Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

DR. Sasa ameanza kuwa Menghi au 6?Kulia lia tu ..wameniletea mtu jimbo langu,wanataka kunitoa. DR.amekuwa mpole sasa hivi..ananikumbusha ule wimbo mwisho wa mwezi ukifika lugha ubadilika..Majivuno kwisha,Sikonge ule mwimbo nani alimbaga vile mwanawane

Hebu tupishe wewe mwenyewe kaja usilete habari za mipasho na taarabu...tunadiscuss issue za maana hapa na Mwakalinga! Chukua mchele kachambue chuya jikoni, umenielewa?
 
Hahahahahh ama kweli ulimi hauona mfupa...NL connect dots!

Kwani hao De la Soul walikuwa wanamaanisha nini?

Kila mtu (hata wewe Masa, NL, NN) mna "ME, MY SELF and I".

Sasa Masa waweza kutuambia hiyo I au YOUR SELF yako ni nani?

NB: Masa, kama humfahamu Mwakalinga na waishi UK, basi juwa kuwa wakati wengine wanaenda shule, wee mkali ulikuwa ......... mhh, sintaandika maana ntaaibisha kwetu.
 
Kwa msiomfahamu, george mwakalinga. Picha yake hii hapa


097.JPG
 
Mkuu nyamaza imradi kaja mwenyewe aliye kuwa nae kule nyie wapambe nyamazeni sasa kwani na bungeni akipita mtaingia nae? Si mtaishia kwenye lango kuu na hapa nyamazeni mnamwaribia sasa kuna baadhi ya mambo amesha wakatalia kuhusu la laptop ni nyie wenyewe wapambe mlio vumisha.

Nimekuelewa mkuu.
Mi natoka kiwira si unajua tena mkuu amewachenga wazee wetu...mwishowe akanza kuwakimbia.
 
Sikonge,

Hapo juu ''Mwenyewe'' nani?

Mwenyewe Mwakalinga.

Si na yeye karudi UK jana na Mtanzania? Atakuja hapa kwa njia moja au nyingine. Si tuliambiwa na Malafyale kuwa: Wakati Mwakalinga George alikuwa Arusha, tayari pia alikuwa Kyela Kiroho.


Sasa ninaposema MWENYEWE kaja, ni kuwa kaja UK na ataweza kuwa JF muda wowote kuanzia sasa (ama ameshafika tayari) au yupo na sisi KIROHO. Na usishangae kuwa anaweza kuwa pia Kyela KIROHO akigawa LAPUTOPU kwa wanaKyela.

Una shida na hilo? Kama huelewi, basi KAWAWA FUNIKA KIKOMBE.
 
Hivi wewe nyani kwanini unataka ku reveal ID za watu?🙂 hebu edit kule bana.

Mwanakijiji tulikubaliana kutokubaliana zama hizo, ila kwa sasa tunazungumza lugha moja. Hamna shaka.

Hii thread imekosa mwelekeo sasa, kwanza mnamlazimisha mtu mwingine kusema yeye ni Mwakalinga wakati sio. Huyu Mtanzania alisomea pale Iringa A level shule ile maarufu ya zamani.

Wewe kama unataka ID ya kweli ya Mtanzania si umuulize tu akupe?
 
Huyo mbona kama mashaka yule wa kwa michuzi?

Samahani,

Huyo mnayemuona ni kweli kabisa kuwa ndiye George Mwakalinga (mzee wa Kiroho). Nafikiri sasa wote tumemuelewa George Mwakalinga wa U**** alivyo.

Mwenye macho haambiwi tazama. Mwenye hekima na atafahamu nina maanisha nani.

Kila la kheri.

Ha ha haaaaa George Mwakalinga umefahamika sasa. Kwi kwi kwiiiiiii
 
Last edited:
Hahahahahh ama kweli ulimi hauona mfupa...NL connect the dots!


Superb observation....

Masa /NN .....ningekuwa mimi nachange ID immediately!....hahhahah!

Kwani hao De la Soul walikuwa wanamaanisha nini?

Kila mtu (hata wewe Masa, NL, NN) mna "ME, MY SELF and I".

Sasa Masa waweza kutuambia hiyo I au YOUR SELF yako ni nani?

NB: Masa, kama humfahamu Mwakalinga na waishi UK, basi juwa kuwa wakati wengine wanaenda shule, wee mkali ulikuwa ......... mhh, sintaandika maana ntaaibisha kwetu.

Mkuu, Sikonge

Unazuga au unajibaraguza? .....kubali tu ulimi hauna ''mdzege'' aka mfupa!
 
Huyo mbona kama mashaka yule wa kwa michuzi?

Wewe umekazana unampigia debe kumbe hata sura yake humjui hiki ndicho siku zote kinacho tunamaliza waTanzania wengi tunaangalia majina tu na sifa kemkem bila hata ya kumfahamu mtu mwenyewe. Tumekwisha kwakweli Nyani Ngabu na wewe njoo ugombee Temeke tutakupamba tu.
 
Nyani;

Yule grandson wako mwenye matusi yupo wapi? Siku hizi hakai hata ofisini kupumzika au wamevunja ofisi ya mapumziko ya wabeba mabox na kutanua GODOWN?

Box mbaya sana, njooni tuwe wajasiriamali hapa bongo. Karibuni Mbagala
 
Huyu Mwakalinga ndio yule tulie pata habarizake, kwamba katumwamwa na wazee wa epa aka mafisadi papa aje amng'oe mwakyembe, lakini si katiba inamruhusu kuchaguliwa nakuchagua , tukae natuone lakini kama katumwa namafisadi hii haitakubalika akiliyake itakuwa fupi kama funza.
 
Ulikuwa Kyela na Mwakalinga? Vp ishu ya harambee kwa nini iliingia nyongo?
Kwanini usimshauri akagombea sehemu ingine kama vile Mbeya mjini kuliko kujenga uhasama na Dr.?

HARAMBEE YA UMOJA WA VIJANA WA CCM
Mkuu Field80, kwasababu umeuliza wacha nikujibu. Ilikuwa hii niandike baadaye ila kwasababu watu wengi wameulizia wacha nijibu sasa.

Umoja wa vijana wa CCM Kyela walikuwa na harambee yao ambayo nasikia waliiandaa siku nyingi zilizopita. Wakaamua kumualika mtoto wa JK. Huu mwaliko nimeambiwa walimpatia wakati wa uchaguzi wa umoja wa vijana ngazi ya taifa. Mwenyejiti wa vijana Kyela ni Dr Hunter au Dr. Hanta sijajua jina lake vizuri, ndiye alimwomba mtoto wa JK aende Kyela kusaidia harambee kwa ajili ya miradi ya vijana Kyela.

Huyu Dr. hunter nimewahi kuongea naye mara nyingi ila sijawahi kuonana naye uso kwa uso. Ilikuwa nonane naye tarehe 01/08/2009 lakini ilishindikana maana alikuwa down mno baada ya harambee yao kushindwa kufanyika.

Kuna mtu mwingine kaniambia Dr. Hunter alikubaliana na mtoto wa JK juu ya hili wakati mtoto wa JK anapiga kampeni ya mtu aliyetaka awe mwenyekiti wa umoja wa vijana wa CCM. Na kama kurudisha fadhila akawaahidi wakimwunga mkono basi na yeye atakuja kuwaunga mkono kwenye Harambee (hili sina uhakika nalo sana). Ilipofika huo uchaguzi ndipo wakampa mwaliko rasmi (sikumbuki uchaguzi wa vijana ulifanyika lini).

Baadaye tarehe ikapangwa kuwa ni Ijumaa tarehe 31/07/2009.

Kyela kuna kumbi chache sana ambazo ni kubwa kiasi cha kuchukua watu zaidi ya 200. Kama nakumbuka vizuri ni mbili tu, huenda kuna zingine. Ukumbi bora zaidi kwa maelezo ya baadhi ya watu ni ule kwenye jengo la Mwakalinga. Pia umezibwa kwahiyo sauti haitoki nje na una AC. Hao vijana wakaamua Harambee yao ifanyike hapo.

Siku hiyo ya Ijumaa Mwakalinga alikuwa kijijini kwao katumba na kulikuwa na mkutano wa kimila ambao uliandaliwa kumpa baraka mwanao. Hakuwepo pale mjini wala hakuwa na mwaliko wa kuhudhuria hiyo Harambee.

Kumbe kuna watu wamechukia kwanini ile Harambee ifanyike kwernye ukumbi wa Mwakalinga. Wakatengeneza majungu huku Dar na kutumia vitisho kwamba huyo mtoto wa JK anaenda Kyela kumpigia kampeni Mwakalinga na kwamba kuna vijana wamejiandaa kumzomea na kumrushia mawe.

Wakapeleka hizo habari mpaka kupitia watu wao walioko usalama wa taifa. Wakakuza jambo mpaka wakubwa wakaona hii inaweza kuleta balaa hasa wakiangalia zile vurugu za yule kijana aliyeuliwa na polisi. Inasemekana ikabidi viongozi waamue haraka haraka kwamba huyo kijana asiende.

Harambee hiyo ikavunjika, vyakula vikadoda, pesa milioni 155 walizotegemea zikawa hazipo tena, kisa wamefanya kosa kufanyia hiyo Harambee kwenye ukumbi wa Mwakalinga. Ndio siasa za Kyela hizo.

Mimi sikuwa na hili wala lile, nimerudi mjini hiyo Ijumaa usiku ndio naambiwa mtoto wa JK hajafika kwasababu mheshimiwa mmoja katia fitina.

Wao waliona wanamkomoa mwakalinga lakini ukweli ni kwamba hiyo center ilishalipwa hata kama mkutano ulivunjika. Kibaya zaidi ameishia kuwaudhi vijana wote ambao ndio walihangaika kwa nguvu na mali kuandaa hiyo Harambee.

Kama kuna mtu anamjua huyo mtoto wa JK basi amwulize kama amewahi hata kusikia jina la Mwakalinga.

Mambo kama haya ndiyo yanatufanya watu wengine tuamue kurudi nyumbani na kujaribu kuleta mabadiliko ya kweli. Mimi sikushangaa maana hata sisi huko nyuma tumeshafanyiwa visa kibao. Kuna bank walitaka kufungua branch pale kwa Mwakalinga, mhusika huyo huyo akaenda kutumia undungu na mtoa maamuzi ili kuzuia.
 
Wee Mshamba wacha siasa za akina Jesse.Maswali yako kumi hapo pumba tu,Kwani unataka kupewa jibu ili likusaidie vip?

Imbombongafu kati yangu mimi na wewe,wewe utakuwa mshamba zaidi ila hujijui tu. Jibu hoja kwa hoja siyo hoja kwa matusi. Toa hoja ili upumba wa hoja zangu ujulikane,otherwise wewe ndiye unaleta pumba na huo ni ushamba.

Unajua muda mwingine unapenda kitu au upande fulani mpaka unashindwa kutumia akili vizuri. Inaonyesha umemkubali sana Mwakalinga mpaka unashindwa kufikiria. Umeahidiwa nini? Au kuolewa na Mwakalinga.Wewe inaonyesha ni mtoto wa mwisho kwa mamayo,umenyonya sana kiasi kwamba umekuwa zezeta.

Leta hoja mwanamama siyo unaleta maneno ya saloon humu ndani. Jibu hoja kwa hoja,siyo unakurupuka tu.

Mtanzania kwa kujua nini ninachotaka kujua ameanza kunijibu. Leta hoja.
 
Mwenyewe Mwakalinga.

Si na yeye karudi UK jana na Mtanzania? Atakuja hapa kwa njia moja au nyingine. Si tuliambiwa na Malafyale kuwa: Wakati Mwakalinga George alikuwa Arusha, tayari pia alikuwa Kyela Kiroho.


Sasa ninaposema MWENYEWE kaja, ni kuwa kaja UK na ataweza kuwa JF muda wowote kuanzia sasa (ama ameshafika tayari) au yupo na sisi KIROHO. Na usishangae kuwa anaweza kuwa pia Kyela KIROHO akigawa LAPUTOPU kwa wanaKyela.

Una shida na hilo? Kama huelewi, basi KAWAWA FUNIKA KIKOMBE.

Haha!Hah!Hah!Hah!,,,,nimechoose ''UKAWAWA'' mkuu....isiwe tabu!
 
Back
Top Bottom