Leo sijisikii kuwasalimia, ngoja niende kwenye hicho nilidhamiria kuwashirikisha.
Leo asubuhi muda wa saa 2.28 nilifika eneo la benki ya CRDB Tawi la Nyerere hapa Mwanza. Ilikuwa imebaki kama dakika mbili hivi wafungue milango. Nilikuta baadhi ya wateja wengine wameshafika wanasubiria muda ufike waingie ndani ya Benki kwa ajili ya kupata huduma.
Milango ilivyofunguliwa nikawa wa kwanza kuingia na kwenda moja kwa moja kwenye foleni. Tellers wakati huo walikuwa hawajaanza kuhudumia walikuwa bado wanaweka weka mambo yao sawa.
Hamadi! nikamwona dada mmoja ambaye wakati milango imefunguliwa alienda kaunta (bila shaka alikuwa anaomba kujulishwa salio lake), akaja moja kwa moja akasimama mbele yangu. Nikamuuliza vipi dada mbona unanipita? akajibu kwa shari kubwa, "unasema ninakupita, naona umechanganyikiwa wewe, hivi unajifanya hukumbuki kuwa mimi ndie nimekutangulia kufika hapa kwenye jengo la Benki, wee si umekuja umenikuta hapo nje nasubiri milango ifunguliwe!, mimi na wewe na nani amempita mwenzie?"
Niliamua kukaa kimya sikumjibu, moyoni nikasema huyu dada anataka kunianzishia siku yangu vibaya. Nikamwacha akapita akahudumiwa baadae na mie nikahudumiwa.
Niliamua kukaa tu kimya, hivi ingekuwa ni nyie wenzangu Miss Natafuta, Joseverest na wengineo mngemfanya nini huyu dada ambaye ana onesha wazi kuwa ana kisirani cha asubuhi asubuhi.
Leo asubuhi muda wa saa 2.28 nilifika eneo la benki ya CRDB Tawi la Nyerere hapa Mwanza. Ilikuwa imebaki kama dakika mbili hivi wafungue milango. Nilikuta baadhi ya wateja wengine wameshafika wanasubiria muda ufike waingie ndani ya Benki kwa ajili ya kupata huduma.
Milango ilivyofunguliwa nikawa wa kwanza kuingia na kwenda moja kwa moja kwenye foleni. Tellers wakati huo walikuwa hawajaanza kuhudumia walikuwa bado wanaweka weka mambo yao sawa.
Hamadi! nikamwona dada mmoja ambaye wakati milango imefunguliwa alienda kaunta (bila shaka alikuwa anaomba kujulishwa salio lake), akaja moja kwa moja akasimama mbele yangu. Nikamuuliza vipi dada mbona unanipita? akajibu kwa shari kubwa, "unasema ninakupita, naona umechanganyikiwa wewe, hivi unajifanya hukumbuki kuwa mimi ndie nimekutangulia kufika hapa kwenye jengo la Benki, wee si umekuja umenikuta hapo nje nasubiri milango ifunguliwe!, mimi na wewe na nani amempita mwenzie?"
Niliamua kukaa kimya sikumjibu, moyoni nikasema huyu dada anataka kunianzishia siku yangu vibaya. Nikamwacha akapita akahudumiwa baadae na mie nikahudumiwa.
Niliamua kukaa tu kimya, hivi ingekuwa ni nyie wenzangu Miss Natafuta, Joseverest na wengineo mngemfanya nini huyu dada ambaye ana onesha wazi kuwa ana kisirani cha asubuhi asubuhi.