Rufiji dam
JF-Expert Member
- Feb 20, 2020
- 4,107
- 9,671
Leo nimepanda Mwendokasi ya Kivukoni Kimara muda wa saa 6. Nikawahi mbele kwa Dereva ni sehemu naamini ukikosa seat ni sehemu salama sana.
Ndani ya gari nikawa nawaza shillingi ilivyoota matairi. Kufika Fire(faya) mtu aliyekuwa amekalia kiti akashuka nikajisemea acha nami nikae. Ile nageuka nyuma niangalie kama kuna mzee nimpe hicho kikalio aketi tobaa nikakutana na dada mweupeee sura ina vichunusi hivi. Nikajisemea haya njoo ukae.
Akakaa tukataniana kidogo akashukuru sana, akasema "umejuaje kama nimechoka?" Nikamwambia kujidekeza tu akasema hajalala toka jana nikamuuliza upo ofisi gani akajibu tambua tu sikulala. Nikajinyamazia maana kweli alikuwa amechoka.
Kumchunguza nikaona suruali aliyovaa ya dark blue nikajua huyu ni Askari polisi. Nikashindwa hata kuomba namba si unajua kwenye Mwendokasi hakuna faragha nikasema huyu akishuka tu Kimara ninae eeeh akashukia Korogwe. Nikawaza Mdengereko mie mfukoni nina buku mbili ya kunipeleka Matosa.
Nikamsindikiza kwa macho tu akavuka barabara upande wa Korogwe kama unaenda Mbezi.
Ukweli huyu Askari ni mzuri sana. Kama yoyote anayemjua mfikishie salaam. Undugu ni kusaidiana.
Ndani ya gari nikawa nawaza shillingi ilivyoota matairi. Kufika Fire(faya) mtu aliyekuwa amekalia kiti akashuka nikajisemea acha nami nikae. Ile nageuka nyuma niangalie kama kuna mzee nimpe hicho kikalio aketi tobaa nikakutana na dada mweupeee sura ina vichunusi hivi. Nikajisemea haya njoo ukae.
Akakaa tukataniana kidogo akashukuru sana, akasema "umejuaje kama nimechoka?" Nikamwambia kujidekeza tu akasema hajalala toka jana nikamuuliza upo ofisi gani akajibu tambua tu sikulala. Nikajinyamazia maana kweli alikuwa amechoka.
Kumchunguza nikaona suruali aliyovaa ya dark blue nikajua huyu ni Askari polisi. Nikashindwa hata kuomba namba si unajua kwenye Mwendokasi hakuna faragha nikasema huyu akishuka tu Kimara ninae eeeh akashukia Korogwe. Nikawaza Mdengereko mie mfukoni nina buku mbili ya kunipeleka Matosa.
Nikamsindikiza kwa macho tu akavuka barabara upande wa Korogwe kama unaenda Mbezi.
Ukweli huyu Askari ni mzuri sana. Kama yoyote anayemjua mfikishie salaam. Undugu ni kusaidiana.