Itakuwa dunia yako wewe na huyo mama mwenzio anayejibu 'mpe huyo' (maneno ya saluni na kwenye taarab) lakini kama unamaanisha dunia hii tunayoishi, weka uthibitisho. Au unadhani maneno ya huyu Ganga Chumba ndio sheria? Huyu si muhanga tu wa maumivu ya Messi!
Mimi huwa sibishani kijingajinga bwana, nakupa facts mezani ujinyonge na sio maneno ya kwangu mwenyewe. Huyo Dinho acha akae museum na mwenzake Pele, huku nje yupo Messi 'The Soccer Messiah'.
Hizi rekodi za Lionel Andress 'Leo' Messi zinawauma sana. Hamna la kufanya zaidi ya kuongea maneno ya kujifariji na kujaribu kupaka rangi kaburi. Swali hili hamtaki kulijibu mnawahi tu kuleta ngonjera: Kama Ronaldinho alikuwa that much useful, je Barcelona walimuuza kwa kuwa walikuwa na matatizo ya fedha au yeye alilazimisha kuondoka?