SI KWELI Kwenye ukurasa wa Lema wa X (Twitter) ameandika Mbowe na mwanae wasusa CHADEMA, wagoma kumpa vifaa Lissu kwaajili ya mapokezi ya singida Februari 15

SI KWELI Kwenye ukurasa wa Lema wa X (Twitter) ameandika Mbowe na mwanae wasusa CHADEMA, wagoma kumpa vifaa Lissu kwaajili ya mapokezi ya singida Februari 15

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
MBOWE NA MWANAE WASUSA CHADEMA WAGOMA KUMPA VIFAA VYA MKUTANO LISSU.

Mtoto wa Mbowe (James Mbowe) ambaye ana kesi ya Madai Mahakamani kwa kosa la kutowalipa Mishahara wafanyakazi wake zaidi ya miaka 3 leo ana muhujumu Lissu kwa kumnyima vifaaa vya Mziki na Jukwaa kwa ajili ya Mkutano wake wa mapokezi ya tarehe 15 Feb, 2025 Mkoani Singida.

#NoReformNoElection

photo_2025-02-10_15-53-35.jpg
 
Tunachokijua
Godbless Lema ni mjumbe wa kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA ambaye aliwahi kuwa mwenyekiti wa chama hicho kanda ya Kaskazini. Wakati wa uchaguzi mkuu ndani ya chama hicho uliofanyika January 2025 Lema alikuwa ni miongoni mwa makada ambao walikuwa wakimuunga mkono Tundu Lissu alipokuwa akigombea nafasi ya uenyekiti hadi kushinda dhidi ya Freeman Mbowe aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo kwa miaka 21.

Baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa CHADEMA uliomuweka maradakani Tundu Lissu kuwa Mwenyekiti wa chama hicho akimdondosha mtangulizi wake Freeman Mbowe aliyehudumu nafasi hiyo kwa miaka 21, kumekuwapo na taarifa nyingi zinazosambaa mtandaoni zikidaiwa kutoka pande zote mbili za miamba hii mikubwa kwa siasa za upinzani nchini.

Ikumbukwe kuwa, uchaguzi wa ndani wa CHADEMA ulijitanabaisha kwa kuvuta hisia za watu wengi kutokana na mvutano wa hoja, nguvu za wagombea kwa wapiga kura na mtazamo wa umma juu ya wagombea hao.

Hadi sasa, taarifa nyingi za kuzushwa zimeendelea kutengenezwa na watu, mojawapo ikiwa ni andiko lililodaiwa kuchapishwa na katibu Mkuu wa Chama hicho, John Mnyika kuwaonya team Lissu kuacha mpango wa kutaka kufanya fujo siku ya uchaguzi ambayo JamiiCheck ilikanusha uzushi huo.

Mnamo tarehe 15, Februari 2025 Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lissu anatarajiwa kupokelewa Ikungi, Mkoani Singida baada ya kuchaguliwa Januari 21, 2025.

Kumekuwapo na taarifa inayosambazwa katika mitandao ya kijamii ikimnukuu Godbless Lema kuwa amechapisha katika ukurasa wake wa mtandao wa X akisema "Mtoto wa Mbowe (James Mbowe) ambaye ana kesi ya Madai Mahakamani kwa kosa la kutowalipa Mishahara wafanyakazi wake zaidi ya miaka 3 leo ana muhujumu Lissu kwa kumnyima vifaaa vya Mziki na Jukwaa kwa ajili ya Mkutano wake wa mapokezi ya tarehe 15 Feb, 2025 Mkoani Singida"


Je, ni upi uhalisia wa taarifa hiyo?

Ufuatiliaji wa kimtandao uliofanywa na JamiiCheck ulibaini kuwa taarifa hiyo si ya kweli wala haikuchapishwa na Lema katika kurasa zake rasmi za mitandao ya kijamii.

Aidha chapisho hilo limebainika kuwa ni la kutengenezwa ili kupotosha kwa kusambaza taarifa zisizo za kweli.

Hata hivyo madai yanayomlenga James Mbowe kuwa ana kesi ya Madai Mahakamani kwa kosa la kutowalipa Mishahara wafanyakazi wake zaidi ya miaka mitatu si ya kweli na hahusiki na kesi hiyo.

Hata hivyo Lema pamoja na James wameikanusha taarifa hiyo kwa nyakati mbili tofauti kupitia kurasa zao rasmi za mitandao ya kijamii.

Kwa kutumia Key word Search iliyotumia maneno "James Mbowe" JamiiCheck ilibaini kuwa chapisho hilo lilisambazwa zaidi katika mtandao wa Facebook. Tazama hapa, hapa,hapa, hapa, na hapa.
MBOWE NA MWANAE WASUSA CHADEMA WAGOMA KUMPA VIFAA VYA MKUTANO LISSU.

Mtoto wa Mbowe (James Mbowe) ambaye ana kesi ya Madai Mahakamani kwa kosa la kutowalipa Mishahara wafanyakazi wake zaidi ya miaka 3 leo ana muhujumu Lissu kwa kumnyima vifaaa vya Mziki na Jukwaa kwa ajili ya Mkutano wake wa mapokezi ya tarehe 15 Feb, 2025 Mkoani Singida.

#NoReformNoElection

View attachment 3231857
si watumie vifaa vya aliekua makamu mwenyekiti? au yeye Lisu alikabidhi nini kwa makamu mwenyekiti mpya mathalani gentleman ?

yaani mwenyekiti mzima wa chama analilia speakerz za mtu binafsi zenye thamani chini ya 2m? Kweli kuna uongozi hapo?🐒
 
MBOWE NA MWANAE WASUSA CHADEMA WAGOMA KUMPA VIFAA VYA MKUTANO LISSU.

Mtoto wa Mbowe (James Mbowe) ambaye ana kesi ya Madai Mahakamani kwa kosa la kutowalipa Mishahara wafanyakazi wake zaidi ya miaka 3 leo ana muhujumu Lissu kwa kumnyima vifaaa vya Mziki na Jukwaa kwa ajili ya Mkutano wake wa mapokezi ya tarehe 15 Feb, 2025 Mkoani Singida.

#NoReformNoElection

View attachment 3231857
Kwanza Lema uwe na adabu. Pili sio kazi ya watoto wa Mbowe kutoa vifaa vyao vya muziki kwa ajili ya chama, chama kijitegemee!
 
Chama kama hakina hizo vitendea kazi mwacheni Mzee wa watu.tumieni gharama kupata hivyo vitu kama siyo mali yenu,Lema anachojuwa ni kulalamika tu,hajuwi hizo spika zilikuwa mali ya nani hata.
 
Lisu hakujua kuwa akishinda itabidi aanze kujitegemea, na sikutegemea uongozi uliopita. Sasa ni wakati wake kusimama na uongozi ili chama kiendelee na shughuli zake bila kisingizio.
 
MBOWE NA MWANAE WASUSA CHADEMA WAGOMA KUMPA VIFAA VYA MKUTANO LISSU.

Mtoto wa Mbowe (James Mbowe) ambaye ana kesi ya Madai Mahakamani kwa kosa la kutowalipa Mishahara wafanyakazi wake zaidi ya miaka 3 leo ana muhujumu Lissu kwa kumnyima vifaaa vya Mziki na Jukwaa kwa ajili ya Mkutano wake wa mapokezi ya tarehe 15 Feb, 2025 Mkoani Singida.

#NoReformNoElection

View attachment 3231857
Lema acha kupayuka hovyo, kesi ya madai iliyoko mahakamani na kunyimwa vifaa vya mziki kuna uhusiano gani?
 
Nilisema narudia tena nampa Lisu miezi mitatu uongozi utamshinda ataanzisha migogoro isiyo na maana ili aonekane anahujumiwa
 
Kama hivyo vifaa ni mali ya James basi ana kila haki kukataa navyo.
 
MBOWE NA MWANAE WASUSA CHADEMA WAGOMA KUMPA VIFAA VYA MKUTANO LISSU.

Mtoto wa Mbowe (James Mbowe) ambaye ana kesi ya Madai Mahakamani kwa kosa la kutowalipa Mishahara wafanyakazi wake zaidi ya miaka 3 leo ana muhujumu Lissu kwa kumnyima vifaaa vya Mziki na Jukwaa kwa ajili ya Mkutano wake wa mapokezi ya tarehe 15 Feb, 2025 Mkoani Singida.

#NoReformNoElection

View attachment 3231857
Nmepita kwenye page ya Lema twitter sijaona post kama hyo hslafu mtoto wa Mbowe mwenye kesi ya kutowalipa wafanyakazi wake anaitwa Dudley Mbowe huyo James Mbowe sidhani kama ni mtt wa damu wa Mbowe.
 
Kwani hayo mapokezi hayawezi kufanyika bila vifaa vya muziki na jukwaa? Mwambieni Lisu apande hata juu ya mti team FAM wabaki na mziki wao na jukwaa lao. Huko wabaki na mwenyekiti wao
Hadi unapoona wanalalamika mitandaoni, ujue vifaa vina umuhimu, tena mali ya familia. Sasa kama kweli akina Lema wanajenga taasisi isiyomtegemea mtu mmoja mmoja, kulikuwa na haja gani ya yeye kupost malalamiko hayo? Mwambieni Lema aache ujinga
 
Back
Top Bottom