LATRA mtoe adhabu inayomhusu mhusika, mabasi mliyoyafungia hayana makosa, igeni wafanyavyo trafiki

LATRA mtoe adhabu inayomhusu mhusika, mabasi mliyoyafungia hayana makosa, igeni wafanyavyo trafiki

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Trafiki hawawezi kulifungia gari kwa kosa la kutowasha taa usiku, watamuadhibu dereva. Mabasi mliyoyafungia hayana hitilafu yoyote tatizo ni madereva walizima ving'amuzi, hivyo madereva wangeadhibiwa.

LATRA hayo mabasi yapo barabarani kwa mikopo benki na wamiliki wanatakiwa wailipe hiyo mikopo na kuilipa hiyo mikopo basi linatakiwa liwe barabarani liingize fedha, sasa nyie mmeyafungia hao wamiliki watapata wapi pesa ya kurejesha mikopo!

Latra hayo mabasi ndiyo yanayowaweka ofisini hivyo hamtakiwi kuyaonesha ubabe, wenzenu trafiki hutoa adhabu kwa mhusika, kama gari ni bovu watalizuia kuwepo barabarani na kama gari ni zima watamuadhibu dereva kwa kosa alilolifanya na hawatalihusisha gari.

Nawashauri mbadili adhabu yenu iende kwa mhusika.
 
Ni vizuri washughulike na kinachosababisha watu wa magari wazime vingamuzi.

Bila hivyo zitakuwa tu kama mbio za sakafuni.
 
Ni vizuri washughulike na kinachosababisha watu wa magari wazime vingamuzi
Bila hivyo zitakuwa tu kama mbio za sakafuni.
Mimi kilichoniudhi ni nia ya Latra kutaka kuwafilisi wenye mabasi, wao wanadhani wenyemabasi ni matajiri bila kujua wengi wana madeni ya kutisha ila wanakomaa tu, hata hivyo wanaozima ni madereva.
 
Trafiki hawawezi kulifungia gari kwa kosa la kutowasha taa usiku, watamuadhibu dereva. Mabasi mliyoyafungia hayana hitilafu yoyote tatizo ni madereva walizima ving'amuzi, hivyo madereva wangeadhibiwa.

LATRA hayo mabasi yapo barabarani kwa mikopo benki na wamiliki wanatakiwa wailipe hiyo mikopo na kuilipa hiyo mikopo basi linatakiwa liwe barabarani liingize fedha, sasa nyie mmeyafungia hao wamiliki watapata wapi pesa ya kurejesha mikopo!

Latra hayo mabasi ndiyo yanayowaweka ofisini hivyo hamtakiwi kuyaonesha ubabe, wenzenu trafiki hutoa adhabu kwa mhusika, kama gari ni bovu watalizuia kuwepo barabarani na kama gari ni zima watamuadhibu dereva kwa kosa alilolifanya na hawatalihusisha gari.

Nawashauri mbadili adhabu yenu iende kwa mhusika.
Labda mimi sijaelewa vizuri kuhusu ving'amuzi. Kinapofungwa kwenye gari na mamlaka husika, kuna namna yeyote ya dereva au mmiliki wa basi kukizima kihalali?

Kwa ninavyofikiria hapa, ukiona basi lolote mfumo wa king'amuzi umechezewa basi mmiliki anajua na anahusika vizuri. Wewe dereva huwezi kukurupuka kumuita fundi aje achakachukue huo mfumo pale unapojisikia tu maana hiyo ni sawa na kucheza na moto.

Basi nyingi sana siku hizi zimechezewa huo mfumo. Dereva anaendesha mpaka ikianza kupiga kelele kuna fail switch ambayo akiminya tu inakata mawasiliano ya king'amuzi na live speed. Sasa hapo unakuta dereva anatembea hadi 100kph na hakuna kelele inatoka na hata huko latra wanaona chuma iko na mwendo legal. Ukitaka ujue kama hii ni kweli, siku ukisafiri safari ndefu kaa siti ya mbele kabisa ambayo itakuwezesha kumuona dereva vizuri akiwa anaendesha utaona tu maana haina siri.

Na basi nyingi sana wana hiyo michezo, na nina uhakika mamlaka husika wanajua au baadhi ya viongozi wa mamlaka husika wanajua hilo maana ni jambo ambalo halijajificha kabisa. Kwahiyo mimi naona ni sahihi basi kufungiwa na dereva kupigwa faini ya kuvunja sheria ya kuendesha basi la abiria kwa mwendo kasi
 
Labda mimi sijaelewa vizuri kuhusu ving'amuzi. Kinapofungwa kwenye gari na mamlaka husika, kuna namna yeyote ya dereva au mmiliki wa basi kukizima kihalali?

Kwa ninavyofikiria hapa, ukiona basi lolote mfumo wa king'amuzi umechezewa basi mmiliki anajua na anahusika vizuri. Wewe dereva huwezi kukurupuka kumuita fundi aje achakachukue huo mfumo pale unapojisikia tu maana hiyo ni sawa na kucheza na moto.

Basi nyingi sana siku hizi zimechezewa huo mfumo. Dereva anaendesha mpaka ikianza kupiga kelele kuna fail switch ambayo akiminya tu inakata mawasiliano ya king'amuzi na live speed. Sasa hapo unakuta dereva anatembea hadi 100kph na hakuna kelele inatoka na hata huko latra wanaona chuma iko na mwendo legal. Ukitaka ujue kama hii ni kweli, siku ukisafiri safari ndefu kaa siti ya mbele kabisa ambayo itakuwezesha kumuona dereva vizuri akiwa anaendesha utaona tu maana haina siri.

Na basi nyingi sana wana hiyo michezo, na nina uhakika mamlaka husika wanajua au baadhi ya viongozi wa mamlaka husika wanajua hilo maana ni jambo ambalo halijajificha kabisa. Kwahiyo mimi naona ni sahihi basi kufungiwa na dereva kupigwa faini ya kuvunja sheria ya kuendesha basi la abiria kwa mwendo kasi
Umechanganya king'amuzi na kidhibitimwendo, kinachopiga kelele ni kidhibiti mwendo, kingamuzi kinafanyakazi kupitia satalaiti ya angani, hivyo basi huonekana kuanzia linapoondoka mpaka linapofika, haya likipinduka linaonekana na kuwezesja msaada kupatikana mapema, sasa dereva anachoweza kufanya ni kuchomoa waya wa betri anapotaka na kuuchomeka tena hivyo kulifanya basi kuonekana na kupotea! Kila basi linaking'amuzi chake hivyo mwenyebasi hawezi kuwemo ndani ya mabasi yake yote kwa wakati mmoja.
 
Tanzania wahuni wamepewa majukumu makubwa wanaamua wafanye nini wakati wowote bila kuangalia madhara yake kwa jamii hii ishu aina tofauti na wale walioenda kupora hela kwenye maduka ya kubadilisha fedha wakisema ni wahujumu Uchumi...Nchi ngumu sana hii...
 
Kama ni tofauti na za, kama ni mfano na za ni halisi.
LATRA imeundwa kwa Sheria yake na hata Majukumu yake ni tofauti na Yale ya Trafiki. Jifunzeni kusoma Sheria zilizoanzisha mamlaka na taasisi mzielewe kabla ya kulalamikia utaratibu halali wa kisheria.
 
LATRA imeundwa kwa Sheria yake na hata Majukumu yake ni tofauti na Yale ya Trafiki. Jifunzeni kusoma Sheria zilizoanzisha mamlaka na taasisi mzielewe kabla ya kulalamikia utaratibu halali wa kisheria.
Naona mgumu wa kuelewa lugha ya kiswahili, ukiambiwa jifanye unakula hauchukui chakula na kukila, ukila haitakuwa kama.
Usiamini wewe peke yako ndiye unayezijua sheria, ujue wapo wengine wengi wanazijua pia, ligi za Yanga na Simba zinawapotosha sana.
 
Taja kosa lililofanywa na basi na kusababisha liadhibiwe wakati halina ubovu wowote, dereva amefanya kosa la kuzima king'amuzi bila kujua kuwa halitaonekana barabarani, mdomo umetukana kichwa kimepigwa makofi!
hao wanazima VTS alaf wanakanyagia 100kph, hao mabosi wenye basi wanajua fika michezo inayofanyika, Sauli yule pale, wakati anazindua zile basi za Mbeya, anamsifia dereva kwa kukimbiza chuma barabaranai, bure kabisa

LATRA wakamatie hapohapo,
 
Back
Top Bottom