Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Hili ni Swali ambalo Watanzania tunapaswa kujiuliza , kwamba kwa miaka mingi ofisi ya CAG imejitahidi sana kuanisha mapungufu , Wizi , upotevu na Uchafu wote unaofanywa kwenye mashirika na idara za serikali , wako walioonyeshewa vidole moja kwa moja ( Wengi wao majina yao yanafahamika )
Lakini kwa miaka yote hiyo hakuna hatua zozote za kisheria zimechukuliwa dhidi ya Watuhumiwa hao wanaofahamika ( niko tayari kusahihishwa ) .
Sisi Wananchi tumeanza kuitilia mashaka Serikali yetu kwamba ripoti ya CAG yaweza kuwa mbinu ya kizamani ya serikali ya ccm ya Kupumbaza wananchi ili waone kwamba serikali yao iko makini , CAG yuko Makini , Takukuru iko Makini , Rais anafokea wezi na mchwa wa Taifa , au Rais Kanuna nk . wakati kwenye ukweli Serikali haina umakini wowote ule , na ndio maana wezi wa Taifa wako kila mwaka na wengi wao baada ya kuharibu mahali pale wanahamishiwa pengine , ama wanapandishwa vyeo .
Sasa kwa kufupisha , Swali langu ni dogo tu , Ni akina nani waliotajwa kwenye ripoti ya CAG ambao waliwahi kushitakiwa Mahakamani au kuhukumiwa kwa Haki ?
Lakini kwa miaka yote hiyo hakuna hatua zozote za kisheria zimechukuliwa dhidi ya Watuhumiwa hao wanaofahamika ( niko tayari kusahihishwa ) .
Sisi Wananchi tumeanza kuitilia mashaka Serikali yetu kwamba ripoti ya CAG yaweza kuwa mbinu ya kizamani ya serikali ya ccm ya Kupumbaza wananchi ili waone kwamba serikali yao iko makini , CAG yuko Makini , Takukuru iko Makini , Rais anafokea wezi na mchwa wa Taifa , au Rais Kanuna nk . wakati kwenye ukweli Serikali haina umakini wowote ule , na ndio maana wezi wa Taifa wako kila mwaka na wengi wao baada ya kuharibu mahali pale wanahamishiwa pengine , ama wanapandishwa vyeo .
Sasa kwa kufupisha , Swali langu ni dogo tu , Ni akina nani waliotajwa kwenye ripoti ya CAG ambao waliwahi kushitakiwa Mahakamani au kuhukumiwa kwa Haki ?