Leo nimegundua kwanini watu wakifumaniana wanafanya ukatili

Leo nimegundua kwanini watu wakifumaniana wanafanya ukatili

IKARAHANSI

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2019
Posts
398
Reaction score
479
Habari za muda huu waheshimiwa

Jana nimeona video clip inayomuonyesha Mwanaume aliyekatwa masikio baada ya kufumaniwa akizini na mke wa mtu ikisambaa kupitia mitandao ya kijamii, video clip hiyo ilisindikizwa na maneno ya Wakili (nimemsahau jina) aliyekuwa akifafanua kuwa kosa la kumfumania mkeo au mumeo kisheria adhabu yake ni kulipa faini kwa aliyefumaniwa au kufungua shauri la talaka endapo mume/mke atajisikia kufanya hivyo.

Sasa nikajiuliza namna mke anavyouma (kwa jinsi mapenzi yalivyo) halafu nimemfumania na jamaa nikaamua kufuata sheria kwa kwenda mahakamani, sote tunaujukiritimba wa mahakamani ikiwemo kupigwa kalenda, kuacha kazi/shughuli ya kuniingizia kipato kwa ajili ya kuhudhuria shauri mahakamani (upotevu wa muda) kumbe hatimaye ni kulipwa faini (ikiwa atakutwa na hatia). Sasa nikajiuliza zaidi mgoni wangu akinilipa fidia si ni kama ametoa mahari?

Kwa maana nyingine ni kuwa mtu mwenye ukwasi anaweza kucheza na ndoa yako anavyotaka maana anajua ukimfumania fedha ya kulipa faini anayo hivyo atakuwa mke wenu na siyo mke wako hapo bado sijajua akizaa naye itakuwa vipi. Kwa hukumu ya namna hii ni bora kumuacha mke au kumtia ulemavu mgoni wako ili hata kama utakwenda jela umuache na kumbukumbu ya kusimulia wajukuu zake.

Binafsi nilidhani kuwa kosa la kufumaniwa na mke/mume wa mtu adhabu yake ni kifungo cha jela kuanzia miaka kumi na tano (15 Yrs) na kuendelea, maana ukikutwa na mwanafunzi ni miaka thelathini (30 Yrs) hivyo hii ilitakiwa kuwa nusu yake maana wahusika wanajitambua na wapo juu ya miaka 18.

Binafsi naona adhabu ya kulipa faini haitoshi au wakuu mnasemaje. karibuni kuchangia na povu ruksa mradi tuelimishane.
 
Hata ukiua wote hamna wa kukufanya kitu, hata huyo aliesema maswala ya faini ukimchukulia wa kwake hlf umpe fine hzo milion 3 sidhani kama atkubali, ila sipendi kuongelea wenzangu .

Mimi ukizama anga zangu lazima nichukue maamuzi binafsi na ninaelewa sheria ipo maana huwezi niamulia wakati mimi najua uzito na hasara ya kufinyiwa hapo lazima nihakikishe umeumia.

Corona ipoo chukua tahadhali.
 
Ndoa sio ya kuingia kichwa kichwa, kuoa kila Siku tunaambizana humu
Haya mambo ya kufumaniwa na kufumania ni vitu inatakiwa uvipime haswa kama utaviweza au hutoviweza ukipata jibu muafaka. Ndio ufanye maamuzi ya kuoa.

Wakati jamaa kamkata masikio mwenzake kwa kufumania ukute na mji kashaukimbia maana ni jinai ndio itamfuata, haya umefumania umemkata masikio mgoni, unakimbia mji na kumuacha mkeo akitanua na umalaya wake.

Ukiona mkeo hajatulia njia sahihi kabisa ni kumuacha aendelee na umalaya wake, tafuta aliyetulia.
 
Ndoa sio ya kuingia kichwa kichwa , kuoa kila Siku tunaambizana humu
Haya mambo ya kufumaniwa na kufumania ,ni vitu inatakiwa uvipime haswa kama utavuweza au hutoviweza ukipata jibu muafaka. Ndo ufanye maamuzi ya kuoa.
Wakati jamaa kamkata masikio mwenzake kwa kufumania ukute na mji kashaukimbia maana ni jinai ndo itamfuata , haya umefumania umemkata masikio mgoni , unakimbia mji na kumuacha mkeo akitanua na umalaya wake .

Ukiona mkeo hajatulia njia sahihi kabisa ni kumuacha aendelee na umalaya wake .tafuta aliyetulia.
[emoji106]
 
Mwanamke ukigundua anatoka nje wewe wala usipanic jipe muda tu wa kushusha hasira kimya kimya.

Then taratibu anza kuweka mipango ya kuhama na kupata mji mpya, tafuta mwanamke kimya kimya, mjulishe kinachoendelea na upange nae life.... Piga mimba anzisha familia kimya kimya....

Mambo yakikaa vema mjulishe mke wa sasa kuwa unafanya mpango wa kuoa na unahama hapo. So nyumba aidha unapangisha au uanaiuza unahamia mji wako mpya.
 
Mimi nikimkuta mwanaume chumbani kwangu ndio ndamkung'uta vibaya sana ila kama mwanamke wangu atanyanyua miguu yake toka kwangu kwenda kufanywa huko atakuwa kajipendea nikimgusa mgoni wangu ndakuwa nimemuonea sana.
Mimi hata nikimkuta mwanaume anamla mke wangu kwenye kitanda changu, bado nitamuacha atoke salama, mtu hawezi kuja kwako bila ramani.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Ukifanya hivyo utamuumiza sana mgoni ki mawazo lazima ajiulize unamipango gani na yeye.
Haha either way bora iwe hivo kuliko akuweke busy kwa battle ambalo huna uhakika kama utashinda au litaisha vipi.

Haya unamkodia watu kwa gharama halafu deal inakuja ku backfire unakwenda jela na kuacha projects zako kibao,
Utaona bora ku move on ni njia sahihi sana ukifumania.
 
Hata ukiua wote hmn wa kukufanya kitu, hata huyo aliesema maswala ya faini ukimt*mbea hlf umpe fine hzo milion 3 sidhani kama atkubali, ila sipendi kuongelea wenzangu .

Mimi ukizama anga zangu lazima nichukue maamuzi binafsi na ninaelewa sheria ipo maana huwezi niamulia wakati mimi najua uzito na hasara ya kufinyiwa hapo lazima nihakikishe umeumia.

Corona ipoo chukua tahadhali.
Umezungumza as if kila anayefumaniwa anakuwa chini ya capacity yako
Unaweza ukifumania na mgoni wako akawa wale ku tick all the boxes, likumbuke na hilo.
 
Ndoa sio ya kuingia kichwa kichwa , kuoa kila Siku tunaambizana humu
Haya mambo ya kufumaniwa na kufumania ,ni vitu inatakiwa uvipime haswa kama utavuweza au hutoviweza ukipata jibu muafaka. Ndo ufanye maamuzi ya kuoa.
Wakati jamaa kamkata masikio mwenzake kwa kufumania ukute na mji kashaukimbia maana ni jinai ndo itamfuata , haya umefumania umemkata masikio mgoni , unakimbia mji na kumuacha mkeo akitanua na umalaya wake .

Ukiona mkeo hajatulia njia sahihi kabisa ni kumuacha aendelee na umalaya wake .tafuta aliyetulia.
Haya maneno ni ya busara sana kwa sasa (ikiwa halijakukuta), kwa maana mapenzi ni hisia (usifanye mchezo na kupenda). Lakini pia binadamu tunabadilika yawezekana wakati namuoa alikuwa ametulia ila baada yakuishi na kuzaa watoto watatu kakutana na walimwengu wamembadilisha.

Kitu kingine unapoamua kuachana na mke au mume usijifikirie wewe tu, fikiria pia na watoto watakapotengana na mama au baba yao malezi yao yatakuwaje. Usitamke kuacha mke kama vile ni kwenda chooni kutoa taka mwili (siyo rahisi kiivyo).
 
Mwanamke ukigundua anatoka nje wewe wala usipanic jipe muda tu wa kushusha hasira kimya kimya.

Then taratibu anza kuweka mipango ya kuhama na kupata mji mpya, tafuta mwanamke kimya kimya, mjulishe kinachoendelea, na upange nae life.... Piga mimba anzisha familia kimya kimya....

Mambo yakikaa vema mjulishe mke wa sasa kuwa unafanya mpango wa kuoa na unahama hapo. So nyumba aidha unapangisha au uanaiuza unahamia mji wako mpya.

Sent using Jamii Forums mobile app
Chief, Kama mna watoto huoni kama utakuwa umewakomoa!?
 
Hata ukiua wote hmn wa kukufanya kitu, hata huyo aliesema maswala ya faini ukimt*mbea hlf umpe fine hzo milion 3 sidhani kama atkubali, ila sipendi kuongelea wenzangu .

Mimi ukizama anga zangu lazima nichukue maamuzi binafsi na ninaelewa sheria ipo maana huwezi niamulia wakati mimi najua uzito na hasara ya kufinyiwa hapo lazima nihakikishe umeumia.

Corona ipoo chukua tahadhali.
Kwani huyo mwanamke ni binadam au ni kitu kisichoongea? VIP kama kamwambia jamaa hajaolewa ana mshkaji tu?

Pili kuna umuhim gani kuumiza mtu ambae mke wako akitaka anachukua mtu mwingine?

Kama mke wako ni malaya unadhan utauwa watu wangapi?
Ikitokea umefungwa jela mke wako atabak kuwa wako?

Maamuzi ya busara ni muhim sana kiongozi.. maisha ni kuchagua na kuchanga karata zako vizur...
 
Kupokea pesa kutoka kwa jamaa aliekugongea mkeo Ni fedheha kubwa Sana hapa duniani.

Kuna mtu mtaani alilipwa pesa Kama faini ya kugongewa mkewe akanunua pikipiki. Hata mke ana kudharau zaidi kwamba wew kwenye pesa si lolote ipo siku utatoa rinda kisa pesa.

Kama unapoke pesa ya mgoni wako Kama faini Basi mruhusu tu mkeo aende uwanja wa fisi awe anakuletea hesabu asubuhi.
 
Back
Top Bottom