Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

Kuna uwezekano wa kupata maneno (tape) ya maneno ya Mwakyembe akisema kuwa Mwakalinga yuko jela UK? Itabidi haya yatumike sana wakati wa kampeni. Fanya juu chini upate tape ya maneno hayo.

Mpwa unaweza kusubiri sana huo mkanda mpaka masiya akarudi haujapatikana!
 
Mwakalinga ametoka kuongea na wana Kyela sasa hivi kwenye hotel ya kisasa ya Sativa

Huko Kyela inaonekana wamesha legalize kabisa nini?

Muhimu kutembelea hii Hoteli, if only to take a picture of the banner.
 
Huko Kyela inaonekana wamesha legalize kabisa nini?

Muhimu kutembelea hii Hoteli, if only to take a picture of the banner.

Huyo Mwakalinga atakuwa ni mjinga sana kama katika majumba yote yeye ataamua kufanyia mkutano kwenye hoteli ya Sativa ambapo ndio makao makuu ya Wapambe wa Mwakyembe na ndipo anapolala Mwakyembe akiwa Kyela.

Aache ukumbi kwenye center yake ambao ni wa kisasa zaidi, eti akafanyie mkutano Sativa?

Tutasikia mengi sana mwaka huu, wacha wengine tuendelee kucheka.

Nakubaliana na Sikonge kwamba huyu Mwakalinga ana nafsi tano, mara awe Sativa, hapo hapo anaonana na Lowasa Monduli, hapo hapo anatembelea mbuga za wanyama, hapo hapo yupo mahabusu UK, hapo hapo anasoma JF, kazi kweli kweli!
 
Mtanzania,
Mkuu ndio starehe ya JF kwani uzushi na vijembe ndio mseto unaokubalika..Wa ghana huita FUFU!
Tatizo moja tu ni kwamba tunagombana sisi wenyewe ktk swala dogo sana la Ubunge kiasi kwamba kumeingia uhasama mkubwa baina ya watu hawa...wakati mimi najua fika kwamba Mbunge hawezi kubadilisha kitu ikiwa serikali nzima imeisahau Kyela..That is a fact wakubali wasikubali maendeleo ya Kyela yanategemea huyo mbunge atakuwa na nguvu gani ktk serikali hiyo..

Haya madogo tu yamefikia hapo, sasa fikiria yanayowakuta kina Kibaki, Mugabe na wengineo upate kujua chuki za kiafrika huanzia wapi..Kinachoniuma mimi ni kufikiria tu kwamba hapa watu wanagombea zaidi lile jina la Ubunge -Tittle wakati hawa watu wawili wote ni muhimu kwetu sisi wananchi na ingekuwa vizuri wakajipanga wao kwa manufaa ya umma badala yake chuki inazidi kujengwa wakati Mwakalingfa hata hajarudi Bongo kugombea Ubunge.
Sasa fikiria akirudi na kutangaza itakuwaje, si ndio wataitafuta roho yake kabisa..Na yote hii kwa sababu tu mtu anataka kugombea Ubunge..
Jamani JK anazo nafasi 10 za kuchagua wabunge wake.. Mwakyembe bado anayo nafasi kubwa sana ya kuchukuliwa na JK kama mbunge wa Taifa, na hakuna sababu wala haja ya hawa ndugu wawili tena toka chama kimoja kugombania vipande vya nyama ktk sinia zima la Pilau..
Namwomba sana huyu Mwakalinga na Mwakyembe waondoe tofauti zao hata kama kuna chuki kubwa iliyotokana na Uzembe asili wa Kiafrika (Kujivunia cheo)..akumbuke tu cheo ni dhamana na udugu wetu hautoikani na kabila wala wilaya ni zaidi ya mapana hayo..
 

Mkuu Engineer,

Imefika wakati sasa mnaolripoti matukio yanayoendelea kujiri Kyela mje na ushahidi, hii maneno matupu hii ni kujaribu kupakaziana na kuzushiana.

Mi nadhani wale mlio upande wa Mwakyembe pamoja na wale wa kambi ya Mwakalinga mnapotoa shutuma au tuhuma, mara mwakyembe kasema hivi mara mwakalinga kafanya vile, muwe mnaweka na ushahidi. Hii itatusaidia kuendelea vizuri na mjadala kwa kujadili hoja za msingi badala ya kuendelea kujadili ushabiki na majungu.

Naamini tangu tuanze kuwajadili Mwakyembe na mwakalinga kila mmoja amejaribu kuelezea namna anavyomuona nani anafaa kuwa mbunge wa kyela, sasa tufike mahali tuweke pembeni ushabiki na majungu, tuzungumze facts.Vinginevyo tutakuwa tunafanya debate isiyo na maana yoyote kwa maslahi ya kyela na Tanzania kwa ujumla.
 

Mwita,
Achana na Said Nkumba, yule sasa hivi angelikuwa JELA huko Texas kwa Shilom na mke wake wa Kizungu, tungelikuwa tumeshaanza kumwita DEAD MAN WALKING. Hapo inasubiriwa tu sahihi ya Gavana Bush.

Hayo maneno MEKUNDU ya kwako, umeandika maneno makubwa sana. Kuna vitu tunafahamu ila wewe hufahamu. Kama ungelikuwa mfuatiliaji wa Makala hizi za Mwakyembe, basi pana wakati kama sikosei Mwiba aliliandika. Labda tu nikuambia kwamba "Ndiyo maana Mwakyembe alikuwa na uhakika ataukwaa na yeye UWAZIRI kwa kazi yake, mara baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Ila Kikwete akamuweka chini. Na hilo sishangai maana kama wengine kama mimi hapa Sikonge napata habari zake, je Mkwere si ana nyingi zaidi?

Mwita, hii ni SIASA. Mwakalinga akishinda, naona nusu ya ushikaji utakufa siku hiyo hiyo kwi kwi kwiiiiiiiii. Naomba Mungu ASIZUZUKE na cheo kama ambavyo hajazuzuka na ELIMU, Kukaa Ulaya, Pesa na kazi nzuri.
 

Mkandara,
Hamna cha kuongeza wala kupunguza. Ukianzia ukurasa wa kwanza, na kusoma ujumbe wa ndugu yangu Masanilo, unapata picha ya wazi kabisa TAI walikuwa wanasubiri jina la Mwakalinga litokee JF na walibebe juu juu.
Kwa kuwa hawamfahamu Mwakalinga, na kazi anakofanyia hawawezi kupata data zozote, inawawia vigumu sana kupigana na adui ambaye yeye anawaona mabaya na mazuri yao yote, na wao hawamuoni.

Hii inakuwa kama mtu mwenye kigugumizi akigombana na mtu. Wee unavyompa maneno yake na yeye hawezi kukujibu, hawa jamaa huwa wanakuwa watu wa hasira sana sana.
Wengine tunajitahidi kutoa data za Mwakyembe ambazo zinajulikana. Hatutungi habari zozote kama Malafyale. Pia kuna mtu anaitwa ENGINEER. Huyu bwana kila mtu anamfahamu kuwa ni mtu wa kuongezea chumvi na hampendi Mwakyembe. Nilishasema waziwazi kuwa huyu hata kama angeligombea Lowassa jimbo la Kyela, Mugabe, RA, Chenge nk basi yeye angelisaidia hao watu. Sidhani kama anampenda Mwakalinga ambaye ndiyo kwanza juzi kakiri mwenyewe kuwa "nilishangaa kumuona G. Mwakalinga" -kwa mara ya kwanza.​
Sasa Mkandara hebu niambie hili jambo kweli linawezekana? Na hili kaliandika Malafyale na kuja kupewa suport na akina Masanilo, Mwafrika, Shalom, Yo Yo, NN, Nsesi nk nk.
Kwamba Mwakalinga kwa kutumia Nguvu za kiroho:
Alikuwa Arusha na hapohapo: kuwan na Lowassa aliyekuwa Dodoma bungeni, kufungua mkutano Kyela, kutembelea vijiji vya Kyela, kuwa jela UK, kuja kujibu shutuma JF.​
Na huyo anayeandika ni Malafyale. Tena aandikia kutoka Texas anapoishi na yeye na kutunzwa na Mkewe wa Kizungu. Hana cha kufanya na muda wote anautumia kutunga Pumba.
Labda tuwafungulie makala maalumu Malafyale na Engineer. Washabiki wawe Masanilo, Shalom na upande mwingine Samwel na Ibombo
 

Sikonge,
Endelea kumuombea tu mwakalinga kama ulivyoanza.Cheo ni maneno nyingine ndugu yangu acha kabisaaaa. Ukiwa na vijisenti hakuna wa kukuhofia sana, sana sana utaishia kutoa viofa vya bia na nyama choma kwenye mabaa na watu watazidi kukuimbia mapambio, lakini madaraka?!hiyo kitu ingine, hicho ndio kilevi kinachowashinda nguvu wengi.

Halafu mkuu usisahau huko ulaya ni ugenini, huwezi kuwa na jeuri kwenye nchi ya wenyewe, huko ulaya sio kama bongo tunanyanyaswa na wageni ndani ya nchi yetu.(nimekumbuka ushenzi wa hawa waburushi wa north mara na wale wachina waliomfungia mmasai ndani ya kontena kule manyara)
Pia ni rahisi kumuona mwakalinga KUWA ana vijisenti kibongo bongo, LAKINI kiulaya ulaya atakuwa mtu wa kawaida sana, isitoshe huko ulaya ni watu wengi sana wanavyo kwahiyo anakuwa mule mule tu.

Ngoja niwahi Gokona nikaangalie kama nitapata vijimawe vya dhahabu angalau nipate mlo wa kesho, i'm out mazee.
 
I love watanzania, wanaichukia CCM ila wanampenda Mwakyembe!
 
Moshi wa kwenye matanuru ya tumbaku kwa mtoto madhara yake huonekana ukubwani....! Ile kambi nyingine hujaitaja akina Samwel, Mtanzania, Kigogo na Sikonge. Binadamu bwana kunya anye kuku akinya bata kaharisha!

Si lazima nikubaliane na Mtanzania na hapa JF hatujuani hiyo Elimu unayoona wewe Mwakalinga anayo umejuaje kama Kanda2 si wa level hiyo ama hata kumzidi, acha mambo yako ndugu yangu.

Kinachosikitisha alichofanya Mwakyembe hamkioni ila mnataka tumpe taulo Mwakalinga simply anaukumbi Kyela na Supermarket na sijui hotel, hakuna substance hapo, atafanya nini Kyela maana huyu ukifatilia posts zake zote ni mtu mwenye chuki na kwa kuwa ametumwa sidhani azima yake itafanikiwa huyu si wa wanaKyela akagombee kulee....mumeanza name calling sijui ndo sera za Mwakalinga, or texas or shalom ni Masa na hata yule mzee wa JF mnamwita ni Mwafrika sijui Nsesi acheni hizo! No to Mwakalinga 2010 in the polling ballots....hiyo ndo habari!
 
I love watanzania, wanaichukia CCM ila wanampenda Mwakyembe!

I hate CCM to death ila wale walio kimakosa kule I fully supports them....kama akina Kilango, Mwakyembe, etc etc wameonyesha wanaweza na wanauthubutu.
 
Tatizo la Mwakyembe amejaa uongo na uzushi mwingi, ndio maana Kikwete alimnyima uwaziri safari zote mbili na hatapa ng'oo kama Kikwete akiendelea kuongoza Tanzania pamoja na kujikombakomba kote.

Watu wana macho na wanaona nini kinafanyika Kyela na nani anafanya mambo Kyela. Anacha kuchapa kazi muda wake umekwisha sasa anadhani majungu ya uongo yatamuokoa 2010. thubutu.

Kama Mashimba alifukuzwa kwa sababu ya Mwakalinga, je Hawa ngurume alifukuzwa kwa sababu ya nani? Njia ya muongo fupi.
Tatizo wapambe wake wote ni mbumbuu, watamshauri nini? utopia tu.

Anatapatapa ameshindwa pa kutokea na hana jipya, upeo wake kimaendeleo umefikia kikoma.

Kgwamaka
 
Shoshushoshuuuuu chichiiiiii chachaccchaaaa. Napiga mluzi tu hapa.
 

Hawa Ngurumo
Naye kishatimuliwa huyu mama sitokaa nimsahau,
 
Kwa mtindo huu Tanzania itaendelea kuwa kichaka cha mafisadi.Hivi ninyi mnaompigia debe huyo Mwakalinga mmeshajiuliza AMESHAWAFANYIA NINI WAPIGA KURA WA JIMBO HILO badala ya hadithi za ATAFANYA HIKI NA KILE?

Siasa za kuangalia personality ya mtu zimechangia sana kutufikisha hapa tulipo.Badala ya kuangalia uwezo wa mtu (kwa kipimo cha aliyokwisha accomplish kwa eneo husika au taifa) watu wanaangalia sura (like ilivyokuwa kwa JK),upole,kuishi ughaibuni,idadi ya digrii (including za vyuo feki) na upuuzi mwingine kama huo.

Simpigii debe Mwakkyembe lakini angalau yeye anaweza kutembea kifua mbele na kusema HE DARED!What about huyo Mwakalinga?Japo simfahamu vizuri lakini taarifa kwamba ameombwa na WATU flani kupambana na Mwakyembe-sio kwa vile ana uchungu wa maendeleo ya wana Kyela bali kumdhibiti Mwakyembe-inanifanya nimweke kundi moja na mafisadi.Simple truth is,akishinda (which means kumwangusha Mwakyembe) mission yake na mafisadi itakuwa accomplished.Mnaopayuka kumpigia debe mtakuwa wa kwanza kuja hapa kulalama "oh huyu jamaa tulitegemea angefanya hiki au kile lakini wapi..." Unfortunately,that would be too late to change anything.

Jiulize: Amekufanyia nini na sio untarajia atakufanyia nini.Huu sio wakati wa kucheza karata-tatu za kisiasa,we need people who are truly committed to kuangamiza ufisadi na mafisadi.Na hata kama ana mapungufu,Mwakyembe has shown a way.What about Mwakalinga?
 
Mlalahoi,

..Mwakalinga is not the incumbent candidate kwa hiyo wananchi hawapaswi kumchagua[ikiwa atapita] kwa kuangalia amefanya nini huko Kyela.

..ikiwa Mwakalinga atagombea basi wananchi wanapaswa kuangalia kile atakachowaahidi na kupima kama ana uwezo,uzoefu/background, na resources, kutekeleza ahadi zake.

..Dr.Mwakyembe kwasababu amekuwa mbunge kwa miaka mitano anapaswa kupimwa kwa yale aliyoyafanya ktk uongozi wake, pamoja na ahadi mpya anazotoa.

..tatizo ni kwamba hoja hii imetawaliwa zaidi na ushabiki. wachangiaji wamejikita zaidi ktk kurushiana vijembe badala ya kujenga hoja za nani kati ya Mwakyembe na Mwakalinga atawafaa zaidi wananchi wa Kyela ktk harakati zao za kujiletea maendeleo.
 

Madesa Hayo
Hivi Mbeya kuna Swing states or swing Villages
Sasa huyu mwakalinga kama yeye ni mtaalam wa Computer si bora awekeze kwenye fani yake ya Computer kwani nchi inahitaji wataalamu wa Computer than Wabunge
 
Hivi naomba kuuliza what's so special about Kyela? ni kwa sababu ya Mwakalinga na Mwakyembe au kuna cha zaidi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…