Lady Jaydee: Clouds FM ni wanafiki, wanataka wahongwe ili wapige nyimbo za wasanii

Lady Jaydee: Clouds FM ni wanafiki, wanataka wahongwe ili wapige nyimbo za wasanii

sijawahi kuwa shabiki wa Jide. I'm not dissing. Lakini hamna anything special kuhusu uimbaji wake, ni kama mimi niende kurecord tu kwenye beats poa.
 
Kwani aliyekutoa ana haki ya kukushusha? Kwani mtu akikusaidia ina maana ana haki ya kufanya lolote juu yako sulalamike?

kuacha kupiga nyimbo zako ndo kukushusha?si zipo radio/tv stations nyingine kwa nini usipeleke huko zikapigwa?kama yeye alifanyiwa promo enzi hizo kuna ubaya gani na diamond akafanyiwa same thing sasa?au jide anamiliki/anahisa clouds?acheni ushamba
 
Hakuna siku aliyoniudhi Mhe.J 2nyi kama ile siku aliyokubali beef liishe hawa Kloudz wanaua sanaa yetu hapa TZ lakini watu hawaaamini
 
Tatizo letu wabongo ni kukurupuka kusiko na kufikiria... kwa masikio yangu nimeusikia wimbo huu ukipigwa mara kadhaa kwenye kituo hicho halikadhalika niliusikia ukiwa introduced kwenye radio hiyo kwenye kipindi cha xxl na pia nimeisikia mara kadhaa kwenye vipindi tofauti... sitetei may be kama kuacha kuipiga wawe wameacha kuipiga hivi karibuni... ila akisema wimbo wake hauchezwi ni muongo... then inaonesha dhahiri wengi wanaocomment katika hili si wasikilizaji wa radio ila ni ushabiki ndio umetawala.. ni kweli wana matatizo ila si katika hili... binti ana jengine sio suala la wimbo kutokuchezwa hiyo ni sababu ya kujikusanyia idadi ya wafata mkumbo na ushabiki.

true.very true
 
LADY JAY DEE: CLOUDS FM NI WANAFIKI, WANATAKA WAHONGWE ILI WAPIGE NYIMBO ZA WASANII

Mwanamziki nguli wa Bongofleva, Lady Jay Dee ameamua kuwapa madongo Clouds FM kupitia Twitter leo kutokana na wimbo wake mpya uliotoka hivi karibuni Joto hasira kutopigwa katika radio hiyo. Jay Dee ameandika kuwa radio ya watu isiyopiga nyimbo za wasanii wa watu ila wasanii wao tu.
>> Angalia tweet za Queen of Bongofleva huyo pichani
Jay Dee pia anaonekana kujizatiti na kujiamini kuonyesha kuwa yupo kwa lolote yeye kama Komandoo Binti Machozi aliandika tena "Kill me if u can. Am on Fire, siogopi ng'oooooo Jipangeni, Ni kweli nimelamba sumu, lakini hainidhulu. Nakunywa maziwa daily, I will survive".

Hata hivyo si Jay Dee pekee kuanza kulaumu kwani wapo wanamuziki wengine wanaolaumu nyimbo zao kutokupigwa hasa Mr II aka Sugu

578053_452019121541333_147761534_n.png
 
Aende kwenye Maskani ya Mume wake Times Fm,mnafiki sana

Inamaana alikuwa hajui kama hao Wafu ni wanyonyaji?

Ndo kaona leo?

Wasanii wangapi wanakosa haki yao kwasababu ya hao MBWA!?alikuwa halioni hilo?

Unafiki kitu kibaya sana

Bora hata yeye huu mziki umemtoa,watu wamesota sana kutokana na huu unyonyaji wa hawa Wanyama

Endeleeni kujipendekeza nyie si ndio mnaowapa chat hao

HAKUNA RANGI MTAACHA KUONA!

Sent from BlackBerry 8520
 
Dada na wewe pumzika kidogo. Wakati mumeo yuko radio ya watu alikuwa haachi kupiga nyimbo zako. wakati mwingine nyimbo mbili ndani ya kipindi kimoja cha jahazi, utafikiri wewe ni msanii pekee mwenye hati miliki ya Clouds.

Ni hii hii radio ya watu walioipa promo Nyumbani lounge Kupitia Gadner, sasa leo hii mmetoka wote unaanza kelele. Ningekuwa mimi ningenyamaza na kufuta machozi mi binti machozi.
 
Sasa zile kwaya anazoimba nani anataka kusikia...???? Watu wamejipanga wamemkalia juu anahaha kutafuta mlango wa kutokea heheheheeeee.... jitahidi kuomba mungu akupe mtoto walau mmoja ulee mama.. huu muziki unaung'ang'ania ila wenyewe haukutaki... nilikukubali way back not now adayz hata ningekuwa mimi dj au presenter nisingecheza ngoma zako.. hauvutii kusikilizwa Mama.
 
Mbona kaongea tena kimafumbo kama yeye kweli ni mwanaume na ameamua kufunguka?!
KakaJambazi Jaydee ni mwanamke bhanaaa!...........wape hi radio ya 60.6% a.k.a kipaza sauti cha kawambwa
 
kwa nyie mnaoamini katika hizo Dini zilizoletwa na Meli basi nadhani mnafahamu kuwa miongoni mwa dhambi inayozungumzwa sana ni dhambi ya Unafiki.

Huyu makengeza alikuwa wapi siku zote wenzake walipokuwa wanalalamikia haya yanayomkuta sasa?

Leo hii shuzi linamnukia anajishaua kukimbilia Twitter, alikuwa wapi siku zoote wenzake walipokuwa wanalalamika?

Afunge bakuli lake na aache unafiki.
 
Nadhani kinachomuma Jide ni Clouds kufagilia SKYLIGHT BAND.

Hili nalo neno. Na kingine ni pale mumewe alipoamua kuenda Times Fm badala ya kurudi Clouds na pia baada ya Jaydee kupeleka kipindi chake EATV.Ila ninachomlaumu huyu dada,prof J,Q Chillah na wasanii wengine wakubwa wanaobaniwa ni kwamba wakati Mh.Sugu anapambana na tabia hii chafu,hawa walinyamaza kimya hata kukemea tu walishindwa!,hawajachelewa,wajiunge na harakati za Sugu!. Q Chillah pia aliwahi kulalamika na kuwachana live watangazaji wa XXL wa radio hiyohiyo tena wakiwa wanamuhoji. Chunguza umesikia lini mara ya mwisho nyimbo za 20% kwenye radio hiyo? Tena zote zina beat na maadili mazuri tu! Kuna nyimbo hapo Clouds zinapigwa kutwa mara tano na ukizichunguza hazina radha wala maadili!
 
kwani lazima iwe cloudh tu mbona twenty alitolewa na magic na tuzo tano akabeba ile ni biashara wanahaki ya kuangalia biashara yao mbona nyimbo mpya ya roma .qchief sizikii
 
kuacha kupiga nyimbo zako ndo kukushusha?si zipo radio/tv stations nyingine kwa nini usipeleke huko zikapigwa?kama yeye alifanyiwa promo enzi hizo kuna ubaya gani na diamond akafanyiwa same thing sasa?au jide anamiliki/anahisa clouds?acheni ushamba

Hiyo nayo point uliyoongea kuna ukweli asilimia kubwa ndani yake..... kwa ku urgue with point nakupongeza sina commnet.
 
Hivi bongo kuna redio moja tu??
Hawa wasanii wa bongo mi nawaita wajinga kwa sababu wao ndio wanafiki na wataendelea kuburuzwa na hao clouds mpaka mwisho wa dunia, unafiki wa kwanza ni kutoziamini/kudharau redio nyingine na kuona kuwa nyimbo zao haziwezi ku hit mpaka zipigwe na clouds. Na unafiki wa wao kwa wao wasanii ambao wanatukuzwa na kupambwa kijinga na clouds kwa nia ya kuibiwa wanawatenga wasanii wengine wanajiona wao ndio wao lakini wakibwagwa ndio wanalalamika na kutaka msaada(ndio yaliyomkuta jay dee) ushauri wangu kwa wasanii jikazeni lenu liwe 1 unganeni kiukweli sio kinafiki, mtakuwa matajiri wa kubwa na hamtolalamika ovyo. Maana kwa unafiki wao ndio unawasumbua
 
Back
Top Bottom