Uchaguzi 2020 Kwenye mitandao ya kijamii na mtaani, Membe hakubaliki

Uchaguzi 2020 Kwenye mitandao ya kijamii na mtaani, Membe hakubaliki

Msukuma Original

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2018
Posts
928
Reaction score
3,330
Napenda kuwajulisha wapinzani wa kweli kuwa nimefanya utafiti wangu usio rasmi. Nimejaribu kupita Facebook, tweeter, Instagram na humu JF na kwenye vyombo vya usafiri nakugundua kwamba wananchi wengi walio upande wa upinzani hawakubaliani na ujio wa Membe.

Hoja yao ya msingi ni kwamba Membe amekuja upinzani baada ya kufukuzwa, maana yake asingefukuzwa angekuwa bado mwana CCM. Kwa mantiki hiyo wananchi wanaona kwamba hana mapenzi na upinzani isipokuwa matatizo yake na chama chake cha awali ndio kimefanya aje upinzani.

Angekuwa anaupenda upinzani angeondoka kabla ya kufukuzwa kama ilivyokuwa kwa Lazaro Nyalandu. Ni sawa sawa na mtu na mpenzi wake wanakwaruzana ndio anaamua kumuacha na kwenda kwa bwana mwingine. Angekuwa anampenda huyo bwana mpya angemfuata kabla ya kugombana na mpenzi wake wa zamani.

Maana yake ni kwamba mpenzi mpya kapata mwenza baada ya mpenzi wake kukorofishana na bwana ake. Siku wakipigiana simu na kuweka tofauti zao pembeni mahaba yatarudi kama zamani na mpenzi mpya ataachwa kwenye mataa.

Napenda kuhitimisha kwa kusema kwamba upinzani wasimsimamishe Membe, wananchi wenye mapenzi ya dhati na upinzani hawamtaki Membe. Bora Nyalandu mara 100 kama Lissu atashindwa kurudi nchini au kama ataletewa mizengwe na mamlaka za Kiserikali.
 
Utafiti wako ulitumia methodolijia gani?

Membe anakubalika sana, nimefanya utafiti binafsi juu ya hilo!

Wewe umeuliza wakulima wangapi, wafanyakazi wangapi, wanawake wangapi, wanaume wangapi, umeuliza vijana wangapi, wazee wangapi, umeuliza watu mikoa ipi.

Yote haya lazima uzingatie ili kupata sampuli inayowakilisha picha ya umma.

Umma utazidi kumpenda na kumkubali Membe kwa sababu maono yake ni yaleyale ambayo wananchi majority wamekuwa wakilia na kusaga meno katika utawala huu mfano maslahi ya wafanyakazi, maslahi ya watumishi wa vyombo vya usalama, Ajira kwa vijana, Maslahi ya wakulima, Katiba mpya iliyo bora, etc

Mimi utafiti wangu binafsi unaonyesha Membe anakubalika kuliko Magufuli na kukubalika huku kutaendelea kila siku baada ya kampeni kuanza.

Kama kukiwa na uchaguzi huru na haki Magufuli ajiandae kukabidhi Ikulu kwa Membe au Lissu
 
Utafiti wako ulitumia methodolijia gani

Membe anakubalika sana, Umeuliza wakulima wangapi, wafanyakazi wangapi, wanawake wangapi, wanaume wangapi, umeuluza vijana wangapi, wazee wangapi

Umeuliza watu mikoa ipi.

Yote haya lazima uzingatie ili kupata sampuli inayowakilisha picha ya umma

Mimi utafiti wangu binafsi unaonyesha Membe anakubalika kuliko Magufuli na kukubalika huku kutaendelea kila siku baada ya kampeni kuanza.

Kama kukiwa na uchaguzi huru na haki Magufuli ajiandae kukabidhi Ikulu kwa Membe au Lissu
Ameshakwambia yeye ni msukuma. Sasa habari za methodolojia kwa msukuma huyu huoni ni matusi?
 
Utafiti wako ulitumia methodolijia gani

Membe anakubalika sana, Umeuliza wakulima wangapi, wafanyakazi wangapi, wanawake wangapi, wanaume wangapi

Umeuliza watu mikoa ipi.

Yote haya lazima uzingatie ili kupata sampuli inayowakilisha picha ya umma

Mimi utafiti wangu binafsi unaonyesha Membe anakubalika kuliko Jiwe na kukubalika huku kutaendelea kila siku baada ya kampeni kuanza.

Kama kukiwa na uchaguzi huru na haki Magufuli ajiandae kukabidhi Ikulu kwa Membe au Lissu
Hapana mkuu. Membe hajulikani zaidi ya mikoa ya kusini na Dar es salaam. Mikoa mingine yote iliyobakia hawajawahi hata kumsikia. Lissu ndio the real deal. Lissu ndio chaguo sahihi kwa upinzani, ikishindikana Lissu basi Nyalandu atatufaa maana Nyalandu aliondoka mwenyewe ccm baada ya kutokubaliana na dhuluma zao. Ila Membe ameondoka baada ya kufukuzwa. Mwenye akili anaweza kung'amua nani ni anaweza kuwa reliable kupeperusha bendera ya upinzani.
 
Hapana mkuu. Membe hajulikani zaidi ya mikoa ya kusini na Dar es salaam. Mikoa mingine yote iliyobakia hawajawahi hata kumsikia. Lisu ndio the real deal. Lisu ndio chaguo sahihi kwa upinzani, ikishindikana Lisu basi Nyalandu atatufaa maana Nyalandu aliondoka mwenyewe ccm baada ya kutokubaliana na dhuluma zao. Ila Membe ameondoka baada ya kufukuzwa. Mwenye akili anaweza kung'amua nani ni anaweza kuwa reliable kupeperusha bendera ya upinzani.

Lissu anakubalika sana hilo sina ubishi,

Isipokuwa kama Membe akisimama na Magufuli, Magufuli anapigwa asubuhi na mapema.

Watu wana hasira na utawala wa Magufuli zaidi kuliko kutomjua Membe.

Nyalandu huyo anashika mkia kwenye kukubalika!
 
Msukuma Original,
Lakini sauli aliyebatizwa kuitwa Petro alikuwa farisayo aliyewaua na kuwatesa wakristu, lakini ni huyu sauli ndo kaeneza injili duniania kuliko petro swahiba yake Yesu.
Dogo usikariri
 
Ukute hujui kuwa yeye no mtanzania na ana Uhuru wa kujiamlia chochote tofauti na unavyofikiria moyoni kwako
 
Back
Top Bottom