Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
[emoji3516]
Mwaka2002 Mwisho Mwampamba wa Moro alikua mtanzania wa kwanza kushinda shindano la Big Brother Afrika kule kwa Madiba na aliporudi kwetu Morogoro akafanyiwa mapokezi makubwa ya heshima.[emoji112]
Mwaka 2004 Selemani Msindi wa Moro akashinda Ufalme wa Rhymes/Bongo fleva Tz jijini Dsm akapata zawadi ya gari na aliporudi kwetu Moro akafanyiwa mapokezi ya kihistoria ya heshima.[emoji112]
Mwaka 2008 Francis Cheka wa Moro alishinda mchezo mgumu wa ngumi jijini Dsm dhidi ya aliyekua bondia bingwa asiyeshindika Rashid Matumla akapewa zawadi ya gari na aliporudi kwetu Moro akafanyiwa mapokezi makubwa ya heshima.[emoji112]
Mwaka 2020 @twaha_kiduku wa Moro alishinda pambano kubwa la ngumi mbele ya Dula Mbabe jijini Dsm akapata zawadi ya gari na kama kawaida aliporudi kwetu Moro akafanyiwa mapokezi makubwa.[emoji112]
Na Katika matukio yote hayo @k_mandonga alikua mstari wa mbele kwenye mapokezi akianza kutupokea kutokea mikese akiwa kidali wazi akitembea na kusindikiza msafara wa mapokezi hadi Moro mjini huku akiwa na furaha kuliko watu wote.[emoji95]
Ndio maana sishangai kuona na yeye leo anapokelewa kwa heshima mjini kwetu Moro baada ya kumpiga Wanyonyo wa Kenya sugunyo za kutosha kutoka Ukraine akiwa nchini kwao Kenya.[emoji1787]
Hapa kupitia Mandonga tunajifunza kuwa ukiwakunjulia moyo wengine basi nawewe utakunjuliwa moyo na wengine kwani waungwana husema aliwazalo mjinga au mjanja ndilo litakalo mtokea na mkono unaotoa ndio mkono utakaopokea "Kunja Sura kunjia Roho".[emoji106]
Each one Teach one.[emoji3578]
Sina Hatia.[emoji119]
"Mimi namfahamu muda mrefu Mandonga. Mandonga ni bondia wa zamani hapa Morogoro, ana jina Morogoro muda mrefu tu hivi vituko vyake asije mtu akamuiga, amezaliwa navyo."
"Ukisema umuoge kama Kaoneka anaongea au anaenda kanisani kutafuta huruma za Mungu anajitafutia shida. Mandonga vile ndivyo alivyozaliwa" - Afande Sele, Msanii wa muziki.
Mji kasoro bahari
Mwaka2002 Mwisho Mwampamba wa Moro alikua mtanzania wa kwanza kushinda shindano la Big Brother Afrika kule kwa Madiba na aliporudi kwetu Morogoro akafanyiwa mapokezi makubwa ya heshima.[emoji112]
Mwaka 2004 Selemani Msindi wa Moro akashinda Ufalme wa Rhymes/Bongo fleva Tz jijini Dsm akapata zawadi ya gari na aliporudi kwetu Moro akafanyiwa mapokezi ya kihistoria ya heshima.[emoji112]
Mwaka 2008 Francis Cheka wa Moro alishinda mchezo mgumu wa ngumi jijini Dsm dhidi ya aliyekua bondia bingwa asiyeshindika Rashid Matumla akapewa zawadi ya gari na aliporudi kwetu Moro akafanyiwa mapokezi makubwa ya heshima.[emoji112]
Mwaka 2020 @twaha_kiduku wa Moro alishinda pambano kubwa la ngumi mbele ya Dula Mbabe jijini Dsm akapata zawadi ya gari na kama kawaida aliporudi kwetu Moro akafanyiwa mapokezi makubwa.[emoji112]
Na Katika matukio yote hayo @k_mandonga alikua mstari wa mbele kwenye mapokezi akianza kutupokea kutokea mikese akiwa kidali wazi akitembea na kusindikiza msafara wa mapokezi hadi Moro mjini huku akiwa na furaha kuliko watu wote.[emoji95]
Ndio maana sishangai kuona na yeye leo anapokelewa kwa heshima mjini kwetu Moro baada ya kumpiga Wanyonyo wa Kenya sugunyo za kutosha kutoka Ukraine akiwa nchini kwao Kenya.[emoji1787]
Hapa kupitia Mandonga tunajifunza kuwa ukiwakunjulia moyo wengine basi nawewe utakunjuliwa moyo na wengine kwani waungwana husema aliwazalo mjinga au mjanja ndilo litakalo mtokea na mkono unaotoa ndio mkono utakaopokea "Kunja Sura kunjia Roho".[emoji106]
Each one Teach one.[emoji3578]
Sina Hatia.[emoji119]
"Mimi namfahamu muda mrefu Mandonga. Mandonga ni bondia wa zamani hapa Morogoro, ana jina Morogoro muda mrefu tu hivi vituko vyake asije mtu akamuiga, amezaliwa navyo."
"Ukisema umuoge kama Kaoneka anaongea au anaenda kanisani kutafuta huruma za Mungu anajitafutia shida. Mandonga vile ndivyo alivyozaliwa" - Afande Sele, Msanii wa muziki.
Mji kasoro bahari