Lengo la Serikali ni kuwaua wakosoaji? Kesi ya Uhaini ni eneo la kujifunza

Lengo la Serikali ni kuwaua wakosoaji? Kesi ya Uhaini ni eneo la kujifunza

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Kuwakamata na kuwashtaki wakosoaji wa mkataba mbovu wa DPW na Tanzania ni picha inayodhihirisha lengo la serikali yetu tukufu inayojitukuza kuliko uwepo wa Mungu.

Wakili Mwabukusi, Nyangali, Slaa ni public figures ambao serikali inahofia kuwanyamazisha kama ilivyojaribu kwa Tundu Lissu hapo awali.

Kuwashtaki kwa kosa la Uhaini ni picha inaiweka serikali kwenye mizania ya malengo yake kwa hatua mbalimbali za kuizima hii hoja inayojadiliwa sasa nchi nzima na wananchi.

USHAURI
  1. Serikali inabidi ikubali kukosolewa kwa kila hatua inayopiga ya maendeleo
  2. Ukosoaji na kupinga waziwazi siyo tishio kwa ustawi wetu kama nchi bali ni afya ya ushindani wa kifikra hususani kwenye kujenga hoja
  3. Kuwajengea hofu wananchi kwa kuonesha matumizi makubwa ya nguvu kupitia dola ni kuongeza athari za kukosa uvumilivu wa hoja na kisiasa
  4. Serikali kufanya maamuzi na yakaleta utata kimantiki ni vyema ikatumia njia za kidemokrasia kuzikabili hoja kuliko mabavu na vitisho
  5. Mimi kama mwananchi sijioni salama mbele ya serikali yangu. Kwa nini serikali inishughilikie kwa kutoiamini? Je, NI LAZIMA kuiamini serikali kwenye kila kitu?
RAI
Serikali iwaachie wanaharakati na wakosoaji wanaohoji maudhui ya mkataba huu ambao kila mtu sasa amegundua kuwa tunawekwa rehani.
 
Ndiyo maana nasema una utoto! Kuna issue hot Mdude, wewe unaleta mambo ya chopa....
Mungu wa mbinguni hatakubariki kamwe
Wewe unapambana hapa Jf kwa ID fake 😂 Wenzako wako Mbeya na wengine wako Dar wakimpambania Mdude

Wewe ndio kwanza unawapiga marungu nguruwe upate kuwachinja kibudu 😃😃🌟
 
we elimu yako ni kiwango gani, uchochezi, uzushi, upotoshaji, uhaini siyo ukosoaji. Nchi hii ina sheria na taratibu zake, ina viongozi walioapa kulinda ulinzi na usalama wa nchi yetu, lazima utii sheria za nchi vinginevyo unashughulikiwa. Wale ni wahalifu kila mtu alikuwa anawasikia walichokuwa wanahubiri usituletee upuuzi wako kaa kimya wacha washughulikiwe wapuuzi wale.

Watu wanaongea kabisa kumwondoa rais madarakani, wanaongea habari za kuvunja muungano, wanatukana, wanachochea wananchi kufanya maanadamano ya kuitoa serikali madarakani kwa njia haramu bado useme wanakosoa, we akili umemwazima nani, tuanzie hapo.

Watu wanasema tuamke tusiogope, huu siyo uchochezi? Muungano ni mojawapo ya tunu za taifa letu. siyo wa kuuchezea, aliondolewa aliyekuwa rais wa Zanzibar Aboud Jumbe kutaka kuvunja muungano, sembuse hao sisimizi? Hakuna mtu wa kuuvunja huu muungano una manufaa zaidi kuliko kitu kingine chochote. Hata hivyo wanzanzibari km siyo wote wengi wao ni wenyeji wa Tanzania bara mfano mzee Ally Hassan Mwinyi alihamia Zanzibar akiwa mtoto mdogo, alizaliwa Pwani wilaya ya Mkuranga.

Nenda pale Tanga, ndugu zao wako Pemba, Unguja wengi walitokea mikoa ya Pwani na Dar Es Salaam. Kutoka Dar mpaka Unguja(Zanzibar) ni kilomita 50 tu, kwanza nawashangaa akina Mwabukusi, Nshalla, Slaa na wengine kujifanya wana uchungu na bandari ambayo iko kilomita zaidi ya 1000 kutoka walikozaliwa mpaka iliko bandari kuliko waliozaliwa na kukulia karibu na bandari yenyewe.

Wazanzibar km siyo wakoloni kuigawa nchi zetu ndio wangelikuwa wenye bandari ya Dar Es Salaam kuliko siye tulio mbali huku bara. Muungano wetu una mkono wa Mungu mwenyewe na hautakaa uvunjike, sisi ni ndugu.
 
Wewe unapambana hapa Jf kwa ID fake 😂 Wenzako wako Mbeya na wengine wako Dar wakimpambania Mdude

Wewe ndio kwanza unawapiga marungu nguruwe upate kuwachinja kibudu 😃😃🌟
Kwani unajuaje kuwa siko Mbeya . Kichwa kibovu, unaweza kuwa Dar na smart phone unapambana hapo hapo unaingia JF!
 
Kuwakamata na kuwashtaki wakosoaji wa mkataba mbovu wa DPW na Tanzania ni picha inayodhihirisha lengo la serikali yetu tukufu inayojitukuza kuliko uwepo wa Mungu.

Wakili Mwabukusi, Nyangali, Slaa ni public figures ambao serikali inahofia kuwanyamazisha kama ilivyojaribu kwa Tundu Lissu hapo awali.

Kuwashtaki kwa kosa la Uhaini ni picha inaiweka serikali kwenye mizania ya malengo yake kwa hatua mbalimbali za kuizima hii hoja inayojadiliwa sasa nchi nzima na wananchi.

USHAURI
  1. Serikali inabidi ikubali kukosolewa kwa kila hatua inayopiga ya maendeleo
  2. Ukosoaji na kupinga waziwazi siyo tishio kwa ustawi wetu kama nchi bali ni afya ya ushindani wa kifikra hususani kwenye kujenga hoja
  3. Kuwajengea hofu wananchi kwa kuonesha matumizi makubwa ya nguvu kupitia dola ni kuongeza athari za kukosa uvumilivu wa hoja na kisiasa
  4. Serikali kufanya maamuzi na yakaleta utata kimantiki ni vyema ikatumia njia za kidemokrasia kuzikabili hoja kuliko mabavu na vitisho
  5. Mimi kama mwananchi sijioni salama mbele ya serikali yangu. Kwa nini serikali inishughilikie kwa kutoiamini? Je, NI LAZIMA kuiamini serikali kwenye kila kitu?
RAI
Serikali iwaachie wanaharakati na wakosoaji wanaohoji maudhui ya mkataba huu ambao kila mtu sasa amegundua kuwa tunawekwa rehani.
Kosoeni ila msilete uhaini.
 
we elimu yako ni kiwango gani, uchochezi, uzushi, upotoshaji, uhaini siyo ukosoaji. Nchi hii ina sheria na taratibu zake, ina viongozi walioapa kulinda ulinzi na usalama wa nchi yetu, lazima utii sheria za nchi vinginevyo unashughulikiwa. Wale ni wahalifu kila mtu alikuwa anawasikia walichokuwa wanahubiri usituletee upuuzi wako kaa kimya wacha washughulikiwe wapuuzi wale. Watu wanaongea kabisa kumwondoa rais madarakani, wanaongea habari za kuvunja muungano, wanatukana, wanachochea wananchi kufanya maanadamano ya kuitoa serikali madarakani kwa njia haramu bado useme wanakosoa, we akili umemwazima nani, tuanzie hapo.

Watu wanasema tuamke tusiogope, huu siyo uchochezi? Muungano ni mojawapo ya tunu za taifa letu. siyo wa kuuchezea, aliondolewa aliyekuwa rais wa Zanzibar Aboud Jumbe kutaka kuvunja muungano, sembuse hao sisimizi? Hakuna mtu wa kuuvunja huu muungano una manufaa zaidi kuliko kitu kingine chochote. Hata hivyo wanzanzibari km siyo wote wengi wao ni wenyeji wa Tanzania bara mfano mzee Ally Hassan Mwinyi alihamia Zanzibar akiwa mtoto mdogo, alizaliwa Pwani wilaya ya Mkuranga. Nenda pale Tanga, ndugu zao wako Pemba, Unguja wengi walitokea mikoa ya Pwani na Dar Es Salaam. Kutoka Dar mpaka Unguja(Zanzibar) ni kilomita 50 tu, kwanza nawashangaa akina Mwabukusi, Nshalla, Slaa na wengine kujifanya wana uchungu na bandari ambayo iko kilomita zaidi ya 1000 kutoka walikozaliwa mpaka iliko bandari kuliko waliozaliwa na kukulia karibu na bandari yenyewe. Wazanzibar km siyo wakoloni kuigawa nchi zetu ndio wangelikuwa wenye bandari ya Dar Es Salaam kuliko siye tulio mbali huku bara. Muungano wetu una mkono wa Mungu mwenyewe na hautakaa uvunjike, sisi ni ndugu.
Pumba tupu
 
Back
Top Bottom