Kwetu tunachukulia poa ila wamalawi wanazungumzia kila siku Ziwa Malawi / Nyasa, Wanataka ziwa lote la nini ?

Kwetu tunachukulia poa ila wamalawi wanazungumzia kila siku Ziwa Malawi / Nyasa, Wanataka ziwa lote la nini ?

wastani kwa idadi

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2024
Posts
503
Reaction score
1,432
Nawashangaa sana wamalawi, yani karibia kila siku ajenda kuu za kimataifa lazima wagusie ziwa Malawi / Nyasa.

Mpaka wa kusini wa Ziwa Nyasa na Msumbiji uliwekwa kupitia mikataba kati ya Uingereza na Ureno, ambayo iligawa mpaka wa ziwa katikati.

Hata hivyo, mpaka kati ya Tanzania na Malawi ulitokana na mkataba kati ya Uingereza na Ujerumani 1890 enzi hizo Tanganyika ikiwa koloni la Ujerumani, ambao uliweka ziwa lote chini ya himaya ya Uingereza (baadaye likarithiwa na Malawi).

Lakini sheria hizo ni za zamani, kwani kwa mujibu wa sheria za sasa za kimataifa, mipaka ya maziwa kwa kawaida hugawanywa katikati (kama ilivyofanyika kati ya Malawi na Msumbiji).

Soma Pia: Serikali: Marufuku Kutumia Ramani ya Tanzania kutoka Google Kufundishia Wanafunzi, Inaonesha Ziwa Nyasa liko Malawi

Malawi haitaki kukubali sheria za kisasa za kimataifa, badala yake inasisitiza kufuata sheria za zamani.

Wao wanachoamini ziwa kuitwa Malawi ni lao, hapa kwetu kuna ziwa Tanganyika lakini tumegawana na Congo bila shida.

Yani inavyoonekana wao wanachotaka upande wa Tanzania tusitumie maji ya ziwa bila idhini yao, wavuvi wa upande wetu wasivue samaki, n.k.
 
1738343622514.png
 
Nawashangaa sana wamalawi, yani karibia kila siku ajenda kuu za kimataifa lazima wagusie ziwa Malawi / Nyasa.

Kama ni jina la Lake Malawi halina uzito kwasababu hapa kwetu tuna Lake Tanganyika lakini Border imechorwa pasu kwa pasu na Congo, wala hakuna shida.

Yani inavyoonekana wao wanachotaka upande wa Tanzania tusitumie maji ya ziwa bila idhini yao, wavuvi wa upande wetu wasivue samaki, n.k.
Soma andiko la kiuanazuoni limechambua jambo hili kwa undani.

 
Mpaka wa kusini wa Ziwa Nyasa na Msumbiji uliwekwa kupitia mikataba kati ya Uingereza na Ureno, ambayo iligawa mpaka wa ziwa katikati.

Hata hivyo, mpaka kati ya Tanzania na Malawi ulitokana na mkataba kati ya Uingereza na Ujerumani 1890 enzi hizo Tanganyika ikiwa koloni la Ujerumani, ambao uliweka ziwa lote chini ya himaya ya Uingereza (baadaye likarithiwa na Malawi).

Lakini sheria hizo ni za zamani, kwani kwa mujibu wa sheria za sasa za kimataifa, mipaka ya maziwa kwa kawaida hugawanywa katikati (kama ilivyofanyika kati ya Malawi na Msumbiji).

Malawi haitaki kukubali sheria za kisasa za kimataifa, badala yake inasisitiza kufuata sheria za zamani.
 
Ukitaka kumtesa Mtanzania basi mpe ukweli ulioandikwa aende akausome. Halafu ukute imeandikwa kwa kimombo, hapo ndio shida kubwa zaidi. Hiyo ni adhabu tosha kwake, na kuliko kuteseka atakacha kusoma.
Hiyo article imekaa vizuri mnoo, wapenda maarifa inawafaa.
Mpaka wa kusini wa Ziwa Nyasa na Msumbiji uliwekwa kupitia mikataba kati ya Uingereza na Ureno, ambayo iligawa mpaka wa ziwa katikati.

Hata hivyo, mpaka kati ya Tanzania na Malawi ulitokana na mkataba kati ya Uingereza na Ujerumani 1890 enzi hizo Tanganyika ikiwa koloni la Ujerumani, ambao uliweka ziwa lote chini ya himaya ya Uingereza (baadaye likarithiwa na Malawi).

Lakini sheria hizo ni za zamani, kwani kwa mujibu wa sheria za sasa za kimataifa, mipaka ya maziwa kwa kawaida hugawanywa katikati (kama ilivyofanyika kati ya Malawi na Msumbiji).

Malawi haitaki kukubali sheria za kisasa za kimataifa, badala yake inasisitiza kufuata sheria za zamani.
 
Nawashangaa sana wamalawi, yani karibia kila siku ajenda kuu za kimataifa lazima wagusie ziwa Malawi / Nyasa.

Sheria za kimataifa, nchi zikikutana kwenye maji mnagawana kati kwa kati.

Wao wanachoamini ziwa kuitwa Malawi ni lao, hapa kwetu kuna ziwa Tanganyika lakini tumegawana na Congo bila shida.

Yani inavyoonekana wao wanachotaka upande wa Tanzania tusitumie maji ya ziwa bila idhini yao, wavuvi wa upande wetu wasivue samaki, n.k.

Upande wa Msumbiji ziwa limepigwa pasu kwa pasu wapo kimya, kwanini kelele ziwe kwa Tanzania tu ?
Hivi ule wimbo wa mchakamchaka usemao “Banda wa Malawi atuvalia ngozi ya simba kututishia Watanzania. Hatujali, hatujali…” bado unaimbwa na watoto wa shule?

Wamalawi nadhani huwa wanatikisa kiberiti chetu. Yaani wanakubali kwamba mpaka wao na Msumbiji uko katikati ya ziwa Nyasa, lakini (sijui kwa kutuonaje sisi) hawakubali kwamba mpaka wao na Tanzania uko katikati ya ziwa. Hao wanataka shari tu!
 
Na mapandikizi ya Malawi yamejaa Tanzania na hawana vibali vya kuishi Tanzania. Serikali ifanye kama alivyofanya trump, hii ya kujifanya wakina mama huruma itakuja cost sana hii nchi.
 
Ukitaka kumtesa Mtanzania basi mpe ukweli ulioandikwa aende akausome. Halafu ukute imeandikwa kwa kimombo, hapo ndio shida kubwa zaidi. Hiyo ni adhabu tosha kwake, na kuliko kuteseka atakacha kusoma.
Hiyo article imekaa vizuri mnoo, wapenda maarifa inawafaa.
Umeisoma mkuu?

Mimi nimeisoma kurasa zote sijaruka hata paragraph moja.

Hata mimi imenifumbua macho mambo mengi sana nilikuwa sijui.

Mfano, nilikuwa sijui kuwa Nyerere na Kawawa walishakubali tangu miaka ya 1960s kuwa mpaka halali wa Tanzania na Malawi upo katika ufukwe wa mashariki wa ziwa Nyasa/Malawi.

Hili jambo lilishakubaliwa zaidi ya mara moja, tena mara nyingine jambo limeelezewa kama jibu la swali la bungeni Tanzania lililo katika Hansard.

Tatizo watu hawasomi.

Hili andiko la kiuanazuoni limeonesha suala hili lilivyo tata kuliko watu wengi wanavyofikiri.
 
Back
Top Bottom