Lema atua Tanga Mjini, ashangaa na kulia baada ya kukuta Watu bado wanaishi kwenye Magofu zama hizi!

Aache ushamba wa kichaga, baada ya kukaa Canada amekuwa km kichaa. Wenzake wamezaliwa Marekani hawashangai hayo anayoyashangaa. Maskini akipata kidogo matako hulia...
 
Acha upoyoyo na wewe uchagani kuna umaskini tena wa kutisha ndio maana hawatulii kwao wanaishi km wakimbizi ndani ya nchi. Wadanganye wasiofahamu huko machame. Mnapenda visifa vya hovyo tena kwa kudanganya. Aache ushamba wenzake wamekaa Ulaya zaidi yake
 
Haaaaaaaaaaaaaaa
Kwa hili namshukuru sana Lema; ni kweli ukiendaga Ulaya halafu ukirudi huku kwetu wewe mwenyewe unaona haibu kwa hali iliyopo, kwe Lema yupo sahihi ingawa sisi wengine tungeona aibu kusema.

Kweli Ulaya na Sehemu nyingi Africa ni sawa na Mbingu na Jehanum; huwezi kufikiri kivipi mtu anaenda ulaya na anarudi hapa na ana adapt; yaani difficult
 
Moshi pana nafuu sn
 
Lema ingekuwa amezaliwa huko alikotoka halafu iwe ndo mara yake ya kwanza kufika Tanzania angetuua kwa presha kwa haya Mambo aliyoyakuta, yaani Lema wakutuona sisi tunaishi kama wadudu kweli.........!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwa ujumla nchi hii ina umaskini mkubwa sana. Kuna maeneo ukienda, unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.

Waafrika wengi wanaishi katika umaskini mkubwa wakiwa wameridhika kwa sababu hawana exposure, hivyo wanafikiri watu wote Duniani wanaishi kwa namna hiyohiyo au inayokaribiana na hiyo.

Kuna wakati, nakumbuka tulikofi ndege kwaajili ya kufanya airborne survey, tulipotua kijiji kimoja, wale wazungu ambao ilikuwa mara yao ya kwanza kuja Afrika, walisema kuwa japo hawakuwepo wakati wa karne ya 18, lakini kwa kupitia maandiko ya kihistoria, ni dhahiri maisha ya barani kwao wakati wa karne ya 18 yalikuwa bora maradufu kuliko yale waliyokuwa wanayashudia kwenye vijiji vingi vya Tanzania.

Kuna baadi ya mikoa, vijijini ni balaa kubwa. Mpaka leo watu wanaishi kwenye tembe, nyumba za tope au mabanda ya miti na nyasi. Niliwahi kwenda hifadhi ya Kigosi, huko Ushirombo, nilichokiona kwenye vijiji vya njiani ilikuwa ngumu kuamini. Watu wanaishi kwenye mashimo. Banda linakuwa halina ukuta, paa linasimama juu ya ardhi. Katikati ya hilo paa la nyasi na miti wanachimba shimo. Hilo shimo ndiyo nyumba..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…