Lengai Ole Sabaya na Wenzake wawili wahukumiwa miaka 30 Jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha

Lengai Ole Sabaya na Wenzake wawili wahukumiwa miaka 30 Jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha

Tutarajie miujiza na mazingaombwe kufanyika,sio ajabo kwa Tz
Sio tu Tanzania wa kwetu, hizo court of appeals zipo duniania kote, ndio haki yenyewe, huweza chelewesha hapa ikapatikana pale. Kikubwa tujifunze Patience.
 
Katiba yako inakataza mwanajeshi aliekufuzwa asijitafutie kazi /kapato?

Inakataza mtu binafsi asiwaajiri??

Hebu jitahid usifanane na user name yako basi , utafanya upuuzwe wakat una akili timamu tu
Mpaka anajiita hivyo ni kuwa anajijua Kabisa ni Mjinga
 
Kosa alilohukumiwa nalo halina adhabu ya kunyongwa.

CCM mmezoea kupindisha sheria kuwafurahisha nyinyi binafsi na wake zenu.

Unataka anyongwe kwa kosa ambalo halina adhabu ya kunyongwa ?
Mtanyooka tu vijana ccm mliokuwa nyuma ya huyo mccm mwenzenu ,jambazi .

ambo moja kumbukeni “MALIPO NI HAPA HAPA DUNIANI”. Umekumbuka na sabaya wako mlivyotumia polisi kuvuruga shamba la mbowe kwa kung'oa mazao shambani Kwame?“.

Imetimia mkiwamaliza wapinzani,mtaanza kutafunana nyie kwa nyie
 
Wanajukwaa poleni kwa kumbukumbu ya kifo cha muasisi wa Taifa letu,Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Bila shaka baada ya Hukumu ya Lengai Ole Sabaya kuhairishwa tarehe 1/10/2021 ilipangwa kwamba itatolewa leo. Hivyo tuelekeze masikio yetu katika viunga vya mahakama.

=======

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili leo Ijumaa Oktoba 15, 2021 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kusikiliza hukumu ya kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha.

Hakimu mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Amalia Mushi aliahirisha hukumu hiyo Oktoba Mosi, 2021 baada ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Odira Amworo, kutokamilisha kuandika hukumu hiyo.

Agosti 24 mwaka huu, Sabaya na wenzake Sylvester Nyegu na Daniel Mbura walikamilisha kujitetea mahakamani hapo baada ya Jamhuri kukamilisha mashahidi 11 na vielelezo vinane.

Sabaya alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Juni 4, mwaka huu baada ya kukamatwa Mei 27 wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Chanzo: Mwananchi

UPDATE: MAHAKAMA YAMKUTA NA HATIA OLE SABAYA


Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imemkuta na hatia Lengai Ole Sabaya na wenzake katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha.

Mahakama ilimpatia nafasi Ole Sabaya ajitetee(Shufaa) kwanini asipewe adhabu kali naye aliiomba Mahakama imuonee huruma kwani si yeye bali alikuwa anatekeleza amri ya mamlaka ya uteuzi, pia ameomba mahakama imuonee huruma kwani ana mchumba anayetegemea kufunga naye ndoa na mahari ameshalipa.

UPDATE: SABAYA NA WENZAKE MIAKA 30 JELA

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wamehukumia na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.

WASIFU WA OLE SABAYA

Lengai Ole Sabaya amezaliwa 26/12/1986 mkoani Arusha. Amesoma Shahada ya Sayansi katika Elimu Chuo Kikuu cha Mtakatifu John Dodoma (St. John University).

Ole Sabaya aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) Mkoa wa Arusha na pia aliwahi kushika wadhifa wa Udiwani katika kata ya Sambasha Wilaya ya Arusha Mjini mwaka 2015.

Ole Sabaya aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro tarehe 28 Julai 2018 ya aliyekuwa Rais wa Tanzania awamu ya tano, Hayati John Pombe Magufuli.

Sabaya alitenguliwa nafasi hiyo ya ukuu wa Wilaya ya Hai tarehe 13 Mei 2021 na Rais Samia Suluhu Hassan ili kupisha uchunguzi wa makosa yaliyokuwa yakimkabili ikiwemo unyang’anyi wa kutumia silaha. Tarehe 15 Oktoba 2021 Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Arusha imemhukumu Sabaya na wenzake kifungo cha miaka 30 jela.

Zaidi soma...

HAKIMU Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Arusha, Odira Amworo amesema mshtakiwa Lengai Ole Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai amekutwa na hatia katika kesi iliyokuwa ikimkabili pamoja na wenzake. Hakimu amesema hayo Oktoba 15, 2021 wakati akiendelea kuchambua hoja wakati akisoma hukumu ya Sabaya na washitakiwa wenzake watatu.

Sabaya baada ya kukutwa na hatia anaiomba mahakama imuonee huruma kwani sio yeye bali alikuwa anatekeleza maagizo ya Mamlaka yake ya Uteuzi, pamoja na hayo mshtakiwa huyo anabainisha ana mchumba walikuwa wafunge ndoa na mahari ameshatoa.

Awali Hakimu Amworo amesema hakuna shaka washitakiwa watatu walifika dukani kwa Mohamed Saad siku ya tukio. Ameongeza kuwa amethibitisha mshitakiwa wa kwanza Lengai Ole Sabaya na mshitakiwa wa pili Sylivester Nyegu walikuwa wanafahamiana.

Ameeleza kuwa imethibitika mshitakiwa wa kwanza alikuwa na bastola ndani na nje kulikuwa na watu wawili wenye silaha hivyo, hakuna shaka duka la shahidi wa kwanza lilivamiwa na watu wenye silaha na lilikuwa chini ya watu wenye silaha.

Hata hivyo, amesema hakuna silaha iliyotumika katika tukio hilo, hivyo hakuna shambulizi la kutumia silaha. Hakimu amesema kati ya mashahidi 11 waliotoa ushahidi wao dhidi ya Sabaya, ni mashaidi wawili tu ndio ambao ushahidi wao haukuwa na mashiko.

Sabaya amekutwa na hatia kabla ya kupewa nafasi na watuhumiwa wenzake wajitetee ili Wapungiziwe adhabu.
Siasa za Bongo bhana usipokuwa makin mwisho wako lazima uwe mbaya.
Chamsingi ni kuongoza watu kwa mujibu wa kabuni taratibu na sheria na siyo kuongoza kimabavu.

nimeiona picha hij fb
Screenshot_20211016-140853.jpg
 
mbona picha ya dem wake tiyar ishatupiwa humu, angalia kwenye thread ya 30 hadi 35 zimetupiwa nyingi tu, demu lina shep nzr, sura nzr, na dimpoz afu dem amepanda ameenda hewani yaonesha ni mnyarwanda maana ana figa ya kinyarwanda.

Huyu demu tiyari wajuba washamweka kune mahesabu yao. Huyu halazi siku anachukuliwa. Hata jamaa yake alivojitetea vile, tiyari alishajua hana chake pale.
Kabisa mkuu. Chombo Safi kabisa. Usikute naye alimpora mtu maana lile jambazi hatari. Kama alimpora mtu sasa nafikiri ni glass za wine zinagongana tu.
 
Mnaposhangilia pia mjiandae hizi kesi zote zipo chini ya TISS Hawa mahakimu hukumu wanaandikiwa.

Ni sawa sababya kufungwa lakini majonzi yatakuwa makubwa Sana kwa Mbowe Kama wafuasi wa chadema hawataingia barabarani.

Inawezekana Mbowe hatutamuona Tena mpaka 2026 Tena kwa dharau ataachiwa kwa msamaha wa Rais.
Afungwe Kwa makosa yepi Mkuu kwani Sabaya kabambikiwa kesi au ni kweli kayatenda makosa yaliyomtia hatiani??

Mbowe kesi yake iko wazi na waliotengeneza wameshindwa kudhinitisha mpaka sasa. Na hata akifungwa Kwa uonevu tayari tumeshajiandaa kisaikolojia kwani ukweli tumeshaufahamu.
 
Best sabaya hajawahi kushitakiwa kwa mauaji! Hayo mashitaka ya kutunga hayana maana ipo siku atakuwa huru!
Mkuu, hiyo ya "mashtaka ya mauaji" umeitoa wapi? Andishi langu halisemi popote kuwa ameshtakiwa kwa kosa la mauaji.

Sasa kama unavyosema mashtaka aliyokutwa na hatia ni ya "kutunga", hilo unalijuwa wewe. Na vipi, kwa nini usingejitokeza mahakamani kupinga hayo "mashtaka ya kutungwa"? Unaacha hadi mtu wako anadhalilishwa hivi halafu ndio ujitokeze JF kutetea, itasaidia kitu gani sasa!

Nami naamini, kuna siku atakuwa huru baada ya kutumikia kifungo chake, na pengine wakati huo atakuwa amejirudi na kujutia maovu aliyokuwa akiwafanyia watu wengine.
 
SUKUMA GANG wamejipanga, rufaa kuingizwa mahakamani jumatatu saa moja na robo asubuhi!

Kesi kurindima, hapa na pale mahakama kuu ita confirm kifungo, watakata
Wanajukwaa poleni kwa kumbukumbu ya kifo cha muasisi wa Taifa letu,Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Bila shaka baada ya Hukumu ya Lengai Ole Sabaya kuhairishwa tarehe 1/10/2021 ilipangwa kwamba itatolewa leo. Hivyo tuelekeze masikio yetu katika viunga vya mahakama.

=======

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili leo Ijumaa Oktoba 15, 2021 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kusikiliza hukumu ya kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha.

Hakimu mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Amalia Mushi aliahirisha hukumu hiyo Oktoba Mosi, 2021 baada ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Odira Amworo, kutokamilisha kuandika hukumu hiyo.

Agosti 24 mwaka huu, Sabaya na wenzake Sylvester Nyegu na Daniel Mbura walikamilisha kujitetea mahakamani hapo baada ya Jamhuri kukamilisha mashahidi 11 na vielelezo vinane.

Sabaya alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Juni 4, mwaka huu baada ya kukamatwa Mei 27 wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Chanzo: Mwananchi

UPDATE: MAHAKAMA YAMKUTA NA HATIA OLE SABAYA


Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imemkuta na hatia Lengai Ole Sabaya na wenzake katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha.

Mahakama ilimpatia nafasi Ole Sabaya ajitetee(Shufaa) kwanini asipewe adhabu kali naye aliiomba Mahakama imuonee huruma kwani si yeye bali alikuwa anatekeleza amri ya mamlaka ya uteuzi, pia ameomba mahakama imuonee huruma kwani ana mchumba anayetegemea kufunga naye ndoa na mahari ameshalipa.

UPDATE: SABAYA NA WENZAKE MIAKA 30 JELA

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wamehukumia na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.

WASIFU WA OLE SABAYA

Lengai Ole Sabaya amezaliwa 26/12/1986 mkoani Arusha. Amesoma Shahada ya Sayansi katika Elimu Chuo Kikuu cha Mtakatifu John Dodoma (St. John University).

Ole Sabaya aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) Mkoa wa Arusha na pia aliwahi kushika wadhifa wa Udiwani katika kata ya Sambasha Wilaya ya Arusha Mjini mwaka 2015.

Ole Sabaya aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro tarehe 28 Julai 2018 ya aliyekuwa Rais wa Tanzania awamu ya tano, Hayati John Pombe Magufuli.

Sabaya alitenguliwa nafasi hiyo ya ukuu wa Wilaya ya Hai tarehe 13 Mei 2021 na Rais Samia Suluhu Hassan ili kupisha uchunguzi wa makosa yaliyokuwa yakimkabili ikiwemo unyang’anyi wa kutumia silaha. Tarehe 15 Oktoba 2021 Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Arusha imemhukumu Sabaya na wenzake kifungo cha miaka 30 jela.

Zaidi soma...

HAKIMU Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Arusha, Odira Amworo amesema mshtakiwa Lengai Ole Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai amekutwa na hatia katika kesi iliyokuwa ikimkabili pamoja na wenzake. Hakimu amesema hayo Oktoba 15, 2021 wakati akiendelea kuchambua hoja wakati akisoma hukumu ya Sabaya na washitakiwa wenzake watatu.

Sabaya baada ya kukutwa na hatia anaiomba mahakama imuonee huruma kwani sio yeye bali alikuwa anatekeleza maagizo ya Mamlaka yake ya Uteuzi, pamoja na hayo mshtakiwa huyo anabainisha ana mchumba walikuwa wafunge ndoa na mahari ameshatoa.

Awali Hakimu Amworo amesema hakuna shaka washitakiwa watatu walifika dukani kwa Mohamed Saad siku ya tukio. Ameongeza kuwa amethibitisha mshitakiwa wa kwanza Lengai Ole Sabaya na mshitakiwa wa pili Sylivester Nyegu walikuwa wanafahamiana.

Ameeleza kuwa imethibitika mshitakiwa wa kwanza alikuwa na bastola ndani na nje kulikuwa na watu wawili wenye silaha hivyo, hakuna shaka duka la shahidi wa kwanza lilivamiwa na watu wenye silaha na lilikuwa chini ya watu wenye silaha.

Hata hivyo, amesema hakuna silaha iliyotumika katika tukio hilo, hivyo hakuna shambulizi la kutumia silaha. Hakimu amesema kati ya mashahidi 11 waliotoa ushahidi wao dhidi ya Sabaya, ni mashaidi wawili tu ndio ambao ushahidi wao haukuwa na mashiko.

Sabaya amekutwa na hatia kabla ya kupewa nafasi na watuhumiwa wenzake wajitetee ili Wapungiziwe adhabu.
Kila kosa miaka 30
Jumla miaka 90
Baada ya Sabaya kujitetea Mahakama ikaaamua kufanya adhabu zote ziende pamoja , wakampiga 30mila kiuhalisia ilibidi ale 90.
 
Hii hukumu ya sabaya ni namna tunaandaliwa kisaikolojia kupokea hukumu ya mbowe.amka kijana,mbowe kaisha...
MATAGA mnawashwa nini? kwani Mbowe pekee ndio ana kesi?
MTAGA na UVCCM akili zenu ni kama ngedere, yani jambazi na libakaji na lihujumu uchumi na clip zipo, wananchi wanasema, yeye mwenyewe amekiri alikuwa anatumwa alafu bado tu mnasimama nalo? haki-ya-nani mnanuka damu na hamna huruma kabisa na waTanzania
 
Back
Top Bottom