia nao wataamini jamaa yupo vizuri kwao hamna shida kasheshe siku nakata moto marafiki wahuzunika kwa kujali tu wanaenda kwetu kunizika mzee hahah,papendeni kwenu ni aibu mnafika msiba wa jamaa town alikuwa kibopa kwao anaenda kushushwa chini ya mwembe usiombe iwe wakati wa kiangazi maana hata miti nayo itamkataa.
 
Imenikumbusha Msanii LuluDiva alivyofiwaga na mama yake aligoma mabest zake wasipige picha za huko kwao Kijijini alipozikiwa bi.mkubwa wake.

Wenzake walikuwa wanaishangaa nyumba yao ya udongo wakati mjini anaonekana ni wakishua.
 
Tujaribu kuwa na moyo wa kutunza siri
mazingira tunayo yakuta huko misibani
kutangaza uliyoyaona baada ya kurudi unamuweka mfiwa katika wakati mgumu baada ya kurudi katika makazi yake

Enyi wasindikizaji wa wafiwa kuweni na vifua haipendizi kuanza kutangaza vijumba viko hivyi choo kilikuwa vile chakula kilikuwa hakitoshi nk
Tuvumiliane tuwe na utu sio wote wametoka katika familia bora
Nb
hivi kuna ulazima kubebana na watu lukuki endapo msiba umetokea mkoani??
Ujumbe mzuri sana aisee
 
Tujaribu kuwa na moyo wa kutunza siri
mazingira tunayo yakuta huko misibani
kutangaza uliyoyaona baada ya kurudi unamuweka mfiwa katika wakati mgumu baada ya kurudi katika makazi yake

Enyi wasindikizaji wa wafiwa kuweni na vifua haipendizi kuanza kutangaza vijumba viko hivyi choo kilikuwa vile chakula kilikuwa hakitoshi nk
Tuvumiliane tuwe na utu sio wote wametoka katika familia bora
Nb
hivi kuna ulazima kubebana na watu lukuki endapo msiba umetokea mkoani??
Haya mambo inategemea na marehemu show off alizokuwa anawafanyia alipokuwa hai.
 
Kuna mkuu mmoja Maj Gen mmoja hivi ilibidi SUMA JKT watumwe kwao kwanza kuweka hata rangi kwenye kuta zilizo katika katika huko kwa babake ndio akazikwe hakuwa na nyumba wala chumba

USSR
Mtu amekula kiapo Cha kifo atakumbuka kujenga kwao au kutibu kwanza msongo wa mawazo wa kiapo hicho Kwa totozi na gambe!!?

Kuna mambo mengine serikali iangalie namna ya kuwajengea Hawa jamaa nyumba huko makwao aiseh!
 
let say unaishi dar, ukifa ukazikwa huko kuna ndugu zako wengi hawatakuja, hawataliona kaburi lako. Kuzikwa mbali na ndugu zako wengi ni sawa na kuzikwa kusikojulikana. Pale dar labda uwe na uwezo kifedha walau kaburi lako lijengewe ili lisipotee muda mrefu kuna ndugu watajikongoja kuja dar kuona ulikozikwa. Kuzikwa nyumbani unakotoka ni bora

Mimi naomba kujulishwa, kuna ulazima gani ndugu kuliona kaburi? Kaburi likipotea nini kitatokea? Kuzikwa nyumbani unakotoka kuna faida gani?
 
Mtu amekula kiapo Cha kifo atakumbuka kujenga kwao au kutibu kwanza msongo wa mawazo wa kiapo hicho Kwa totozi na gambe!!?

Kuna mambo mengine serikali iangalie namna ya kuwajengea Hawa jamaa nyumba huko makwao aiseh!
Sio kuwajengea, hilo nakataa. Kama ni hela wanapata sana tu kwanini waishi maisha ya kujionesha mijini na wasahau kujenga makwao? Inatakiwa wakumbushwe hiki wanachokifanya huku mijini basi wakumbuke na makwao kwani huwa wanawapa watu cha kusema pale wanapohudhuria misiba yao. Siku hizi hata ukimkuta Askari aliyeajiriwa ndani ya miaka mitano tu unakuta tayari kwao alipotokea/kwa wazazi wake ameshawajengea.
 
Kuna kitu watu hwataki kukisema lakini ukweli ni kwamba maisha ya kijijini yamejaa chuki na zongo saana kuna jamii ukianza kujenga nyumba kijijini kama haujajipanga walahi hautoweza kuingia kwenye hiyo nyumba ukiwa mzima ni jeneza tu ndiyo litaingizwa na hii imepelekea wengi kutokujenga nyumba ya maana kwao.
Huku kujijini kipindi cha nyuma hata ukitaka kusafiri hauagi unamuaga mama baba na ndg wa karbu saana na kuondoka unaondoka kama unafika tu kijiji cha jiran kumbe ndiyo unasepa hivo.
Lakini pia kingine ni uwezo. Unakuta mtu amejikongoja saana mpk akajenga nyumba mjin mpka aje ajenge nyingine kijijin inamchukua tena miaka kadhaa
Tanga hawajambo huko mkuu?
 
Back
Top Bottom