Tumezisikia kesi zikiihusisha serikali ya Tanzania.Tumeyasikia madege yakishikiliwa. Hivi serikali yetu inasimamia haki wapi?
1. Angalia hili la kuwafutia watoto wadogo matokeo ya mitihani. Wapi hukumu za jumuiya zinakubalika? Kwa nini hawakuwakamata wahalifu na kuwashughulikia kikamilifu hao?
2. Agiza kitu nje uone mlolongo wa makodi na tozo zenye lengo la kutaifisha tu ulichoagiza. Kutalazimishwa storage charges za ajabu ajabu humo, lengo likiwa upokonywe kiharamia tu hicho ulichoagiza.
3. Anza biashara yoyote. Kodi watakayotaka ni payable in advance na bila kujali utapata faida au la.
4. Ni kwenye lipi serikali ya Tanzania iko kwenye facilitation?Wao ni kwenye kuwakamua watu tu. Serikali hii ni chanzo cha umaskini wa wengi na umaskini uliopo.
5. Angalia ada za shule na vyuo kuona uhalali wa viwango vilivyopo. Nani ana regulate au hata kuwatetea walaji kwenye ya namna hii dhidi ya serikali?
6. Angalia polisi na mahusiano yao na watu. Mizania inawanyeshea vidole kwenye unyang'anyi kutokea kwenye maisha ya watuhumiwa hadi wa mali dhidi ya raia.
7. Angalia sekta za serikali na rushwa. Wapi Pako salama? Ni immigration, NIDA, polisi, TRA, Tanroads au Tanesco?
8. Angalia sheria iliyojiwekea serikali kwa manufaa yake. Mfano, likikamatwa gari na wahamiaji haramu au mali ya magendo au waliyojiainishia wao, serikali watalitaifisha hata kama mwenye nalo hahusiki na kadhia nzima inayogombewa.
9. Magari faini ya dereva inafungamanishwa na mwenye gari hata kama hahusiki na linaloitwa kosa. Lengo likiwa kumlenga zaidi mwenye gari Ili kumpoka chochote kinchowezekana.
10. Gonga mnyama pori. Linganisha na mnyama pori kuathiri watu.
11. Angalia sheria na kanuni za mamlaka zozote za serikali kuwaelekea watu. Mwendo ni mahusiano yasiyokuwa na usawa. Ni ma EFD, ving'amuzi, nk?
12. Nk nk.
Sheria nyingi zimewekwa na serikali kwa manufaa yake pekee dhidi ya watu bila hata ya chembe ya aibu, yote kwa maslahi yake.
Enyi wanasheria ya nini kuyaacha yanayoendelea kana kwamba ni halali? Kulikoni nyie kuendelea kutoa ushirikiano kwao kunako hali kama hizi?
Kulikoni kutokuonyesha jitihada za kutosha za kupatikana mustakabali mwingine ikibidi hata kuwasusia haramu zao?
Tuzitegemee mahakama za nje pekee hadi lini kwenye kusikia neno haki dhidi ya madhwalimu hawa?
1. Angalia hili la kuwafutia watoto wadogo matokeo ya mitihani. Wapi hukumu za jumuiya zinakubalika? Kwa nini hawakuwakamata wahalifu na kuwashughulikia kikamilifu hao?
2. Agiza kitu nje uone mlolongo wa makodi na tozo zenye lengo la kutaifisha tu ulichoagiza. Kutalazimishwa storage charges za ajabu ajabu humo, lengo likiwa upokonywe kiharamia tu hicho ulichoagiza.
3. Anza biashara yoyote. Kodi watakayotaka ni payable in advance na bila kujali utapata faida au la.
4. Ni kwenye lipi serikali ya Tanzania iko kwenye facilitation?Wao ni kwenye kuwakamua watu tu. Serikali hii ni chanzo cha umaskini wa wengi na umaskini uliopo.
5. Angalia ada za shule na vyuo kuona uhalali wa viwango vilivyopo. Nani ana regulate au hata kuwatetea walaji kwenye ya namna hii dhidi ya serikali?
6. Angalia polisi na mahusiano yao na watu. Mizania inawanyeshea vidole kwenye unyang'anyi kutokea kwenye maisha ya watuhumiwa hadi wa mali dhidi ya raia.
7. Angalia sekta za serikali na rushwa. Wapi Pako salama? Ni immigration, NIDA, polisi, TRA, Tanroads au Tanesco?
8. Angalia sheria iliyojiwekea serikali kwa manufaa yake. Mfano, likikamatwa gari na wahamiaji haramu au mali ya magendo au waliyojiainishia wao, serikali watalitaifisha hata kama mwenye nalo hahusiki na kadhia nzima inayogombewa.
9. Magari faini ya dereva inafungamanishwa na mwenye gari hata kama hahusiki na linaloitwa kosa. Lengo likiwa kumlenga zaidi mwenye gari Ili kumpoka chochote kinchowezekana.
10. Gonga mnyama pori. Linganisha na mnyama pori kuathiri watu.
11. Angalia sheria na kanuni za mamlaka zozote za serikali kuwaelekea watu. Mwendo ni mahusiano yasiyokuwa na usawa. Ni ma EFD, ving'amuzi, nk?
12. Nk nk.
Sheria nyingi zimewekwa na serikali kwa manufaa yake pekee dhidi ya watu bila hata ya chembe ya aibu, yote kwa maslahi yake.
Enyi wanasheria ya nini kuyaacha yanayoendelea kana kwamba ni halali? Kulikoni nyie kuendelea kutoa ushirikiano kwao kunako hali kama hizi?
Kulikoni kutokuonyesha jitihada za kutosha za kupatikana mustakabali mwingine ikibidi hata kuwasusia haramu zao?
Tuzitegemee mahakama za nje pekee hadi lini kwenye kusikia neno haki dhidi ya madhwalimu hawa?