Huyu Mzee anajua sana dini hasa ya kikristo na ni mshauri wa Askofu wake
Maneno meeeeengi kupoteza muda,kumbe hata mistari haijui.Anatueleza safari zooote hizo, itusaidie nini.
Wabunge hawa wameshaadhibiwa bado spika anachukua muda mreefu (Hapo tunasema kumsimanga mbunge mmoja kulikoni hapo),
Mambo haya yanatusikitisha Watanzania jambo lisilokuwa na tija kwa Watanzania ndilo linachukua muda mrefu ndani ya bunge kujadiliwa? Ni kwamba wabunge hawakielewi au wanafanya makusudi wapate posho liende.
Tulitegemea katika hili kamati imeshatoa maamuzi lisipoteze tena muda lipite ndiooooooooooooooooo mambo yasonge.
Kwa bunge la leo,tulitegemea kabisa kusikia matatizo yaliyojitokea au kero mbalimbali zilizotokana na maamuzi ya wabunge zikawa kero kwa wananchi na kwao pia baada ya maamuzi yao kujadiliwa na kutolewa ufafanuzi na maamuzi mapya.Badala yake kipindi cha bunge kimekuwa cha mipasho.
Tulitegeme kusikia mjadala mzito na wa kina juu ya Tozo za simu,petroli kupanda kila kukicha, kodi za majengo zinazokatwa kwa makosa ukinunua umeme,usalama wa wananchi,katiba ya nchi,kubambikiwa makesi,msongamano wa mahabusu magerezani nk.kuna vitu kibao tena vya msingi.
Badala yake Spika wa Bunge anatueleza safari zake zisizo na lolote kwetu,na wabunge wanapiga makofi.Thisi is shame halafu bado Sina hakika kama gharama zote za safari hizo kama ni za kwake au ni kodi za wananchi wanyonge wa Tanzania.
Tujadili mambo yanayawaletea wananchi umaskini,tena wa kutupwa yaliyoamuliwa na wabunge waliopelekwa bungeni kuwakilisha wananchi na kuyatafutia suluhu.
Kwa sasa wabunge wetu wanajiwakilisha wenyewe na kuiwakilisha serikali.(Leo hii serikali imetangaza mafuta petroli diesel mafuta ya taa bei imepanda.Ilikuwa petroli shs.2543/-sijui kesho asubuhi inawezekana ikawa 2600/- kwa lita.Sasa najiuliza,marehemu tangu aongoze hii nchi kwa miaka 5 kama ilipanda ni kwa kiasi kidogo sana.Kwa nini sasa hivi inapanda kila mwezi, pili kwanini hatusikii tena mwezi huu imeshuka,mwezi mwingine imepanda kuna nini.Au huko nako kuna tozo ya posho za