Inasemekana siti aliolewa baada ya kwanza kutopenda kuonekana hadharani ndio maana
tena kuna stori nyingi zaidi wakati anaoa na hali ilivyokua ambazo wacha niziite za vijiweni
swali la kizushiSio kweli
Sitti na Khadijah wote aliwaoa zamani sana
wakati anajiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani...alikuwa na wake wawili
akawa ameyumba kiuchumi kiaina
Rafiki yake Kitwana Kondo akamsaidia sana....ndo chanzo cha Kitwana Kondo
kuja kuwa untouchable kiaina wakati wa Mwinyi
Roho mbaya tu za watu kwa Mwinyi.Mkuu kinacho nishangaza ni kuwa mfumo wa vyama vingi sifa nyingi anapewa Nyerere wakati aliyekuwepo madarakani ni Mwinyi sijajua kwa nini anasifiwa Nyerere
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]najaribu kuwaza ndo angekua faru john.......pasingekalika angeteketeza ukoo mzima[emoji188][emoji188]Halafu kuna njemba ilimkataga mabanzi mubashara hadharani yaani watu wana laana dunia hii.
Na upole ule wa Mzee mwinyi unatoa wapi ujasiri wa kumuadhibu na sucker slap...alinifurahisha alipomsamehe. That's was tottaly humane and humble.
swali la kizushi
kwanini ukimgusa Mwinyi na SAS lazima uje uwakingie vifua humu jamvini una uhusiano nao ??
Kuelewa mchango wa Mwinyi unapaswa kwanza kuelewa hali ya nchi ilivyokuwa wakati anakuwa Rais...
Nchi ilikuwa na Redio moja tu Redio Tanzania..na magazeti ya chama na serikali...
hakuna kabisa sehemu ya kukosoa wala kueleza matatizo...
na baada ya vita ya Iddi Amin kiuchumi nchi ndo ikayumba kabisa
Sera za Nyerere za ujamaa na kila kitu kufanywa na serikali kuanzia kuuza mikate
hadi nguo n kadhalika ilisha feli....
watu wanapanga foleni kununua sukari na sigara
mtu akienda Kenya mnamuagiza colgate na sabuni za lux...
hali ilikuwa mbaya except kwa wachache waliokuwa na nafasi...
Mwinyi akaapishwa mwaka 1985....by the time anaondoka 1995..
Ilikuwa nchi tofauti kabisa.......magazeti tele..TV na redio...tele
vyama vya upinzani.....hadi uchaguzi wa 1995 kulikuwa na mdahalo kwenye tv
hapo ndo Lipumba akaibukia CUF....
Vitongoji kama Sinza vikawa maarufu wakati wa Nyerere ni kulikuwa na mashamba tu ya mpunga..
magari ikawa ruksa unanunua bila kuomba kibali..
Sasa wapo wanaosema hakufanya lolote...
labda mabadiliko yangekuja tu bila yeye...
but wengi wanaosema hivyo hawakuwepo enzi hizo
Anzisha thread yako tumuhoji mwalimu au karume au mkapa au kikwete au magu..simple Sanambona wapo wengi ujahoji jombi !kama mwalimu, karume ,mkapa ,kikwete ,muheshimiwa magu ! au nao sio watu jombi ?
Sababu najua kuna unfairness ya uandishi wa historia
Nyerere anatukuzwa....Kawawa anapondwa..akati utawala ni huo huo
Hata sasa pay attention siku moja Magufuli ataitwa 'mtakatifu'
Historia ya nchi hii inajulikana kwa hitilafu zake....
Mkuu kinacho nishangaza ni kuwa mfumo wa vyama vingi sifa nyingi anapewa Nyerere wakati aliyekuwepo madarakani ni Mwinyi sijajua kwa nini anasifiwa Nyerere
Kwa hili sina uhakika, inaweza ikawa siasa. Huyu Mzee kwa kipimo changu cha kiuanadamu ni mcha Mungu haswaa.Alikuwa anasikiliza sana ushahuri wa mke wake kuliko baraza la mawaziri
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] [emoji115][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]najaribu kuwaza ndo angekua faru john.......pasingekalika angeteketeza ukoo mzima[emoji188][emoji188]
swali la kizushi
pia unaweza usilijibu
kwanini ukimgusa Mwinyi na SAS lazima uje uwakingie vifua humu jamvini una uhusiano nao ??
Alibadilisha maisha yangu kuwa mazuri hadi leo. Kwa kuruhusu ajira huria / ruksa nilipata kibali toka wizarani kufanya kazi DANIDA. Halikuwa jambo jepesi miaka hiyo. Huko niililipwa dolar 11,000 mkupuo na maisha yangu kipesa kuwa safi mpaka leo. Mungu aziidishie maisha azine kuona vitukuu, vilembwe nk.Wakuu habar ya majukumu.
Kwanza nitangulize precaution kwamba simtabirii kifo Rais wa awamu ya pili Alhaj Ally Hassan Mwinyi.
Nimekuja hapa kutaka kujuzwa kuhusu Mwinyi kabla hajafa ili tumpe hongera zake akiwa hai. Kumekuwa na kasumba katika nchi yetu ya kumwagia sifa nyingi kiongozi mara tu anapofariki, wakati akiwa amekufa sifa zake humwagwa hata zile ambazo wengine hatukuwahi kuzijua, sijui kwa nini hali hii inasubiri mpaka afe.
Leo nimefikiria kuhusu Mzee Mwinyi simaanishi kumtabiria kifo lakini kwa mwanadamu yeyote anaeamini uwepo wa Mungu anaamini kuna siku atakufa. kwa kulitambua hilo mimi kama kijana ambae wakati Mzee mwinyi anaongoza (1985-1995) nilikua sijapevuka kuweza kupambanua mambo na kwa bahatu mbaya sana watanzania hatuna tabia ya kuweka kumbukumbu zetu kwenye maandishi imeniwea vigumu sana kufahamu uimara na udhaifu wa mzee Mwinyi wakati wa utawala wake.
Hivyo nimekuja humu kuwaomba wajuzi wa mambo ambao wao pengine walikuwa na ufahamu wa kutosha kipindi cha Mwinyi watujuze strength na weakness za utawala wake ili apatiwe haki yake akiwa hai tusisubiri Mzee amefariki tuanze kujaza nyuzi humu kila mtu akijifanya kunfahamu Mzee. Nimejifunza hili kwenye msiba wa Mzee Sitta tukiambiwa mambo mengi ambayo hata hatukuwahi kuyafahamu.
tabia hii tuache watanzania, leo nimeona nianze na hili tuambieni kuhusu Mzee Mwinyi.
Nawasilisha