Fanya haya
Chukua discover 3 uishi kwenye maisha haya
1. Kuwa makini na service sana pamoja na spea kuwa bei kumbuka discover 3 injini yake ilikuwa na shida Ndio wakaamua kutoa discover 4 hii ilifanyiwa marekebisho makubwa
2.kuhangaika kutafuta garage na ukipata unapewa bei mbaya kisa unaonekana una hela Kumbe Hamna
3.inabidi uishi mikoa hii mwanza ,arusha ,moro,pwani, na dar
Ikiwa hauishi hii mikoa hata oil tu itabidi upaki gari
4. Uwe na moyo wa nguruwe ikitokea tatizo uwe wa kupotezea sababu ukiwaza sana utapata pressure na ufe sana Ila ukiwa na moyo wa nguruwe Huna shida ikizingua unapaki tu
5.hutakiwi kuweka vitu vya ziada Kama mziki kufanya hivyo ni kutafuta gari lije liwake moto mapema sana Ila Kama ulaya au south afrika kuna specialist wazuri
Nunua subaru upate haya
1.service na Vifaa vinapatikana kwa wengi pamoja na wataalamu wapo
Hata ww ukinunua mtaani mpo wengi kupitia kuongea na Watu utatatua changamoto haraka
2.toka subaru watoe XT hakuna changamoto kubwa sana japo zenye turbo zina hitaji umakini kidogo
3.ukinunua XT ishi kokote kule na Mwenye pressure anamiliki halisumbui sana ni sawa na kuoa mpare hata maharage mtakula kila siku na halalamiki
NOTE: gari za waafrika ni toyota sababu toyota ni baba yetu aliishi tanzania Ila katika kutafuta life akahamia japan Ndio Maana ukinunua tofauti na hapo utahangaika sana sababu unakuwa umevunja miiko ya baba