Leo nimekumbuka namna mpenzi/ mama wa watoto wangu alipoanza kunishinda kipato baada ya kupata kazi kila kitu kikaparaganyika

Leo nimekumbuka namna mpenzi/ mama wa watoto wangu alipoanza kunishinda kipato baada ya kupata kazi kila kitu kikaparaganyika

Angawa wapo wanawake ambao hata wakiwa financially stable wanaheshimu ndoa zao ,ila walio wengi wana kuwa jeuri na kazarau flani hivi kwa wanaume zao, kazalika kwa wanaume vile vile ingawa kwa wanawake mmmmmm anakua don't touch me
Utambiwa mwanaume huna mbele wala nyuma kama mche wa sabuni 🀣🀣🀣🀣
Wenye degree wacha waolewe na wenye degree wenzao sie bodaboda tutaoa hawa hawa fomu foo failure tunatulia kwa amani

Huyu aliyekuja na wazo la kusomesha wanawake kwa kweli nikimkuta mbinguni aisee itakuwa murder in heaven kwa kweli
 
Pole ndugu...
Ila hii story mbona mbona zimekuwa nyingi...
Ni kweli mwanamke akikuzidi tu kipato jitayarishe kuondoka na kuanza maisha mapya. Wanakamilika na kuwa mashetani kamili!
Kumbe mnajua kuwa nimasheta i sasa y mnayafuga mashetani ndani ya nyumba wajameni?
 
Haya mambo haya yanapendeza kusimuliwa tu hivi kwa wenzako......usiombe yakukute......ni mazito...............

Mdogo wangu nakumbuka yalipomkuta alikuwa anashinda chooni kutwa kama mende......hata chakula hali anasema hakina ladha.......

Ila mapenzi hayana baunsa......ukiwa hujaingia kwenye kumi na nane unaweza ukaongea mengi sana ya kejeli na dharau........

Baba yangu mdogo alikuwa anaongea sana shombo.....siku aliyokimbiwa na mkewe ndio nikajua haya mambo hayana mwenyeji......

Alikuwa anashinda ukweni anaomba msamaha mpaka usiku analala kibarazani kama mlinzi........dah!!

Haya mambo haya.....huwa yanaanza kama utani vile.....
Hatari saana
 
Miaka 5 nyuma nilipatwa na hiki kisa, sijui huwa kuna nini kinatokea kwa wenzetu naweza kusema alikuwa mke kabisa maana kwao walinifahamu posa na mahari nilishamaliza na watoto wawili nimemzalisha sasa kipindi chote hicho alikuwa anafanya shughuli ndogondogo tu.

Sasa ikatokea fursa sehemu nikamwambia mama kwa haya maisha tunayoishi itachukua muda kutoboa hapa ebu kamatia iyo fursa ya kazi tusaidizane bwana bwana bwana kumbe ndio nilikuwa namaliza familia yangu wakuu kitendo cha yeye kupata ile kazi tu na vile nilimtumia mtu ninayemjua ilikuwa rahisi sana kwake kutoboa.

Picha linaanza kwanza amepangiwa mkoani akili ikacheza mmh nikiwa nipo kwenye dilema ya maamuzi kwao wakawa wapo karibu nae zaidi na wakamwambia aende huko kwa kuwa watoto bado wadogo waende kwa bibi yao yaani mama yake hadi mambo yatakapokuwa sawa kule then awachukue.

Basi mwezi ukaisha mwezi wa pili mara miezi sita nikaanza kuona mapicha picha kwanza sikuwahi kuona hela yake ingawa alikuwa analipwa mara 4 ya mshahara wangu bado nilitakiwa kutuma pesa ya matumizi kwangu hakuwa shida maana naelewa mwanaume ndio mtunza familia kifedha.

Alifanikiwa kurudi kipindi cha mwanzo mwanzo tu tena akaniletea nyodo hatari stori zake sasa ooh mwaka huu nanunua gari sijui wewe umeshindwa hiki na kile nikitaka tunda anajivutaa nikajisemea hii ngoma ndio imeshavuja hapa...kwakweli haikufika hata mwaka tukabwagana.

Hakuna kipindi nilikonda kama kipindi kile full mawazo alafu ndugu zake wananichora tu kenge wale!
ilibaki kidogo nidondoke nifeee!

Kuna mama mmoja mtu wa makamo akanifuata na kuniweka chini kisha akanipa ushauri mmoja wa nguvu sana akaniambia kijana wangu usiwe mnyonge hivyo tafuta mwanamke mdogo na mzuri kuliko mkeo then furahia maisha haya maisha ni mafupi sana na utamsahau.

Kwa kweli namshukuru sana yule mama maana from there maisha yalibadilika taratibu nilianza kumsahau yule mwanamke na mambo yake ingawa bado muda mwingine naumia ila ndio maisha isee
tuishi nao kwa akili!

Kwanini nimeleta huu uzi..?
Nataka vijana wenzangu hasa hawa wadogo ambao wanajianda kuingia kwenye maisha ya familia wawe makini na kujitaidi wajipende na wao wasijitoe sana kwa ajili ya familia zao things change na maumivu utayopitia sio ya kawaida mm nilikuwa najiona mgumu nilikuwa nashangaa wanaume wanaolalamikia wake zao ila yalivyonikuta nilijishangaa najikaza ila uso na mwili vilijionyesha kuwa nipo kwenye maumivu jamani maumivu ya mahusiano hayaelezeki tena kwa sisi ambao tulishakuwa na familia utashangaa chakula hakipiti wala maji hayashuki..kuna bond inayojitengeneza ukishazoea kuwaona watu wako wa karibu kila siku kuitoa hiyo ni ngumu sana yaani kuna muda nilikuwa nikikaa hivi fikra za watoto wangu wapo mbali muda niliopoteza kuwa na mwanamke yule nilikuwa nafamilia ghafla naishi mwenyewe machozi yanatoka yenyewe tu....
Nashukuru sana gospel music inafariji sana.
Wazee wa ngwasuma a.k.a kataa ndoa wanazidi kuokota points, wanazid kujikita kileleni ..
Upinzani ni mkali sana [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ndio maana nikamwambia tulia kwanza maadam kaz alinipa mimi, sasa kaharibu mwenyewe. Hawa viumbe kuna namna ya kuenda nao hata kama ni kiutani utani πŸ˜‚πŸ˜‚
Anataka haraka kuna wanawake wengine hatuendi hivyo binafsi sipendi kutongozwa hadharani labda uwe utani kama wa bibi na mjukuu, ndo maana kuna pm
 
Back
Top Bottom