LATRA mtoe adhabu inayomhusu mhusika, mabasi mliyoyafungia hayana makosa, igeni wafanyavyo trafiki

LATRA mtoe adhabu inayomhusu mhusika, mabasi mliyoyafungia hayana makosa, igeni wafanyavyo trafiki

Trafiki hawawezi kulifungia gari kwa kosa la kutowasha taa usiku, watamuadhibu dereva. Mabasi mliyoyafungia hayana hitilafu yoyote tatizo ni madereva walizima ving'amuzi, hivyo madereva wangeadhibiwa.

LATRA hayo mabasi yapo barabarani kwa mikopo benki na wamiliki wanatakiwa wailipe hiyo mikopo na kuilipa hiyo mikopo basi linatakiwa liwe barabarani liingize fedha, sasa nyie mmeyafungia hao wamiliki watapata wapi pesa ya kurejesha mikopo!

Latra hayo mabasi ndiyo yanayowaweka ofisini hivyo hamtakiwi kuyaonesha ubabe, wenzenu trafiki hutoa adhabu kwa mhusika, kama gari ni bovu watalizuia kuwepo barabarani na kama gari ni zima watamuadhibu dereva kwa kosa alilolifanya na hawatalihusisha gari.

Nawashauri mbadili adhabu yenu iende kwa mhusika.
we unawashwa na nini wakati matajiri wamekaa kimya halafu hivyo ndivyo sheria inavyosema au we unataka ujitungie sheria yako. Tii sheria bila shuruti acha blablah za mikopo.
 
Kosa limefanywa na dereva kwanini gari liadhibiwe? Hii haikubaliki kwani ni adhabu ya kijinga.
Rudi darasani ujue dhana ya adhabu. Rais wa nchi amekosea nchi inawekewa vikwazo, nchi imekosea nini? Nendeni shule mnatusumbua sana na viujinga vyenu huku mitandaoni
 
Mimi kilichoniudhi ni nia ya Latra kutaka kuwafilisi wenye mabasi, wao wanadhani wenyemabasi ni matajiri bila kujua wengi wana madeni ya kutisha ila wanakomaa tu, hata hivyo wanaozima ni madereva.
we umejuaje vyanzo vya matajiri? hiyo adhabu ni ndogo watii sheria
 
Rudi darasani ujue dhana ya adhabu. Rais wa nchi amekosea nchi inawekewa vikwazo, nchi imekosea nini? Nendeni shule mnatusumbua sana na viujinga vyenu huku mitandaoni
Unajua kuwa madereva husika wanaendesha mabasi mengine, sasa nani ameadhibiwa!
 
Ni vizuri washughulike na kinachosababisha watu wa magari wazime vingamuzi.

Bila hivyo zitakuwa tu kama mbio za sakafuni.
Wewe naye ina maana hujui kwanza kazi ya hizo VTS?!!kwani usingekuja na kauli hii!!
 
Taja kosa lililofanywa na basi na kusababisha liadhibiwe wakati halina ubovu wowote, dereva amefanya kosa la kuzima king'amuzi bila kujua kuwa halitaonekana barabarani, mdomo umetukana kichwa kimepigwa makofi!
Mambo mengine msiwe mnatetea ujinga!!eti dreva anafanya hivyo bila kujua kuwa hataonekana awapo barabarani??unafikiria hicho kifaa ni kama waya wa spika tu kuwa kila mtu anajua nikichomoa tu huu waya spika haita toa sauti?!!kuna utaalam wa kufanya hiyo kitu na ni lazima mwenye gari/msimamizi ahusike hapo!!kwa upendo gani dreva alionao kwa tajiri hadi aingie gharama hizo tena sio ndogo ili kumnufaisha tajiri??tena kwa taarifa yako huo mchezo hadi huko LATRA,kuna watu wa kuadhibiwa wanaosimamia mfumo huo!!
 
Naona mgumu wa kuelewa lugha ya kiswahili, ukiambiwa jifanye unakula hauchukui chakula na kukila, ukila haitakuwa kama.
Usiamini wewe peke yako ndiye unayezijua sheria, ujue wapo wengine wengi wanazijua pia, ligi za Yanga na Simba zinawapotosha sana.
Ligi za upinzani wa hoja nazipenda sana Tena sana kwa kuwa mpaka nashiriki nakuwa nimejipanga vya kutosha.

Sasa subiri nikuambie, wewe ni kuadi na umetumwa kufanya ukuadi na ni mtupu wa taratibu na Sheria za usafirishaji za LATRA.

LATRA hawawezi kufanya Kama Trafiki abadani kwa kuwa LATRA ni mamlaka ya udhibiti usafiri ardhini na vyombo vinavyodhibitiwa na LATRA ni vyombo vilivyosajiliwa kama vya biashara.

Kwa Sheria za LATRA ,kuna makosa ya dereva na makosa ya mmiliki. Anayetakiwa kulipia na kuutunza mfumo wa VTS ni mmiliki ,dereva yeye kapewa gari tu.

Wanaopewa semina na mafunzo ya kuutunza mfumo wa VTS ni wamiliki ,hapo unaona ni sawa kwamba mfumo mzima anaujua mmiliki na ni jukumu la mmiliki kuhakikisha mfumo upo sawa kila siku, eti dereva ndio awajibike kwa makosa ya mfumo?
 
Ligi za upinzani wa hoja nazipenda sana Tena sana kwa kuwa mpaka nashiriki nakuwa nimejipanga vya kutosha.

Sasa subiri nikuambie, wewe ni kuadi na umetumwa kufanya ukuadi na ni mtupu wa taratibu na Sheria za usafirishaji za LATRA.

LATRA hawawezi kufanya Kama Trafiki abadani kwa kuwa LATRA ni mamlaka ya udhibiti usafiri ardhini na vyombo vinavyodhibitiwa na LATRA ni vyombo vilivyosajiliwa kama vya biashara.

Kwa Sheria za LATRA ,kuna makosa ya dereva na makosa ya mmiliki. Anayetakiwa kulipia na kuutunza mfumo wa VTS ni mmiliki ,dereva yeye kapewa gari tu.

Wanaopewa semina na mafunzo ya kuutunza mfumo wa VTS ni wamiliki ,hapo unaona ni sawa kwamba mfumo mzima anaujua mmiliki na ni jukumu la mmiliki kuhakikisha mfumo upo sawa kila siku, eti dereva ndio awajibike kwa makosa ya mfumo?
"kuna makosa ya dereva na makosa ya mmiliki", kwahiyo hakuna makosa ya gari! Gari ndiyo iliyoadhibiwa na dereva na mmiliki hawakuadhibiwa, kuwa mamlaka hakuifanyi isiwe na adhabu ya mmiliki, dereva na gari hata hivyo mbona adhabu hizo Latra wanazo kwani wamewahi kuwafungia madereva, mabasi na wamiliki kutokana na aina ya kosa, hapa kosa kalifanya dereva aliyezima vts, makosa haya matatu na trafiki wanayo na kila kosa lina adhabu yake, dereva akizidisha mwendo anaadhibiwa yeye, gari kama linahitilafu huzuiwa lisibebe abiria na mmiliki naye anayo sehemu ya adhabu yake. Trafiki hawezi kuifungia gari isitembee barabarani mwezi mmoja eti kwa sababu dereva alilewa! Hicho ni kiroja.
Baada ya ufafanuzi huu sasa nakukaribisha unitukane mpaka ninyoroke, karibu.
 
Hii nchi Kuna uonevu sana!! Sasa mwenye bus (mmiliki) mwenye Magari 10 atawezaje kuwepo kwenye kila bus!? Dereva ana leseni iliyoidhinishwa na Serekali Hivyo anajukumu la kuheshimu taratibu
 
Back
Top Bottom