Leo ndio nimejua kwanini TANESCO wamegoma kushusha bei ya umeme hata baada ya Bwawa kuanza kazi mwakani

Viwanda vinahitaji mtaji,Bei ya umeme ni factor ndogo,mtu hawezi anzisha kiwanda kisa tu Bei ya umeme ndogo
 
Bt kwa akili ya kawaida tu how comes 2600Megawatts ziongezeke then bei isishuke jmn,I wish angekuwepo chuma...yan watu huku umeme ushakuwa wa kuwashia taa tu hata kutumia pasi inaonekana ni anasa kwa sababu ya gharama kubwa ya umeme.
Kabisa, lengo la mradixlilikuwa kushusha bei ya umeme na kichagiza ukuaji wa viwanda ili vijana wapate ajira na kukuza uchumi. Leo hii hata kutumia heater kuchemshia maji ni anasa, umeme watu wanawashia taa tu, tena ya nje inawashwa moja tu.., vieanda viko hoi, umeme bei juu!! Sasa zinaingiaje Megawatt 2,100 mpya kabisa na bei isishuke?! How!???
 
Huo mradi wa kuongeza megawatt umejengwa bure?
Hizo gharama za ujenzi nani analipa? Si mwananchi? Sasa anepaswa kufaidika na uwekezaji wake ni nani kama si mwananchi?
Na kama gharama za kuzalisha umeme zinashuka, na umeme ni mwingi kuliko demand ya ndani ni kwanini bei isishuke?
 
Hizo gharama za ujenzi nani analipa? Si mwananchi? Sasa anepaswa kufaidika na uwekezaji wake ni nani kama si mwananchi?
Na kama gharama za kuzalisha umeme zinashuka, na umeme ni mwingi kuliko demand ya ndani ni kwanini bei isishuke?
Unalipaje wakati hata kodi hulipi
 
Viwanda vinahitaji mtaji,Bei ya umeme ni factor ndogo,mtu hawezi anzisha kiwanda kisa tu Bei ya umeme ndogo
Acha kujitoa akili, umeme (nishati) ni critical factor katika uzalishaji wa kisasa, ni kama yalivyo mafuta, bei ya hivi viwili vikishuka, impact yake kwenye sekta zote ni kubwa mno!
 
Nakupata vizuri..yaani Kuna plan inapigwa ya kupiga.
 
Acha kujitoa akili, umeme (nishati) ni critical factor katika uzalishaji wa kisasa, ni kama yalivyo mafuta, bei ya hivi viwili vikishuka, impact yake kwenye sekta zote ni kubwa mno!
Mtu mwenye mtaji ambaye hakuwa na nia ya kuanzisha kiwanda, hawezi anzisha kiwanda kisa umeme umeshuka bei
 
"can’t imagine huyo mama abaki hapo hadi 2030, kweli?!! Tanganyika Tutakuwa na hali gani sisi, si tutakuwa tunatembea tunaongea wenyewe kama wehu?!"

UNAONGELEA ABAKI HADI 2030 WAKATI WAKULUNGWA WANATAKA KUMCHOMOA KABLA MWAKA HUU HAUJAISHA😂😂😂😂🤣🤣
INSHORT WATANZANIA TUMEPIGWA.
 
Hata haiwezi kuwa hivo!

BWN MAHARAGE CHANDE anazo hoja lakini aliongea as if sisi wote tunafanya kazi TANESCO na tunajua hali ilivyo!

Ukweli ni kwamba Mradi ukikamilika kutaisaidia TANESCO kuwa na Stable supply ya Ndani ns Ziada Nje lakini watakuwa na Ombwe la Uwekezaji kwenye Miundombinu ya usambazaji umeme kwa wateja ambao imechakaa sana!

Pili ni Kwamba Deni lililojenga Bwawa ni kubwa na hivo ni Afya kwa Serikali kulilipa mapema ili tuweze kupata umafuu wa Finance kwenye maeneo mengine...

Tatu ni kwamba TANESCO inaendeshwa kwa Ruzuku...baada ya Mradi itabidi Shirika lijipange kujiendesha na kuipstia Serikali Gawio Nono!

Ili hayo yawezekane inabidi Tarrifs zibaki hizi hizi kwa miaka si chini ya Mitatu/Mitano kisha ishuke taratibu mpk kuwa competitive and attractive!

Halafu
TANESCO wamerekebisha Sheria na kuruhusu Uwekezaji na uzalishaji wa Umeme na kuuzia TANESCO licha ya Ongezeko linalotegemewa...

Anzaia hapo...
Tafuta fursa wewe binafsi kuanzia hapo...hayo mengine ni Majungu tu!
 
Mtu mwenye mtaji ambaye hakuwa na nia ya kuanzisha kiwanda, hawezi anzisha kiwanda kisa umeme umeshuka bei
Nishati ya umeme ni critical driving factor ya viwanda, hilo ni dhahiri, au mashine viwandani zinaendeshwa kwa mkaa?!
 
Hataree
 
Ombwe la uwekezaji kwenye miundombinu kwa mantiki ipi? Hapa tunazungumzia kwa wateja ambao tayari wameshaunganishwa na gridi, kama umeme umezalishwa mwingi, utaoelekwa wapi wote kama hakuna incentive ya kuwafanya utumike wote na kuisha, maana huwezi kuhifadhi umeme kwenye battery, lazima utumike wote nauishe, na ziada inayobaki iuzwe nje ili kuinua shirika loweza kusimama imara.

Hilo deni unalozungumiza hata sasa linalipwa kwa kodi lukuki zilizopo, inaleta mantiki zaidi kwa umeme ukiozalisjwa kwa gharama nafuu na uliomwingi kuliko mahitaji ya ndani, Ile excess ikauzwa kwa faida nje ya nchi, ila ule unaozwa ndani ukashuka bei accordingly ambapo kupitia ukuaji wa viwanda na kuongezeka kwa ajira serikali ikakusanya kodi kubwa zaidi na kusaidia kulipa mikopo yetu kwa ujumla, na hata ruzuku isihitajike tena, kwa i tayari kuna mapato yatokanayo na uuzaji umeme nje ya nchi.

Kuuza ziada nje ya nchi hakuzuii kushusha umeme ndani ya nchi!

Kibaya zaidi, umeme utakaouzwa nje ya nchi kuna watotocwa vigogo wanaunda vikampuni ili wapokee hizo fedha za mauzo.., mfano huyo wa solar, umeme utoke Rufiji mseme ni wa Solar zake
 
Haijalishi, msisahau na Ahadi alizowapea Waarabu kule Dubai, wa kuwagawia Tanesco baada ya kudumbukiza matrillioni ya Fedha za watoa Jasho Tanzania .

Hatahivyo msiwatafutie pahali pa kutokea, hakuna cha Law of Supply and Demand wala nini...ni Ufisadi tu.

Wanachokifanya ni kujisapply wenyewe.
 
Hili bando nimetoa wapi? Si nimenunua, na kodi si wamekata? Au kodi unazungumzia?
Kwa hiyo iyo hela yako ndo inaenda kuzalisha umeme? Barabara zinajengewa hela ipi? Dawa hospitalini zinanunuliwa kwa hela ipi? Mishahara ya watumishi wa Umma inalipiwa hela ipi?

Icho ki 150 za vocha ndo kifanye upunguziwe umeme? Chizi kabisa wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…