Kwa mujibu wa ratiba ya CCM Wilaya ya Kyela , Leo tarehe 11/9/2020 ndio siku iliyopangwa kuzindua kampeni za uchaguzi, ambapo Mgombea ubunge wake aitwaye Kinanasi ambaye inasemekana miezi 6 iliyopita alikuwa hajui kusoma wala kuandika angetambulishwa rasmi akiwa pamoja na wagombea udiwani wa kata zote.
Hata hivyo, wakiwa katikati ya uzinduzi wao zikaletwa habari za kuungua moto kwa hospitali ya Wilaya hiyo, ambapo baadhi ya wagonjwa walikimbia wakiwa na dripu zao mikononi huku wakiwa wamevaa mashuka ya hospitali, jambo hili halijashangaza sana maana ni wazi kwamba ajali haina kinga, lakini wazee wengi wa Kyela wanatafsiri hali hii kama Mkosi mkubwa kwa chama hicho na wengi wamekitabiria kuangukia pua kwenye uchaguzi huu, wanaamini kwamba safari ya CCM imeanza kwa mguu wa kushoto kitu ambacho si ishara nzuri.
Sisi wengine tunayachukulia kwa umakini mkubwa uliojaa tahadhari sana maono ya Wazee, maana iko wazi kwamba Wazee ni hazina na wameona mengi sana.