Laiti Hayati Magufuli asingeliua upinzani hiki kiburi cha kina Makamba kisingekuwapo

Laiti Hayati Magufuli asingeliua upinzani hiki kiburi cha kina Makamba kisingekuwapo

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200
Ni wazi matatizo yanayoikumbuka Tanzania kwa sasa ni matokeo ya Hayati Magufuli kuufifisha upinzani huku aliamini ni salama kwake hadi hapo angemaliza Utawala wake pasiwepo wa kumsumbua. ALIJIDANGANYA!

Hayati Magufuli pamoja na mazuri yote aliyopata kuyafanya lakini hilo la kuufifisha upinzani na kuunyima fursa ya kuwamo Bungeni hakika kwalo ndilo pungufu na udhaifuye mkubwa na ambao lazima aujutie hata huko alipo.

Leo hii kwa mfano laiti Bungeni wangekuwapo wabunge mfano wa Joseph Mbilinyi hakika hicho kiburi cha wanaojiita CCM yenyewe akina Makamba na Nape hakika kisingekuwepo.

Tabu za umeme na gharama za mabando kupanda holela na asiwepo japo Mbunge wa kuhoji seriously ni kwa sababu waliomo wanahofia 2025 kwenye kura za maoni kutemwa na wamebaki kujipendekeza tu.

Haya yote yanatusibu kwa sababu Hayati Magufuli aliamini mfumo wake huku alisahau kuna kufa. Ona sasa tabu tunazozipitia!

Magufuli kwa hilo ulitukosea sana!

R.I.P.
 
Kipindi anakanyaga watu watu vichwani mlishangilia sana kwakua mlifikiri angeishi milele. Tunapopigania mifumo tunamaanisha maana watu hufa mifumo itabaki milele.

Pole sana inawezekana nawewe ulikua engineer wa ule uhayawani mlifanya 2020.
 
Tabu za umeme na gharama za mabando kupanda holela na asiwepo japo Mbunge wa kuhoji seriously ni kwa sababu waliomo wanahofia 2025 kwenye kura za maoni kutemwa na wamebaki kujipendekeza tu.

Magufuli kwa hilo ulitukosea sana!
 
Ni wazi matatizo yanayoikumbuka Tanzania kwa sasa ni matokeo ya Hayati Magufuli kuufifisha upinzani huku aliamini ni salama kwake hadi hapo angemaliza Utawala wake pasiwepo wa kumsumbua. ALIJIDANGANYA!

Magufuli kwa hilo ulitukosea sana!
Nani kaua upinzani.. hakuna wakuua upinza na wala hajazaliwa na hatazaliwa.
 
Wapinzani hawajawahi kusikilizwa bungeni, zaidi wakiwa "wasumbufu" walikuwa wakiitiwa polisi na kutolewa nje kama vibaka, huyo Sugu uliyemtolea mfano ni mhanga wa huo ujinga, hivyo usimlaumu Magufuli kwa hilo.
 
Wapinzani hawajawahi kusikilizwa bungeni, zaidi wakiwa "wasumbufu" walikuwa wakiitiwa polisi na kutolewa nje kama vibaka, huyo Sugu uliyemtolea mfano ni mhanga wa huo ujinga, hivyo usimlaumu Magufuli kwa hilo.
Pamoja na hilo lakini upinzani huohuo angalau ulituonyesha Sisi Wananchi mapungufu ya Serikali yaliyopata kuwepo na kwalo ama baadhi ya Mawaziri wahalifu walifutwa kazi kwa kulazimishwa ama Rais husika alivunja Baraza lote la Mawaziri.

Usiwabeze tafadhari walifanya mengi mema pamoja na kunyanyaswa.
 
Nani kaua upinzani.. hakuna wakuua upinza na wala hajazaliwa na hatazaliwa.....
Alichofanya yule dhalim ni kuwanyima platform ya kuzungumzia akiamini kuwa anajijenga ili kutawala kiimla bila kuhojiwa lakini kumbe amewanyima Watanzania nafasi ya kusemewa pindi watawala wanapokengeuka.
 
Back
Top Bottom