Leo nimekumbuka namna mpenzi/ mama wa watoto wangu alipoanza kunishinda kipato baada ya kupata kazi kila kitu kikaparaganyika

Kama sijaelewa hiv?
Namaanisha kila mtu ni wakipekee linapokuja suala la kujipa furaha mwenyewe!!
Mfano mtu X anapenda Sana kucheza muziki,mwingine Kula vizuri yaani migahawa yote mjini anajua radha ya vyakula vyao! Mwingine Pombe, mwingine Wanawake!! So furahia maisha na chagua starehe ambayo haikuweki mbali na Mungu wako!!
Tunaishi mara moja!!
 
Sjaelewa hapo mwishoni wazazi wa jamaa walifanyaje?huu mjadala naufuatilia mguu kwa mguu
 
Huwa nawaangalia sana wale ndugu zangu wanaosema hawawezi kutetereshwa na mapenz/mwanamke hata iweje, huwa nawaza wao wamezaliwaje!?

Natamani sana niwe na moyo mgumu mambo yakuumia na mapenz yanaboa sana, sijaoa na sina hamu yakuoa kwa yaliyonitokea tu kwa mchumba bado npo nae ila namchukia.

Natamani hata tuachane nimsahau ila moyo bado umemkomalia tu huyu boya.
 
Nimepata taarifa kuna mtu mtaani kwetu huko kaachwa na mwanamke wake .kamfuata hadi nyumbani kwao kwenda kumpiga na bado anamtafuta na kisu amchome. Kuna watu wakiachsa akili zao hazifanyi kazi kabisa wao wanaona Bora kufa kuliko kuachwa.
 
Aliondoka bila ugomvi na ni ndoa ya kikiristo.
 
Aah hv nitaoaga kweli mm !? Why in this world such things happen hebu mniache tu bana.
 
Ukitaka kujua kuwa huyo mwanamke uliyenaye ni wife material, muangalie pale unapopata matatizo ya kikazi, anakuwa na tabia zipi? (Je anaendelea kukupenda?, anakutia moyo? n.k)

Nakumbuka Kipindi kile cha JPM kuna wafanyakazi wenzangu 6 waliachishwa kazi kwenye lile sakata la vyeti feki. Hadi sasa ni mmoja tu ndio bado yupo na mke wake. wale wengine 5 walishatengana na wake zao na mmoja alifariki

Nimejifunza kuwa kwa wanawake ela yake ni yake ela yako ni yenu wote. mwanamke anapokuwa na uwezo kifedha kuliko mwanaume anakuwa na uhuru wa kufanya chochote na kupelekea dharau kwa mume.

Tuishi nao kwa akili
 
Akili inatakiwa nyingi sana kuishi nao,nilishasema hapo bila kumshirikisha Mungu unaweza kufanya chochote ukajikuta wewe ndio uko matatani,nimepitia hiyo njia nawajua sana hawa viumbe...
 
Ninachojua mwanaume anataka heshima kutoka kwa mkewe na sio upendo
 
Ms R, navumilia aisee na ninaenda na haya Maneno ya Mwanazuoni maarufu duniani πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

Uvumilivu ni mzuri. Matokeo ya kusubiri ni mazuri. Ikiwa Mwenyezi anakufanya ungojee, uwe tayari kwa jambo lililo zaidi ya matarajio yako. Anajua sio rahisi kwako kwa hivyo anahakikisha kuwa inafaa kungojea kwako.
#DontLetMeFall
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…