Leo ndio nimejua kwanini TANESCO wamegoma kushusha bei ya umeme hata baada ya Bwawa kuanza kazi mwakani

Leo ndio nimejua kwanini TANESCO wamegoma kushusha bei ya umeme hata baada ya Bwawa kuanza kazi mwakani

Tangu Maharage pale TANESCO alipotoa tamko lisilo na mantiki na linalo-defy all logical reasoning, kwamba eti hata baada ya Megawatt 2100 kuanza kuzalishwa kwenye bwawa la Nyerere na kuingizwa kwenye Gridi bado eti umeme hautashuka bei, nimekuwa nikiwaza sana nisielewe hii itawezekana vipi?!

Ni kwamba Law ya demand vs Supply inagoma kabisa!! Kwamba matumizi yetu hivi sasa ni Megawatt 1,600, na ndizo zinazalishwa kwa sasa, halafu ghafla uingize Megawatt 3,700 kwenye gridi, huo umeme wote atautumia nani kwa ghafla hivyo hadi uishe?

Tulitegemea kwa kuwa umeme hauwezi kutunzwa kwenye betri, kwamba Tanesco washishe bei ili hadi vijijini wapikie majiko ya umeme, kiasi umeme huo sasa utumike wote bila kupotea, vinginevyo itabidi tufungulie maji bwawani yamwagike bire bila kuzalisha umeme.

Sasa leo ndio nimejua mchezo wanaotaka kufanya, ni mwamba hizo Megawatt 2,100 za Bwawa la Nyerere tutazisikia kwenye bomba tu, maana zitaingizwa kwenye gridi ya taifa na kuwa offloaded kwenda Zambia, Malawi, Uganda, Kenya ,Zanzibar, Burundi, Rwanda, Msumbiji, na hata sentano mbuni hatutaiona ya mauzo ya umeme. How? Kwanini nasema hivi?

1.) Umeme huo hautaonekana kwamba umetoka Tanesco, bali kuna dogo mmoja inadaiwa ni mtoto wa mama yetu, yeye kaongozana eti na maafisa wa Wizara ya Nishati ili azalishe umeme wa Solar na kuiuzia Uganda , 😂😂😂, kwamba umeme utoke Rufiji, mseme ni umeme jua wa huyo dogo? Halafu malipo yote alipwe yeye?!! 😂😂😂 , ujamja wa kizani sana huu...

2.) Inadaiwa January Makamba anakazana sana kuunganisha gridi ya Tanzania na Gridi za Rwanda kupitia Rusumo, na anafanya mikutano na nchi nyingi zinazotuzunguza hasa malawi, Zambia na wengine eti tuunganishe gridi yetu kwa pamoja ili tuuziane umeme panapokuwa na upungufu. Shida hapa ni kwamba umeme utatoka Rufiji halafu watasema ni umeme wa gesi, hivyo malipo yataenda kwa wenye gesi yao.., sisi tutabaki kulipa mkopo wa Trillion 10 zilizotumika kujenga hiko bwawa, kwa tozo za miamala na kodi za majengo za kwenye umeme zilizopoandishwa.

Hivi mtu mwenye akili timamu unakubali vipi kuambiwa kwamba Megawatt 2,100 ziingizwe kwenye gridi na bado zote zitumike ziishe bila kushusha bei?!!!

We are finished!! Tumekwisha...

View attachment 2715874

I can’t imagine huyo mama abaki hapo hadi 2030, kweli?!! Tanganyika Tutakuwa na hali gani sisi, si tutakuwa tunatembea tunaongea wenyewe kama wehu?!

=========================
Hii mijizi ukiona vile mama alivyoirejesha jpm baada ya kuwatema ndio unashindwa hata kuamini kama kuondoka magufuli ni mapenzi ya mungu. Wanajipanga kuiteka nyara nchi.
 
Ujinga ni mzigo kwa hiyo kampuni za kitanzania kwenda kuuza umeme ili kutuletea kipato nayo ni nongwa?

Yaani tayari ni ajenda ya kisiasa sisi masikini kama tunaweza kupata vya kuuza ili tujiingizie kipato ni jambo zuri sio tu kuuza mahindi na maharage.

Kama tunauza na umeme jambo zuri sana hata awe mtoto wa nani binafsi nasupport kampuni za kitanzania kufanya hivyo.

Sio kila siku zinakuwa tu kampuni za kigeni kufanya hivyo napongeza sana kampuni ya tanzania inayofanya h
Hoja hapa watu binagsi wanauza umeme gani nje. Kuna hila za watu binafsi kuuza umeme wa tanesco huku wakijifanya wamezalisha wao.
Jiulize kwa nini kuwe na watu binafsi kutafuta masoko kuuza umeme nje sasa na sio kabla ya kuwepo umeme wa bwawa la nyerere? Tunachotaka ni kushuka bei ya umeme utakopoanza kupatikana kwa gharama ya chini na sio kuuzwa nje na watu binafsi kujidai ni umeme wanazalisha wao.
Januari na maharage lazima kudhibitiwe na umma maana mama amewaweka pale kwa ajili ya upigaji tu. Umma wa wananchi tusikubali.
 
Bwawa kagharamia nani huo ujenzi wake? Maana unaongea as if hilo bwawa kuna mtu huko katoa zawadi pesa yake mfukoni kajenga, na sio wananchi
Uchumi hauendi hivyo, pesa tayari ni za serikali bila kujali ni mkopo au Kodi au Mapato yasiyo Kodi. Sasa kama serikali imeingia gharama kujenga say trillion 6 unadhani italipaje marejesho ya mkopo plus gharama za kuendesha ikishusha bei siku ya kwanza?

Ndio maana nikasema Tanesco ni monopoly so mjadala wake hauwezi husisha demand and supply kwenye kuamua bei.

CCM wanapenda maneno ya kutuhadaa tu ikija utekelezaji wanaturuka. Hata Hilo daraja la busisi likiisha usishangae watu wakatozwa 200 kuvuka hapo.
 
Uchumi hauendi hivyo, pesa tayari ni za serikali bila kujali ni mkopo au Kodi au Mapato yasiyo Kodi. Sasa kama serikali imeingia gharama kujenga say trillion 6 unadhani italipaje marejesho ya mkopo plus gharama za kuendesha ikishusha bei siku ya kwanza?

Ndio maana nikasema Tanesco ni monopoly so mjadala wake hauwezi husisha demand and supply kwenye kuamua bei.

CCM wanapenda maneno ya kutuhadaa tu ikija utekelezaji wanaturuka. Hata Hilo daraja la busisi likiisha usishangae watu wakatozwa 200 kuvuka hapo.
Kwa kushusha gharama za umeme na kuongeza uwekezaji na uzalishaji wa bidhaa Viwandani zenye ushindani Wa soko la ndani na nje, pamoja kuongeza ajira na kukuza uchumi, haitawezesha kulipa deni?
 
Hoja hapa watu binagsi wanauza umeme gani nje. Kuna hila za watu binafsi kuuza umeme wa tanesco huku wakijifanya wamezalisha wao.
Jiulize kwa nini kuwe na watu binafsi kutafuta masoko kuuza umeme nje sasa na sio kabla ya kuwepo umeme wa bwawa la nyerere? Tunachotaka ni kushuka bei ya umeme utakopoanza kupatikana kwa gharama ya chini na sio kuuzwa nje na watu binafsi kujidai ni umeme wanazalisha wao.
Januari na maharage lazima kudhibitiwe na umma maana mama amewaweka pale kwa ajili ya upigaji tu. Umma wa wananchi tusikubali.
Weka evidence mezani ya kuwa umeme watu wanaiba sijui kwenye ndoo wanaenda kuuza nje otherwise ni hadaa.
Huwezi kupunguza bei tutaendelea kujenga taifa la wavivu kwa style hio kama kila kitu kigaiwe bure bure na tutakuwa tunajenga uchumi na huku tunaongeza matobo kwenye uchumi huo huo kwa wakati huo huo ,tukifanya hivyo itakuwa stori ya maendeleo na kukuza uchumi kwetu sawa na pakacha kulijaza maji yanayoingia yote yanatoka na umasikini unaendelea kutaradadi.
 
Weka evidence mezani ya kuwa umeme watu wanaiba sijui kwenye ndoo wanaenda kuuza nje otherwise ni hadaa.
Huwezi kupunguza bei tutaendelea kujenga taifa la wavivu kwa style hio kama kila kitu kigaiwe bure bure na tutakuwa tunajenga uchumi na huku tunaongeza matobo kwenye uchumi huo huo kwa wakati huo huo ,tukifanya hivyo itakuwa stori ya maendeleo na kukuza uchumi kwetu sawa na pakacha kulijaza maji yanayoingia yote yanatoka na umasikini unaendelea kutaradadi.
Umeme wa maji ni mwingi na ni nafuu, objectives za mradi ilkuwa ni kutumia rasilimali ya mto Rufiji kuzalisha umeme wa bei nafuu utakaoweza kuchagiza uzalishaji wenye tija viwandani nankuongeza viwanda vitakavyozalisha bidhaa zenye ushindani katika masoko ya ndani na ya nje, kuzalisha ajira na kukuza uchumi, hayo yataletq mapatocmengi serikalini na kugharamia mikopo yote, kwanini mnapindisha malengo kwa maslahi ya Akina Abduli na kiparangoto?
 
Weka evidence mezani ya kuwa umeme watu wanaiba sijui kwenye ndoo wanaenda kuuza nje otherwise ni hadaa.
Huwezi kupunguza bei tutaendelea kujenga taifa la wavivu kwa style hio kama kila kitu kigaiwe bure bure na tutakuwa tunajenga uchumi na huku tunaongeza matobo kwenye uchumi huo huo kwa wakati huo huo ,tukifanya hivyo itakuwa stori ya maendeleo na kukuza uchumi kwetu sawa na pakacha kulijaza maji yanayoingia yote yanatoka na umasikini unaendelea kutaradadi.

Hapa ndipo pesa inapopelekwa
 
Hivi vipuli vya mitambo ya bwawa la Mwalimu Nyerere vinapatikana wapi?
 
Ujinga ni mzigo kwa hiyo kampuni za kitanzania kwenda kuuza umeme ili kutuletea kipato nayo ni nongwa?

Yaani tayari ni ajenda ya kisiasa sisi masikini kama tunaweza kupata vya kuuza ili tujiingizie kipato ni jambo zuri sio tu kuuza mahindi na maharage.

Kama tunauza na umeme jambo zuri sana hata awe mtoto wa nani binafsi nasupport kampuni za kitanzania kufanya hivyo.

Sio kila siku zinakuwa tu kampuni za kigeni kufanya hivyo napongeza sana kampuni ya tanzania inayofanya hivyo.
Moja ya sababu kubwa ya kujenga mradi huo ni umeme kushuka bei. Ndicho alichotuambia Hayati Magufuli.
Faida za kushusha bei viwanda/migodi vitapunguza gharama za uzalishaji na kuvutia uwekezaji. Impact yake tutaongeza mapato itakuwa rahisi kulipa madeni mnayoyasema, maana tutakuwa na fedha zaidi, aidha tutalinda mazingira, maana matumizi ya mkaa na kuni vitapungua. Tutapunguza gharama za maisha kutokana na kupunguza kwa gharama za uzalishaji viwandani.
Kushusha bei ya umeme ndicho walichotarajia watanzania wengi na ni kama ilisaidia kushawishi watu wengi kuunga mkono huo mradi.
 
Umeme wa maji ni mwingi na ni nafuu, objectives za mradi ilkuwa ni kutumia rasilimali ya mto Rufiji kuzalisha umeme wa bei nafuu utakaoweza kuchagiza uzalishaji wenye tija viwandani nankuongeza viwanda vitakavyozalisha bidhaa zenye ushindani katika masoko ya ndani na ya nje, kuzalisha ajira na kukuza uchumi, hayo yataletq mapatocmengi serikalini na kugharamia mikopo yote, kwanini mnapindisha malengo kwa maslahi ya Akina Abduli na kiparangoto?
Ndio kwa kuwa ni mwingi na ni nafuu kuzalisha na pia viwanda vitakuwa na uhakika wa umeme basi tutajihakikishia profit na ndio tunataka tutengeneze surplus ya kufanya mambo mengine ya kukuza uchumi bei haishushwi acha pesa na surplus itengenezwe tupunguze kodi maeneo mengine ili sekta mbalimbali mtambuka za kiuchumi zikue zaidi na kuchangia zaidi pato la taifa. Maana adha ya viwanda kuwa na njia nyingine mbadala sijui makaa ya mawe au magenereta itakuwa hayahitajiki tena kama njia mbadala kwa kuwa watapata nishati ya uhakika na watalipia na pia watajipunguzia gharama za ziada za kununua mafuta au makaa ya mawe kwa ajili ya uendeshaji wa viwanda kwa kuwa na uhakika wa umeme mwaka mzima.
 
Moja ya sababu kubwa ya kujenga mradi huo ni umeme kushuka bei. Ndicho alichotuambia Hayati Magufuli.
Faida za kushusha zitahamasisha viwanda vilivyopo kupunguza gharama za uzalishaji na kuvutia uwekezaji. Impact yake tutaongea mapato, na tutailinda mazingira, maana matumizi ya njaa na kuni vitapungua. Tutapunguza gharama za maisha kutokana na kupunguza kwa gharama za uzalishaji viwandani.
Kushusha bei ya umeme ndicho walichotarajia watanzania wengi na ni kama ilisaidia kushawishi watu wengi kuunga mkono huo mradi.
Gharama za viwandani zitapungua kwa kuwa watakua na uhakika wa umeme bila kuhitaji installation ya mitambo ya ziada kuzalisha umeme bei watalipa hii hii tu. Lengo kuu la mradi ni kuhakikisha nchi inajitosheleza ktk nishati ya umeme kuepusha mgao wa umeme hili ndio kuu kabisa kukiwa na mgao uzalishaji mali unaathirika sana na pato la taifa linayumba kwa kipindi hicho.
 
Kupikia umeme uogo
Watu wenyewe wa mijini matajiri wanatumia majiko.ya gesi.

Ndio vijijini watumie umeme kupikia?

Jengeni hoja za kueleweka

Subsidy kubwa iwekwe kwenye gesi ya kupikia

Hizo porojo za kusema ohh watapikia majiko.ya umeme vijijini ni uongo uliopitiliza
Sasa unasema ivyo na unaguvu ,Sasa sababu Alie lianzisha Alisha kufa na mmekuja na ya maharege
 
Ndio kwa kuwa ni mwingi na ni nafuu kuzalisha na pia viwanda vitakuwa na uhakika wa umeme basi tutajihakikishia profit na ndio tunataka tutengeneze surplus ya kufanya mambo mengine ya kukuza uchumi bei haishushwi acha pesa na surplus itengenezwe tupunguze kodi maeneo mengine ili sekta mbalimbali mtambuka za kiuchumi zikue zaidi na kuchangia zaidi pato la taifa. Maana adha ya viwanda kuwa na njia nyingine mbadala sijui makaa ya mawe au magenereta itakuwa hayahitajiki tena kama njia mbadala kwa kuwa watapata nishati ya uhakika na watalipia na pia watajipunguzia gharama za ziada za kununua mafuta au makaa ya mawe kwa ajili ya uendeshaji wa viwanda kwa kuwa na uhakika wa umeme mwaka mzima.
Ulichoongea kwakweli kinakosa mtiririko wa kimantiki, sikatai kwamba umejibu, ila ni kama mbwa anabweka tu, hata sielewi hoja yako yabkuoinga kushuka umeme ni ipi, mara majenereta, mara makaa ya mawe, hata sielewi. Ngoja watakaolewa wanisaidie
 
Niliwaambia ccm tukingoja hadi 2025 bado tutavuna mabua, hawa dawa yao ni kuwaondoa kwa nguvu ya umma,wananchi wote tukiingia barabara watatoka tu hii nchi sio mali yao.
Duuu yaani watu waache kula Raha ikulu watoke kisa wewe umeingia barabarani kama ni hivyo wangekuwa washatoka maana Kila siku tuko barabarani na magari
 
Umeme utoke Rufiji halafu mseme ni wa Rostam?

 
Back
Top Bottom