gammaparticles
JF-Expert Member
- Jan 9, 2024
- 1,407
- 3,855
Shambulio la Bomu Dhidi ya Balozi za Marekani (Kenya na Tanzania)
Soma pia:FBI walivyomdaka Thomas Lyimo 1998
Imepita miaka 25 tangu shambulio la bomu la ubalozi wa Marekani jijini Nairobi na Dar es Salaam kusababisha maafa na kuacha majeruhi.
Waathiriwa hao bado wanasaka fidia kutoka kwa serikali ya Marekani.
Soma zaidi: Miaka 20 baada ya mashambulizi ya pamoja Kenya na Tanzania, Ugaidi bado ni kitisho
Douglas Sidialo ni mmoja ya waliojeruhiwa kwenye shambulio hilo la kigaidi la mwaka 1998, naye anasema maisha yake yalibadilika na alipoteza uwezo wake wa kuona.
"Kwa sasa nahitaji usaidizi kufanya shughuli za kila siku." Anasema manusura huyo.
Ili kuiongeza kasi ya kudai fidia kutoka kwa serikali ya Marekani, Kamati ya Muda ya Seneti ilianzisha mchakato mpya. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati hiyo, Agnes Kavindu, anasema "upo mpango wa kukutana na baraza la Seneti la Marekani ili kufuatilia suala la fidia."
Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu mashambulio ya mabomu ya mwaka 1998 dhidi ya Balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania. Mnamo tarehe 7 mwezi Agosti, mwaka 1998, wanachama wa kundi la kigaidi la al-Qa’ida (AQ) sawia walishambulia kwa mabomu Balozi za Marekani Nairobi na Dar es Salaam. Mashambulio hayo yaliwaua watu 224, yakawajeruhi wengine zaidi ya 4,500, na yakasababisha hasara kubwa kwenye majengo ya balozi hizo na uharibifu wa miundo iliyokuwa karibu.
Jijini Nairobi, magaidi walilipua lori lililobebeshwa vilipukaji karibu na maegesho ya ubalozi huo na kuwaua watu 213 — wakiwamo wafanyakazi 44 wa ubalozi (Wamarekani 12 na raia 32 wa mataifa ya kigeni) — na kuwajeruhi watu wengine 4,500, akiwamo Balozi wa Marekani Prudence Bushnell.
Jijini Dar es Salaam, magaidi walioendesha loriu lililobebeshwa vilipukaji walijaribu kuligonga lango la ubalozi, wakapiga risasi masijala ya ubalozi, na halafu wakalipua vilupukaji vyao. Mlipuko huo uliwaua watu 11 na kuwajeruhi 85.
Watu wafuatao walishtakiwa na kupatikana na hatia kwenye mahakama ya serikali kuu ya Marekani kuhusiana na mashambulio hayo:
Tuzo kwa Mahakama pia tuzo zawadi kwa taarifa kuhusu kiongozi wa AQ Sayf al-Adl, ambaye alishtakiwa kwa jukumu lake katika milipuko ya Ubalozi.
Kesi ya mfungwa aliyekuwa akishikiliwa katika gereza la Guantanamo imeanza kusikilizwa katika mahakama ya mjini New York, Marekani, hii ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika kesi ya aina hiyo.
Mtanzania Ahmed Khalfan Ghailani, anayetuhumiwa kusaidia mashambulio ya kigaidi katika ubalozi wa Marekani, Kenya na tanzania mwaka 1998
Mtanzania, Ahmed Khalfan Ghailani ambaye anatuhumiwa kuhusika na mauaji ya watu 224 katika shambulio la mabomu lililotokea mwaka 1998 dhidi ya ubalozi wa Marekani nchini Tanzania na Kenya, alionekana akitabasamu na kutaniana na mawakili wake wakati zoezi la kuwachagua wajumbe wa baraza la mahakama lilipokuwa likiendelea katika chumba cha mahakama mjini New York.
ngawa ulinzi ulikuwa mkali ndani ya mahakama hiyo ambayo iko jirani na eneo lilipokuwa kituo cha biashara cha kimataifa kilichoteketezwa wakati wa shambulio la kigaidi la Septemba 11, maeneo kuzunguuka eneo hilo ilikuwa katika hali ya kawaida, huku watalii, wafanyakazi na wakaazi wa eneo hilo wakiendelea na shughuli zao.
Jana Jaji Lewis Kaplan alichuja jopo la wajumbe hao, ambao hawatajulikana muda wote wa uendeshaji kesi hiyo.
Amefafanua kuwa yeye na wanasheria wa pande zote mbili walikubaliana kupunguza jopo hilo, kutoka mamia ya watu hadi kufikia watu 12, ikiwemo wale wa akiba, ifikapo Jumatatu.
Na katika kuonesha kuwa kesi hiyo ni nyeti, Jaji Kaplan alisisitizia kuhakikishia majaji wa baraza la mahakama kwamba majina yao, sehemu wanazofanyia kazi na makaazi yao hayatawekwa hadharani.
Mwaka jana, Ghailan alikanusha kusaidia mipango ya shambulio hilo la mabomu katika ubalozi wa Marekani Dar es Salaam, Tanzania, huku bomu jingine likilipuka katika muda huohuo kwenye ubalozi wa Nairobi Kenya.
Anadaiwa pia kuwa msaidizi wa karibu wa Osama bin Laden.
Wanasheria wake walijaribu kuizuia kesi hiyo, wakihoji kuwa haki za kisheria za mteja wao zimekuwa zikikandamizwa kutokana na kuteswa katika gereza la siri la shirika la Ujasusi la marekani CIA, na pia kuwekwa kizuizini kwa miaka mitano, ikiwemo katika gereza la Guantanamo, kabla ya kesi yake kusikilizwa mahakamani.
Anakabiliwa na kifungo cha maisha, iwapo atatiwa hatiani.
Kesi hiyo ni mtihani kwa Rais wa nchi hiyo Barack Obama kwa ahadi yake ya kumaliza mateso na ukiukaji wa haki katika vita dhidi ya ugaidi. Kwa mara ya kwanza kesi hiyo ilisikilizwa jana Jumatano.
Itakumbukwa kuwa lori lililosheheni mabomu liliripuka nje ya ubalozi wa Marekani uliokuwa katikati ya jiji la Nairobi na shambulio jengine lilitokea Dar es Salaam katika nchi jirani ya Tanzania kwa wakati mmoja.
Marekani ilimtuhumu kiongozi wa kundi la kigaidi la Al Qaeda, Osama Bin Laden aliyeuawa mwaka 2011, kwa kuamuru na kupanga mashambulizi hayo.
Soma pia:FBI walivyomdaka Thomas Lyimo 1998
Imepita miaka 25 tangu shambulio la bomu la ubalozi wa Marekani jijini Nairobi na Dar es Salaam kusababisha maafa na kuacha majeruhi.
Waathiriwa hao bado wanasaka fidia kutoka kwa serikali ya Marekani.
Soma zaidi: Miaka 20 baada ya mashambulizi ya pamoja Kenya na Tanzania, Ugaidi bado ni kitisho
Douglas Sidialo ni mmoja ya waliojeruhiwa kwenye shambulio hilo la kigaidi la mwaka 1998, naye anasema maisha yake yalibadilika na alipoteza uwezo wake wa kuona.
"Kwa sasa nahitaji usaidizi kufanya shughuli za kila siku." Anasema manusura huyo.
Ili kuiongeza kasi ya kudai fidia kutoka kwa serikali ya Marekani, Kamati ya Muda ya Seneti ilianzisha mchakato mpya. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati hiyo, Agnes Kavindu, anasema "upo mpango wa kukutana na baraza la Seneti la Marekani ili kufuatilia suala la fidia."
Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu mashambulio ya mabomu ya mwaka 1998 dhidi ya Balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania. Mnamo tarehe 7 mwezi Agosti, mwaka 1998, wanachama wa kundi la kigaidi la al-Qa’ida (AQ) sawia walishambulia kwa mabomu Balozi za Marekani Nairobi na Dar es Salaam. Mashambulio hayo yaliwaua watu 224, yakawajeruhi wengine zaidi ya 4,500, na yakasababisha hasara kubwa kwenye majengo ya balozi hizo na uharibifu wa miundo iliyokuwa karibu.
Jijini Nairobi, magaidi walilipua lori lililobebeshwa vilipukaji karibu na maegesho ya ubalozi huo na kuwaua watu 213 — wakiwamo wafanyakazi 44 wa ubalozi (Wamarekani 12 na raia 32 wa mataifa ya kigeni) — na kuwajeruhi watu wengine 4,500, akiwamo Balozi wa Marekani Prudence Bushnell.
Jijini Dar es Salaam, magaidi walioendesha loriu lililobebeshwa vilipukaji walijaribu kuligonga lango la ubalozi, wakapiga risasi masijala ya ubalozi, na halafu wakalipua vilupukaji vyao. Mlipuko huo uliwaua watu 11 na kuwajeruhi 85.
Watu wafuatao walishtakiwa na kupatikana na hatia kwenye mahakama ya serikali kuu ya Marekani kuhusiana na mashambulio hayo:
- Mamdouh Mahmud Salim, mwanachama mwanzilishi wa AQ, alikamatwa mnamo mwezi Septemba, mwaka 1998 nchini Ujerumani na kurejeshwa Marekani. Anatumika kifungo cha maisha gerezani kwa kuhusiana kwake na mashambulio hayo ya mabomu.
- Mnamo mwezi Oktoba, mwaka 2001, majasusi wa AQ Wadih El-Hage, Khalfan Khamis Mohamed, Mohamed Rashed Daoud Al-Owhali, na Mohamed Sadeek Odeh walipatikana na hatia kwa mashtaka ya kupanga na kutekeleza mashambulio hayo ya mabomu na wakahukumiwa kufungwa maisha gerezani.
- Mnamo mwezi Januari, mwaka 2011, jasusi wa AQ Ahmed Khalfan Ghailani alipatikana na hatia na akahukumiwa kifungo cha maisha kwa jukumu lake katika mashambulio hayo ya mabomu.
- Mnamo mwezi Septemba, mwaka 2014, Adel Abdel Bari, mshirika wa karibu wa kiongozi wa AQ Ayman al-Zawahiri, alikiri shtaka la kula njama ya kuwaua raia wa Marekani na kupokea kifungo cha miaka 25 gerezani. Aliachiliwa huru kutoka gerezani mnamo mwaka 2020.
- Mnamo mwezi Mei, mwaka 2015, Khaled al-Fawwaz, naibu wa kiongozi wa AQ ambaye sasa ni marehemu Usama bin Laden, alihukumiwa kifungo cha maisha gerezani kwa kuhusiana kwake na mashambulio hayo.
Tuzo kwa Mahakama pia tuzo zawadi kwa taarifa kuhusu kiongozi wa AQ Sayf al-Adl, ambaye alishtakiwa kwa jukumu lake katika milipuko ya Ubalozi.
Kesi ya mfungwa aliyekuwa akishikiliwa katika gereza la Guantanamo imeanza kusikilizwa katika mahakama ya mjini New York, Marekani, hii ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika kesi ya aina hiyo.
Mtanzania Ahmed Khalfan Ghailani, anayetuhumiwa kusaidia mashambulio ya kigaidi katika ubalozi wa Marekani, Kenya na tanzania mwaka 1998
Mtanzania, Ahmed Khalfan Ghailani ambaye anatuhumiwa kuhusika na mauaji ya watu 224 katika shambulio la mabomu lililotokea mwaka 1998 dhidi ya ubalozi wa Marekani nchini Tanzania na Kenya, alionekana akitabasamu na kutaniana na mawakili wake wakati zoezi la kuwachagua wajumbe wa baraza la mahakama lilipokuwa likiendelea katika chumba cha mahakama mjini New York.
ngawa ulinzi ulikuwa mkali ndani ya mahakama hiyo ambayo iko jirani na eneo lilipokuwa kituo cha biashara cha kimataifa kilichoteketezwa wakati wa shambulio la kigaidi la Septemba 11, maeneo kuzunguuka eneo hilo ilikuwa katika hali ya kawaida, huku watalii, wafanyakazi na wakaazi wa eneo hilo wakiendelea na shughuli zao.
Jana Jaji Lewis Kaplan alichuja jopo la wajumbe hao, ambao hawatajulikana muda wote wa uendeshaji kesi hiyo.
Amefafanua kuwa yeye na wanasheria wa pande zote mbili walikubaliana kupunguza jopo hilo, kutoka mamia ya watu hadi kufikia watu 12, ikiwemo wale wa akiba, ifikapo Jumatatu.
Na katika kuonesha kuwa kesi hiyo ni nyeti, Jaji Kaplan alisisitizia kuhakikishia majaji wa baraza la mahakama kwamba majina yao, sehemu wanazofanyia kazi na makaazi yao hayatawekwa hadharani.
Mwaka jana, Ghailan alikanusha kusaidia mipango ya shambulio hilo la mabomu katika ubalozi wa Marekani Dar es Salaam, Tanzania, huku bomu jingine likilipuka katika muda huohuo kwenye ubalozi wa Nairobi Kenya.
Anadaiwa pia kuwa msaidizi wa karibu wa Osama bin Laden.
Wanasheria wake walijaribu kuizuia kesi hiyo, wakihoji kuwa haki za kisheria za mteja wao zimekuwa zikikandamizwa kutokana na kuteswa katika gereza la siri la shirika la Ujasusi la marekani CIA, na pia kuwekwa kizuizini kwa miaka mitano, ikiwemo katika gereza la Guantanamo, kabla ya kesi yake kusikilizwa mahakamani.
Anakabiliwa na kifungo cha maisha, iwapo atatiwa hatiani.
Kesi hiyo ni mtihani kwa Rais wa nchi hiyo Barack Obama kwa ahadi yake ya kumaliza mateso na ukiukaji wa haki katika vita dhidi ya ugaidi. Kwa mara ya kwanza kesi hiyo ilisikilizwa jana Jumatano.
Itakumbukwa kuwa lori lililosheheni mabomu liliripuka nje ya ubalozi wa Marekani uliokuwa katikati ya jiji la Nairobi na shambulio jengine lilitokea Dar es Salaam katika nchi jirani ya Tanzania kwa wakati mmoja.
Marekani ilimtuhumu kiongozi wa kundi la kigaidi la Al Qaeda, Osama Bin Laden aliyeuawa mwaka 2011, kwa kuamuru na kupanga mashambulizi hayo.