Mkuu Bibilia inasema "ajionavyo mtu nafsini mwake, ndivyo alivyo", km umemfatilia vzr amekubali kuwa alifeli mission zake na sababu kubwa ni akiri yake kubwa. Me nmemsoma toka mwanzo kuwa alitaka kufanya makubwa bila hata support ya mtu lkn akafeli. mf. ubaharia ambao ndo ilikuwa ndoto yake kubwa ikafail, Maisha ya marekani pia akaamua kusepa baada ya kuona hali ishakua tete. Sasa km anajiona yupo hvyo, wewe pia huna sababu ya kumpinga kwakua na wewe ni mwanadamu km yeye na unaona km anavyoona yeye. Sio wote wanaofeli shule kuwa hawana akiri na sio wote wanaofail maisha kuwa hawana akili, inategemea na sababu. Mfano mtu km dr shika watu wakaanza hadi kumdhihaki, kumsemea maneno ya dharau, waandishi wanamuuliza maswali ya kebehi. Sisi ni masikini hadi wa akiri zetu, hatuna subra, ni watu wakukurupuka. Sisemi km nakubaliana na Lemutuz ya kuwa anaakiri kubwa bali nilikuwa natoa angalizo tu kuwa hapa duniani lolote laweza kukutokea, kunawatu wamesoma hadi ulaya wamerudi wamepagawa na hakuna cha maana walichokifanya na accademic wapo vzr na unajiuliza wamepatwa na nini?