Uchaguzi 2020 Lengo ni kuwapata viongozi au lengo ni usahihi wa kujaza fomu?

Uchaguzi 2020 Lengo ni kuwapata viongozi au lengo ni usahihi wa kujaza fomu?

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
9,571
Reaction score
35,475
Tanzania ni Taifa la ajabu sana sijawahi kuona. Dunia inatushangaa na vizazi vijavyo vitakuja kutushangaa. Hivi lengo ni kuwapata viongozi au lengo ni usahihi wa kujaza FOMU? Kwanini imekua ni kama mtihani fulani hivi kwamba mtu akikosea kujaza FOMU anaondolewa kwenye nafasi ya kugombea?

Kwa Nini kusiwe na FOMU nyingi tu katika ofisi za Tume na ziwe ZIKIUZWA. Mgombea aelekezwe jinsi ya kujaza na ikitokea akakosea anunue FOMU nyingine, kwani shida iko wapi? Hata hivyo kwa nini wanaokosea wote ni kutoka vyama vya Upinzani tu? Kwa Nini Tume imeweka mitego kwenye Fomu.

Kwa nini umnyime mgombea haki ya kugombea ikiwa kakosea kujaza FOMU tu, kwa Nini uwanyime wananchi haki ya kumchagua mgombea wanaemtaka kwa kumkataa jina lake kwa sababu tu kakosea kujaza FOMU, kwa nini kusiwe na nafasi ya kupewa fomu nyingine hata kwa kuinunua?

Saa nyingine huwa najisikia mnyonge kuwa Mtanzania. Ni nchi pekee Duniani mgombea akikosea kujaza fomu hana nafasi ya kusahihisha na anaenguliwa kabisa. Halafu hebu fikiria mtu Kama Tundu Lissu kweli anaweza kukosea kujaza Fomu. Iko miaka kuna watalii watakua wanakuja kutangalia au kututazama sisi Watanzania kama Ni binadamu halisi au nusu binadamu nusu wanyama.

Anakua amepoteza Haki yake na wanaompenda wanakua wamepoteza Haki yao ya kumchagua.

Mungu ingilia Kati.
 
Leo ramani ipo hivi.

Kikao cha Mahakama kitaanza na kesi itaitwa. Mshtakiwa hatakuwepo mahakamani kwasababu kaenda kwenye tukio la kihistoria ambalo huja maramoja kila baada ya miaka mitano

Mapema kabisa itatolewa hati ya kukamatwa kwake na asubuhi hii hii yatafanyika mawasiliano na law enforcers wa mkoa ilipo ofisi kuu ya kurudisha fomu na watakua wanamsubiri hapo nje kwenye ofisi ya kusimamia tukio la kihistoria.

Njama zikifanikiwa hataweza kurudisha fomu kwani ataongozana na wasalama hadi sehemu salama akapumzishwe kidogo tayari kwa kusafirishwa hadi kwenye mkoa ilipo kesi yake
 
Alipaswa asahihishwe la ikibidi aulizwe unajaza hapa au unaenda kujazia nyumbani Kama anahisi kukosea anapaswa kusaidiwa kwasababu Ile nihaki yake ya msingi,,
 
kiongozi mzuri ni yule anayejua kufuata sheria za nchi. Dunia itakushangaa sana kama unaweka sheria halafu na baadaye ukazivunja makusudi kwa kisingizia kuwa uvunjaji huo ni mzuri.

Kama sheria huipendi, basi kuna utaratibu wa kuifuta. Hata Richard Nixon alikuwa rais mzuri lakini alipovunja sheria za nchi alikumbana na rungu la sheria hiyo.
 
Tatizo ujinga umewazidi chadema, mkikaa mnawaza uropokaji tu na upotoshaji, kesi ni 26/08/2020, nyie mmekaa tu kulishwa maneno. Mnajitekenya na kucheka wenyewe, mnatia hadi huruma, na hakuna wa kuwaonea huruma uchaguzi huu
 
Kama walikosea tu kwenye protocol ya msiba wa Mkapa, akili mwao wakijazana ujinga kwamba kikubwa kufika msibani, mwishowe wakarudishwa.
 
Kwa technologia ya kisasa, picha ya passport size huwa tiyari ndani ya dakika 2 tuu. Je, hizo dakika mbili tume zetu zimeshindwa kusubiri hadi kumpoteza Mbunge? Mfano Devota Minja wa Morogoro. Hili liangaliwe upya endapo hakuna hila yeyote.
 
Kwa technologia ya kisasa, picha ya passport size huwa tiyari ndani ya dakika 2 tuu. Je, hizo dakika mbili tume zetu zimeshindwa kusubiri hadi kumpoteza Mbunge? Mfano Devota Minja wa Morogoro. Hili liangaliwe upya endapo hakuna hila yeyote.
kwa akil yak hiyo,huyo devota anaweza kumshinda abood?? Acha domo mkuu
 
lee van cliff,
Nafikiri wamekua strict Kwa sababu hawa watu wakitokea wakachaguliwa na wapiga Kura ndio wataenda kututungia Sheria na Ile dhana ya kubeza qualification ya kujua KUSOMA na KUANDIKA naona wengi ata kusoma na kuandika hawajui SASA tume imeamua kutembelea humo.
 
Sasa mtu hata kujaza fomu tu hawezi anagombea ili akafanye nini huko bungeni.
 
Tanzania ni Taifa la ajabu sana sijawahi kuona. Dunia inatushangaa na vizazi vijavyo vitakuja kutushangaa. Hivi lengo ni kuwapata viongozi au lengo ni usahihi wa kujaza FOMU? Kwanini imekua ni kama mtihani fulani hivi kwamba mtu akikosea kujaza FOMU anaondolewa kwenye nafasi ya kugombea?
Kwa Nini ukosee kujaza fomu?
 
Tatizo ujinga umewazidi chadema, mkikaa mnawaza uropokaji tu na upotoshaji, kesi ni 26/08/2020, nyie mmekaa tu kulishwa maneno. Mnajitekenya na kucheka wenyewe, mnatia hadi huruma, na hakuna wa kuwaonea huruma uchaguzi huu
Hivi wewe ni mtanzania halisi?
 
Tatizo ujinga umewazidi chadema, mkikaa mnawaza uropokaji tu na upotoshaji, kesi ni 26/08/2020, nyie mmekaa tu kulishwa maneno. Mnajitekenya na kucheka wenyewe, mnatia hadi huruma, na hakuna wa kuwaonea huruma uchaguzi huu
Ningekusoma, kama kusingekuwa na figisu nyingi kwenye chaguzi ndogo na ule wa serikali za mitaa. Kwa kuiba tu, CCM kiboko. Kana Magufuli ni bora, figisu za nini?
 
Tanzania ni Taifa la ajabu sana sijawahi kuona. Dunia inatushangaa na vizazi vijavyo vitakuja kutushangaa. Hivi lengo ni kuwapata viongozi au lengo ni usahihi wa kujaza FOMU? Kwanini imekua ni kama mtihani fulani hivi kwamba mtu akikosea kujaza FOMU anaondolewa kwenye nafasi ya kugombea?...
Mwl siku moja alishawahi kutoa mfano kwamba mbongo akifungwa macho akajafunguliwa akaambiwa hapa uko london sasa tusijuane basi mbongo utafurahi na kusema Asante mungu.
 
Tanzania ni Taifa la ajabu sana sijawahi kuona. Dunia inatushangaa na vizazi vijavyo vitakuja kutushangaa. Hivi lengo ni kuwapata viongozi au lengo ni usahihi wa kujaza FOMU? Kwanini imekua ni kama mtihani fulani hivi kwamba mtu akikosea kujaza FOMU anaondolewa kwenye nafasi ya kugombea?....

Inasikitisha sana ila tukikua tutaacha. Ni kama wakati ule tulivyokuwa tunaporana hata saa za mikononi, leo hii hamna mwenye time nazo.

Jiulize kwa nini zoezi limewekwa siku moja tu? Kwa nini siyo wiki au hata wiki mbili kiasi kwamba kama kuna mapungufu wahusika wajulishwe wayarekebishe?
 
Lengo la uchaguzi ni kupata viongozi kupitia sanduku la kura.

Kujaza fomu ni njia ya kumtambulisha mgombea.

Kasoro ndogo ndogo katika ujazaji wa fomu yapasa zirekebishwe mchakato ukiendelea. Kama hakuna picha mgombea aambiwe alete picha.

Kutumia kasoro za ujazaji fomu kama njia ya kuwaengua wagombea na kupitisha wengine bila kupingwa ni kichocheo cha nia ovu za kuteka, kupora fomu na hata ufisadi wa namna zote.
 
Back
Top Bottom