Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Unamsifia anayeezeka na kumponda aliyejenga msingi na kuta... Hizi ni akili ama matope?
 
Mzee Mwingi mawazo yake ni mapana sana na uelewa mzuri wa mambo na anakiri ukweli mchungu, wengine watampinga kwa sababu kasema ukweli. Mawazo ya Mzee Mwinyi yaheshimiwe kwa umri, uzoefu na busara zake anasema aliyoyaona na kuyashuhudia
 
Mwinyi sema kazeeka na uzee pia waweza kuwa na mapungufu. Lakini hakuna Raisi aliyefanya makubwa nchi hii Kama Raisi Mwinyi ila hana watu wa kumsifia.Nyerere alikomaa na ujamaa akaja na sokoine wake kukamata watu wote wenye pesa kuwa Ni wahujumu uchumi kwa Nini Wana pesa ?.Matajiri wakasema isiwe kesi wakaacha kununua mazao ya Tanzania kupeleka nje ya nchi kwa bussiness partner wao .matajiri wakaaanza kuficha pesa porini nk Nchi ikawa tupu haina pesa za kigeni na mabenki yakaanza kufilisika hakuna depositors sababu matajiri waliona ukiweka benki unafuatiliwa pesa zako kuwa ohhh pesa zote hizi umetoa wapi Matajiri wakazira wenye pesa zao kuweka benki.Nyerere akajikuta pesa za kigeni hana na mabenki hayana pesa za ndani kwa kufilisika kwa kukosa depositors akaona kuendesha nchi kumemshinda akaona asepe kijanja .Tukubali tukatae Nyerere alikuwa mzuri mambo mengine lakini kwenye uchumi alikuwa sifuri.Akasema nang'atuka neno ambalo hata kamusi ya kiswahili halikuwepo kumbe zigo la uchumi anataka kulibwaga kijanja baada ya kuona limemshinda .Akambwagia zigo Raisi Mwinyi.Raisi Mwinyi nchi ikiwa tupu haina hella za kigeni na mabenki yako hoi bin taabani.Aliposhika akasema sera yangu ruksa jaza duka jaza akaunti za benki utakavyo sikuulizi pesa umetoa wapi.Maduka yakajaa ghafla bidhaa ,pesa za kigeni zikajaa ghafla zimetoka wapi nobody knows and nobody cares.Miduka ya pesa za kigeni ikafurika pesa za kuuza na kununua walitoa wapi nobody knows.Mabenki yakapata depositors kibao tena wa pesa nyingi.Mwinyi kazi aliyofanya Ni kubwa mno kwenye Mambo ya uchumi niwe wazi hata Nyerere ilimshinda.Mwinyi alipokea nchi ikiwa Hali mbaya kuliko wakati ikipata Uhuru akaibadilisha
 
Huyu mzee anajitahidi kusema, lakini ajue tu kuwa alishiriki kuuwa shrika la ndege na mashirika mengingine. Hivyo ni aibu kwa. Ila kama ujuavyo boss haeleweki, anaweza badilika na kufanya jambo lolote wakati wowote. Hivyo ili kuwa salama inabidi ujikombe kwake ili anagalau ukumbukwe.
 
Mzee Mwingi mawazo yake ni mapana sana na uelewa mzuri wa mambo na anakiri ukweli mchungu, wengine watampinga kwa sababu kasema ukweli. Mawazo ya Mzee Mwinyi yaheshimiwe kwa umri, uzoefu na busara zake anasema aliyoyaona na kuyashuhudia
Je hii katuni inaukweli wowote kwenye hili?
 
Hamna cha uungwana wala ukweli.
Mzee ana endeleza unafiki tuu hapo.
Anajikomba kwe vile mwanae ana taka kuwania urais wa Zanzibar.. Akiwa kinyume na Mkulu mwanae hata pata nafasi.. Kula na kipofu usimshike mkono..
 
Mzee Ruksa kaonesha hekima na busara ya kiwango cha juu kuhusu suala la waraka lakini kubwa zaidi ni pale alipoelewa kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano na Rais JPM mwisho wa siku heshima itarudi kwao wote, pia chama na seikali kinacho iongoza.

Kawashinda baadhi ya wazee wastaafu ambao kimsingi wanatindikia au tuseme wana utapiahekma/busara. Wao wanafikiri kazi baada ya kustaafu ni kujenga fitina, kuendekeza chuki, kebehi dharau na kubwa zaidi kunanga wenzao kwa sababu yeyote ile. Kumbe kwa kufanya hivyo wanaziharibu heshima zao na thamani ya utu wao. Kwao wenyewe na kwa vizazi vyao.
 
Duh, Mzee Mwinyi kwa heshima na taadhima, alichosema siyo sahahi, yaani Urais wake plus wa Mkapa plus wa Kikwete unazidiwa na miaka 3 ya Magufuli?
Mzee Mwinyi angejisemea nafsi yake tu lakini kauli yake inaharibu legacy za wenzie
Ina maana madaraja yote makubwa, plus mabarabara, mavyuo vikuu, mavivuko, mashule ya kata, Umeme Kinyerezi 1, Bomba la gesi, uwanja wa ndege terminal III, mwendokasi aliyojenga Kikwete plus uchumi mzuri aliouacha Mkapa vyote hivyo Magufuli kavizidi ndani ya miaka 3?
 
Huyo mzee atuambie kuwa uchumi umekuwa kwa % ngapi?
 
OK, kuporomosha uchumi toka 7% to 4%, kuteka, kuua, hongeara JPM,
 
Mawazo yake. Alishafanya kazi hiyo ya Urais. Anajua alichokisema, kwamba yeye akufanya Cho chore hila kuleta ufisadi
 
Anafanya kwa kufuata misingi ya katiba na sheria au anafanya kama yeye. Wengine Pia kama wasinge heshima katiba,bunge na sheria zingine wangeweza kumzidi huyu wenu. Yeye anajifaninisha na nzagamba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…