Land Rover Discovery 3 Vs Subaru Forester XS

Land Rover Discovery 3 Vs Subaru Forester XS

Mimi binafsi sikushauri kwasababu naona wamiliki wengi wa magari hayo wanalalamikia namna ya uendeshaji, grage mafundi wenye uzoefu spare pia upatikanaji ni mgumu ... kumbuka kuwa Subaru ni Toyota kuihangaikia ni rahisi na mafundi kibao spare zinapatikana kwa urahisi pia šŸ¤
Mjomba (Subaru) Ni Mama (Toyota). Usihofu
 
Fanya haya
Chukua discover 3 uishi kwenye maisha haya

1. Kuwa makini na service sana pamoja na spea kuwa bei kumbuka discover 3 injini yake ilikuwa na shida Ndio wakaamua kutoa discover 4 hii ilifanyiwa marekebisho makubwa

2.kuhangaika kutafuta garage na ukipata unapewa bei mbaya kisa unaonekana una hela Kumbe Hamna

3.inabidi uishi mikoa hii mwanza ,arusha ,moro,pwani, na dar
Ikiwa hauishi hii mikoa hata oil tu itabidi upaki gari

4. Uwe na moyo wa nguruwe ikitokea tatizo uwe wa kupotezea sababu ukiwaza sana utapata pressure na ufe sana Ila ukiwa na moyo wa nguruwe Huna shida ikizingua unapaki tu

5.hutakiwi kuweka vitu vya ziada Kama mziki kufanya hivyo ni kutafuta gari lije liwake moto mapema sana Ila Kama ulaya au south afrika kuna specialist wazuri

Nunua subaru upate haya

1.service na Vifaa vinapatikana kwa wengi pamoja na wataalamu wapo

Hata ww ukinunua mtaani mpo wengi kupitia kuongea na Watu utatatua changamoto haraka

2.toka subaru watoe XT hakuna changamoto kubwa sana japo zenye turbo zina hitaji umakini kidogo

3.ukinunua XT ishi kokote kule na Mwenye pressure anamiliki halisumbui sana ni sawa na kuoa mpare hata maharage mtakula kila siku na halalamiki

NOTE: gari za waafrika ni toyota sababu toyota ni baba yetu aliishi tanzania Ila katika kutafuta life akahamia japan Ndio Maana ukinunua tofauti na hapo utahangaika sana sababu unakuwa umevunja miiko ya baba
Gari kuwaka moto mara nyingi ni pale watu kukosea kufunga ground waya [emoji51][emoji51][emoji51]wabongo hata Digital voltmeter hawatumii wanaotea tuu
 
Gari zingatieni model yake nikimaanisha Umri hiyo gari ya 2005 na 2023 tofauti ya miaka ni mingi sana shida gari za 2014 au 2015 kodi yake ni kuanzia 26m na unapata Discovery 4 ambayo utakua umepunguza usumbufu kwa kiasi kikubwa sana...tunanunua magari yakishakua machakavu harafu tunakuja kulalamika hizi gari mbovu huku dashboard ikisoma Mileage nyingi pia..
 
Gari kuwaka moto mara nyingi ni pale watu kukosea kufunga ground waya [emoji51][emoji51][emoji51]wabongo hata Digital voltmeter hawatumii wanaotea tuu
Ni mfumo unaosaidia kudhibiti mkondo wa umeme(electric current)ili kuilinda circuit hasa kwenye accidential situation.Sasa mafundi wetu utasikia hiyo haina tatizo mbona gari ya Mwakibibi ina miaka kibao inadunda tu[emoji1787]
 
Back
Top Bottom