Ladies kama wewe utachukua hatua gani?

Ladies kama wewe utachukua hatua gani?

Kwa kweli watu walio mdanganya all this time na wanao mfanyia hivo ghafla ni adui zake. ni bora akate mahusiano nao kabla hawajampangia mengine. Aondoke na mwanae (wanae) wote. Huyo jamaa na Housegirl wake wanastailiana, asiwaingilii kati.
 
pole yake jamani .Hawa watu wabaya sana wangeweza hata kumzuru.Ila hapa tunajifunza wakina mama kutowaamini sana hawa wasaidizi wa ndani.
 
, aliyemvumilia
Nyodo?? Walitafuta suluhu wapi mambo yakashindikana? Ivi is it possible mwanamke kumfanyia mumewe nyodo alafu ampende h'gal kiasi hicho na kumuachia uhuru wote huo??(may b)! Mwisho wa siku mi nasema ni bora kujiengua. Huyo mwanamke hapendwi, believe me u...! Yaani mwanaume anafikia hatua ya kujilipua kisa h'gal?! Huyo anakuwa ameshajua kabisa reaction itakuwa ni negative na hivo ameshaamua vyovyote na iwe hata uamue kuondoka kwake poa tu! Hata kama mwanamke alianza nyodo h'gal akiwa ameshazaa, mie bado nashawishika kusema hilo lilikuwa limepangwa tu, we unadhani hiyo siri ingetunzwa mpaka lini?? Au kwa nini asingemhamisha huyo h'gal kimya kimya ili awe anaenda kupata faraja kwa uhuru? Jamani akufukuzae hakwambii tokaa...............!

kipipi my dia si kwamba ninamkandamiza huyu Mke wa ndoa but najaribu kuielewa hii hadithi ambayo kwa kweli ilininyima usingizi jana. Niliposema nyodo nilikuwa ninaangalia tabia ya wanawake wengi ambao tunajisahau tukisha simika mizizi ndoani (umeolewa umezaa basi unajiona unastahili na saa nyingine hata hashma na upendo kwa mwenzio vinapungua kama si kwisha kabisa) huzaa madharau na ugomvi kila kukicha. Suala la kutafuta suluhu si tija, vipi kama suluhu ilitafutwa baada ya mama kuona kuwa sasa namwagwa?
umeuliza kama ni possible kwa mwanamke kumwonyesha nyodo mumewe wakati anampenda msichana wa kazi! Well si kitu cha ajabu hasa kama anajiona anaye msichana wa kazi ambaye ni mwaminifu kwake na anamlelea wanae vema na pengine anamfichia siri zake za kurudi usiku n.k. (Najaribu tu kusoma kwa nguvu nielewe; ni assumptions zangu tu)

Bado nashindwa kuelewa kwa nini mwanaume huyu afanye hivi kwani kwa njia aliyoitumia ni kama vile amaamua kwa makusudi kabisa kumchapa kibao cha maumivu mkewe kama vile mtu anayelipa kisasi kwa mtu aliyemkosea. Ni kama faru aliyejeruhiwa hapa otherwise angefanya hicho ulichokielezea mwishoni mwa post yako..yaani kimya kimya na maisha yakaendelea!

Hapo kwenye red hebu jaribu kupageuza pasomeke ameamua kujilipua kisa MWANAMKE anayemuheshimu, aliyemvumilia na aliyemwaminifu kwake!
 
Salam MMU membaz miss u big T.
Naanza na mkasa unaonishangaza !
Huyu jamaa ,Kabla hajaoa alienda kijijini kwao na kuleta binti mrembo akiwa ni mfanyakazi wake wa ndani
Amekaa nae muda mrefu huku binti akishuhudia pilika za jamaa wakati akileta girlfriends zake Na kufanya utambulisho mzuri tu kuwa ni msichana wake wa kazi na vile vile anamchukulia kama ndugu yake.
Muda wa kuoa ulifika jamaa kaoa na kuleta mke ndani ya nyumba wamekuwa na mahusiano mazuri tu kati ya mke/ mme na binti wa kazi.
Mama mwenye nyumba mungu amemjaalia watoto wawili.
Mara binti wa kazi nae alibeba mimba kisha alimleta jamaa na kumtambulisha kwa dada na shemeji kama ndo baba mwenye ujauzito
walimpokea vyema na kumuuliza nini hatma yao ,jamaa alisema atamuoa mambo yakikaa vizuri
Alienda kwao kujifungua na kukaa miezi sita kisha kurudi kuendelea na ajira yake kama kawaida.
Alifanya vema sana ktk kazi zake za ndani na kumuheshimu sana mke wa jamaa
Mama alimpenda sana na kumchukulia kama ndugu wa mmewe na wake pia,pia baba wa mtoto alikuwa anakuja mara kwa mara kumuona mwanae.
Jamaa baada ya mtoto wa H/G kutimiza miaka 3 Ndipo kaamua kuvunja ukimya kwa kuita ndugu na jamaa kuwatambulisha kwa binti wa kazi
bila kusita alisema huyo binti ana uhusiano nae toka kijijini na hata kabla hamjamuoa wife na mtoto ni wake na ameamua kumuoa kama mke wa pili
Na pia ameshamjengea nyumba anataka kumwamisha………………………
Haya kina mama wenzangumlio kwenye ndoa na mnaotarajia kuingia kama wewe ungechukua maamuzi gani?
Hekima inahitajika hapa …maana mama mwenzetu amechanganyikiwa.
Na nyie baadhi ya akina baba kwa nn mnafanya hivi lakini?
Mbona mnatuumiza sana !
Based on true.

...maisha kwa upande mwingine chukulia tu kama redio kasseti...
9977030-vintage-radio-cassette-recorder-isolated-on-white--cassette.jpg


badala ya kubonyeza rewind > stop # buttons kila mara...
wewe jitie hamnazo bonyeza fast forward tu >>

mpaka hapo walipofikia, kama hakuna kero kubwa kubwa kwanini ajiondoe kwenye hiyo ndoa? too late... amekuwa anaishi na huyo mke mwenziwe miaka nenda rudi...hakuna u - turn itayosaidia kujifariji na "laiti ningejua...!"
 
huyo jamaa ni mzinzi kama wazinzi wengine tu hana lolote,ashukuru tu kwamba amezaa na huyo mama,ningemshauri aachane naye hana maana kwake hamuheshimu hata kidogo,lakini kikwazo hao viumbe wataenda wapi? basi inabidi mama uvumilie tu,ila aweke masharti asiingiliwe sana na huyo kiumbe H/g
 
Huyo mama amwambie mumewe akakae na hg huko alikomjengea huyo hg nyumba, amuache hapo ye na wanae apumue kwanza baba aendelee kutunza wanae na mkewe. Ila wapumzishe mahusiano mpaka akili ya huyo mama itakapotulia.
 
Jamani mwenzenu naumwa nachungulia kidogo na kutoka ..
 
, aliyemvumilia

kipipi my dia si kwamba ninamkandamiza huyu Mke wa ndoa but najaribu kuielewa hii hadithi ambayo kwa kweli ilininyima usingizi jana. Niliposema nyodo nilikuwa ninaangalia tabia ya wanawake wengi ambao tunajisahau tukisha simika mizizi ndoani (umeolewa umezaa basi unajiona unastahili na saa nyingine hata hashma na upendo kwa mwenzio vinapungua kama si kwisha kabisa) huzaa madharau na ugomvi kila kukicha. Suala la kutafuta suluhu si tija, vipi kama suluhu ilitafutwa baada ya mama kuona kuwa sasa namwagwa?
umeuliza kama ni possible kwa mwanamke kumwonyesha nyodo mumewe wakati anampenda msichana wa kazi! Well si kitu cha ajabu hasa kama anajiona anaye msichana wa kazi ambaye ni mwaminifu kwake na anamlelea wanae vema na pengine anamfichia siri zake za kurudi usiku n.k. (Najaribu tu kusoma kwa nguvu nielewe; ni assumptions zangu tu)

Bado nashindwa kuelewa kwa nini mwanaume huyu afanye hivi kwani kwa njia aliyoitumia ni kama vile amaamua kwa makusudi kabisa kumchapa kibao cha maumivu mkewe kama vile mtu anayelipa kisasi kwa mtu aliyemkosea. Ni kama faru aliyejeruhiwa hapa otherwise angefanya hicho ulichokielezea mwishoni mwa post yako..yaani kimya kimya na maisha yakaendelea!

Hapo kwenye red hebu jaribu kupageuza pasomeke ameamua kujilipua kisa MWANAMKE anayemuheshimu, aliyemvumilia na aliyemwaminifu kwake!

Nimekuelewa dear! Lakini nikiiconsider hiyo paragraph yako ya mwisho naeza pata jibu kuwa h'gal kwa sasa ndie chaguo la mume i.e amebeba asilimia kubwa (ndo maana mume kajitosa), and if thats so......now what next??? (heheheee sijasahau nakudai juice yangu)
 
Back
Top Bottom