Le Mutuz: Historia ya kweli juu ya maisha yangu (My American experience)

Le Mutuz: Historia ya kweli juu ya maisha yangu (My American experience)

Mara yangu ya kwanza kucoment JamiiForums, hii story ikiwezekana tengeneza na movie kabisa, my appetite ya kusoma vitabu iliisha nilivyomaliza college but I got to admit kokokubanga umenistroke kipande cha ubongo cha kusoma, I will def Buy your book, ila ningekushauri tu angalia maneno unayoyaandika watoto Wako watakuja kusoma siku moja, hayo ya your ex kuolewa na mwislamu or kuwa mke wa pili sio jambo la kushangilia coz inaonyesha u are just as bitter, and I am pretty much sure she has a story to tell, usually kuna 3 dimensions ya ukweli, your side , her side and the truth. Whatever u decide to write kumbuka tu isiumize watoto wako muweke hizo ego pembeni, mafanikio yako yote means nothing Kama hautaweza kurekebisha uhusiano wako na watoto and that means kutumia akili kubwa boss and ego pembeni
 
Haahaha wewe kiazi kweli kweli sijakwambia upambane na Le kokobanga pambana na hali yako ; le mutuz keshapambana tayari na sasa anakula matunda ya juhudi zake, wewe unaepoyoka huku nyuma ya keyboard ndio upambane kivyako.
mimi tayari nakula Matunda ya Uhuru kazi yangu nikumshangaa Le Kokobangaz kulialia mapenzi Kama ndio ana balehe

Mwakani panapo majaliwa nastaafu kwa hiari miaka 55 , pension almost 350,000,0000, Na kila mwezi 2,000,000 za kunywea bia.
Hahahahahah\
 
Kiukwel story yakaka mkubwa imenifundisha kitu kikubwa sana ambacho huwa kinanikosesha amani nikumake furaha yangu naamani yakile ninachokiamini bila kujali macho yawatu wala maneno yao, namaisha niuzima mengine yapo2 endapo kama ukiwa naafya njema so haina haja yakuumiza kichwa sana mpaka ukakosa amani kwavitu ambavyo vipo2 ambavyo ukifanya juhudi utavipata2 sio kama pumzi
 
Hahaha Do not Hunt what You Can't Eat Safi Sana Mzee Mwenzangu Le Mutuz Ijapokuwa Tuna Utofauti wa Kiitikadi Lakini Niseme Tu Hii Story Yako ImekoNga Sana Nyoyo na Vijana Wana Mengi ya Kujifunza Big Up Sana Le MUTUZ BOMAYEEE Le MUTUZ NYE NYE NYE NYE Le Mutuz CITWAYEN [emoji106]
 
Le Mutuz ni uongo sana sana DMI pale alishindwa mitihani, kidato cha nne alifeli kwa kupata Division zero.

Nimesoma porojo zake IG simply ni mtu anayerubuni watu kwa kutafuta huruma na excuse ya kushindwa kwake Maisha

- Ukifeli kidato cha nne hakuna College USA inaweza kukubali unless urudie High School, usichokijua ni kwamba ili usome College USA unahitaji kupeleka makaratasi yako World Education Centre for Evaluation na wao wanawatumia maofisa wao wa Ubalozi hapa ambao wanajua our Education system so wanawarudishia info kule kua ulifeli Kidato cha Nne huwezi kuingia College kama nilivyofanya,

- Baada ya Kumaliza High School nilienda JKT Oljoro, niliporudi nilikaa miezi kama 7 kabla sijaondoka kwenye Belgium Mzungu kwa Jina la Captain Frawn akamuomba baba yangu anipe kozi ndogo ya Ubaharia pale DMI nilisoma miezi 6 ulipofika wa Saba nikaondoka nikiwa nusu ya kozi ya Fitter Mechanic lakini hivi ni vitu ambavyo vitakuwemo kwenye kitabu, kuna mengi sana sijayaandika lakini yatakuwemo kwenye kitabu, kwa mfano nikiwa DMI nilishawahi kufanya research kwa wiki Mbili Mv. Bukoba, Mv. Liemba na Mv. Mwongozo Kigoma na Mwanza.

- Ungesema nimemuongopea kua hakuwahi kuwa Deported back to bongo, au kwa sasa amebadili dini na kuolewa mke wa pili, ningekuelewa jaribu kubishania mambo ya msingi katika story yangu sio huu utoto utoto!

Thanks.

le Mutuz
 
Mkuu W. J. Malecela nimefurahishwa sana na hii "story" yako, lakini kuna kitu nataka kukushauri hata kama huwa unasema hupendi kushauriwa.

Iko hivi; kwanza achana kabisa na ngono zembe. Kwenye story yako nimeona umegusia mara kadhaa kuwa unamjua sana MUNGU, hivyo kama unalijua NENO la MUNGU kama unavyosema, basi ni lazima ujue kuwa MUNGU, hapendi vitendo vya "uzinzi na uasherati", vitendo ambavyo wewe umekuwa ukivifanya mara kwa mara. Tubu, mwombe MUNGU msamaha, na uanze maisha mapya, na uoe kama ulivyosema kuwa sasa unataka kuoa. Ukioa na kutulia, itakujengea heshima kubwa sana, hasa mbele ya watoto wako.

Pili, watoto wako wameanza kukua sasa, nafikiri mmoja ana miaka 19 kama sijakosea. Kama ni hivyo, huu ni wakati wa wewe kuanza kuwasiliana na watoto wako na kuwa nao karibu hata kama ni kwa njia ya mtandao. Watoto watakuelewa sana kama utaonesha initiative ya kuwa karibu nao kipindi hichi ambacho wanaweza kuchambua wenyewe ipi ni pumba na upi ni mchele. Despite what has happened in the past, but your kids still needs you in one way or another.

Tatu, imefika wakati uachane kabisa na majibizano ya kwenye mitandao na hao unaowaita "mashwetani" wanaotaka kukuangamiza. Ikiwa hutaweza kuacha kujibizana nao, tafadhali sana jaribu kuwa makini sana na vitu unavyo-post hasa picha za "mambebezzz" wako kwani tambua kwamba watoto wako na marafiki zao wanaweza wakawa wanasoma posts zako za mitandaoni, na hiyo itawaadhiri sana watoto wako. Nina uhakika baadhi ya posts ulizoziandika kwenye mitandao zitawaadhiri sana kisaikolijia watoto wako, hasa kama utaendelea kufanya hivyo. Naelewa kwamba "mitandao" ndiyo inakuweka hapa mjini, lakini unaweza kuiendesha kwa akili KUBWA bila kuwaadhiri watoto ambao wanauwezo wa kukufuatilia na kusoma kila kitu.

Nne, usiishie tu kuandika kitabu, ikiwezekana baada ya kutoa kitabu, tafuta mdhamini na utengeneze "movie" itakayohusu historia yako ya kweli ya maisha kuanzia kuwa mtoto wa Waziri Mkuu, kuwa baharia, kwenda New York na kuishi kwa miaka 25 huku ukiwa dereva wa malori, jinsi ulivyokutana na your ex, jinsi mlivyoachana, namna ulivyorudi Bongo na kuanza upya maisha ukiwa na dola 1000 tu, n.k. Naamini hiyo "movie" kama itachezwa vizuri inaweza ikawa ni movie bora kabisa ambayo imewahi kutengenezwa Tanzania kama siyo Africa.

By the way huu ni ushauri tu, na unaweza kuufanyia kazi ama kuupuza. Mimi siku zote huwa napenda sana kuwashauri watu waache maovu, na huwa sijali kama wanasikiliza ama wanadharau. So its up to you to decide bro, but remember this line; "For GOD shall bring every work into judgement, with every secret thing, whether it be good or whether it be evil".

1. Nitakapo oa nitaachana na wabebezz, Biblia inasema ni bora Mwanamke aolewe lakini haikusema lazima aolewe akiwa bikira, unajua maana yake? Itafakari then utanielewa.

2. Watoto wangu ni watoto wangu sihitaji kufanya anything new zaidi ya niliyowafanyia sio wao tu hata na mama yao, so thanks but no thanks, nimekataa ku deal na watoto wangu kwa masharti no way and never!

3. Social Media ndio my Butter and Bread, now sijui kama unajua so far kwenye Social Media huwa ninashindana na Mange na Shilawadu tu, ambao wote 2 ni muhimu sana katika kuongeza my Social MEdia Value kama sio hao na Makosa ya Tundu Lissu recently kunishambulia my Online TV ingeshakufa, wamenisaidia sana kuipandisha juu. Its about business sio kubishana na kama unanifuatilia utagnduka huwa sijibu anyone isipokua hao 2 tu!

4. Kuhusu kuandika Vitabu na mengineyo thanks again niliyajua hayo siku nyingi sana na nilishayaamulia maamuzi magumu tayari so usiwe na wasi wasi I am right on the track.

- Again kama ninavyosema siku zote sijawahi kufanya anything on ushauri wa wengine na sijawahi kumshauri anyone in my life kwa sababu anayeyajua maisha yangu ni mimi mwenyewe tu sio wewe wala anyone else!

le Mutuz
 
hongera story yako ni nzuri, ila mwanamke wako aisee ni kichwa maji sana. hata hivyo, tumesikia upande wa kwanza, kwetu sisi wanasheria umetuaminisha kuwa mwanamke ni wa aina hiyo, tukisikia upande wa pili nao ulete story yake hapa, usijeshangaa mambo yanabadilika ghafla. kwetu sisi wanasheria, huwezi kuamua kesi kwa kusikiliza upande mmoja, kila mtu ana story yake, lakini kwa harakaharaka, kwa kadiri nilivyoanza kukufuatilia nimeamini wewe huwa unaongea kilichopo moyoni na kuna uwezekano mkubwa ukawa mkweli.....umeshaestablish primafacie case inayohitaji x wako au watu wengine wanaokujua upande mwingine wajitetee ili jamii itoe hukumu kwa either kujifunza au kuwakosoa. but generally, kuna jambo kubwa sala la kujifunza kwenye maisha yako, na kwa mwili wako huo angekuwa mtu mwingine angeshakufa kwa pressure zamani sana, au angeshapata stroke...utakuwa uliumia moyo sana.

- Unanifurahisha sana jinsi unavyobadilika badilika kama Kinyonga, kwanza ulijifanya mtu mwema sana baadaye ukaanza kunitukana sasa naona umebadilika tena, hivi kweli wewe hujui kua my ex ameandika hapa kwa miaka yote matusi ya kila namna?

- Well, again mimi hua sina haraka kazi yangu ni Social Media so ukinichokoza humu mimi kazi yangu ni moja tu kutafuta angle ya kutumia ujinga wako kwa faida yangu, my ex katukana kwa miaka mingi sana niamini hajapata hata senti moja kwa kunitukana humu Social MEdia ila mimi ninaingiza pesa kwa kila ninaloandika ndio tofauti yetu,

- Sasa hivi ninaandika kitabu, na nitafanya mengi sana maana ninazo habari nyingi sana na sio kitabu kimoja tu, ninaweza nikaandika kitabu seriously on her tu na kikauza kuliko anything so relax boss hapa kwangu everything is under control, siri yangu ya maisha ni sijawahi kufanya maamuzi nikiwa na hasira huwa ninasubiri nikiwa nimetulia kwanza.

le Mutuz
 
Nlichopenda katika harakat zake zote,kuwin na kufail hajamlaumu mtu yoyote,tofaut na watu wengine akifeli anaanza kulaumu watu kwamba bila fulan kufanya hivi nisingefeli,Lemutuz pamoja na ugumu aliopata kwa ndugu zake from step mother bado amekua ngangari na hajawalaumu ndugu zake wala wazazi wake,anakaambia najilaumu mwenyew kwa ujinga wangu,either kwa kujua ama kutokujua[emoji2]
Kuna ka akili flani hivi amenipandikiza since nimeanza kusoma hii story yake,japo kwa haraka haraka huwez mwelewa

- Akili timamua zilianza kunijia nikiwa Jandoni Porini Dodoma, since then nilishaamua kua maisha yangu ni yangu na matatizo yangu ni yangu hayamuhusu mtu mwingine, mpaka leo ninaishi hivyo!

le Mutuz
 
Huyo Peter Lwangisa nimesoma naye boarding enzi za primary. He used to be the most fearsome bully in school. I remember him as a vicious, violent, brutal individual who would beat you up for no reason. His was a reign of terror until the day he left the school. Kama mnaelewana naye huyo basi you guys must be cut from the same cloth.
Atakuwa ni peter mwingine kabisa not from this planet.
 
Back
Top Bottom