Leo nimemuona Nadir Haroub Cannavaro nikakumbuka kisa chake cha jezi na Eto'o

Leo nimemuona Nadir Haroub Cannavaro nikakumbuka kisa chake cha jezi na Eto'o

Cvez

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2018
Posts
4,405
Reaction score
13,411
Mwaka 2008 Taifa Stars enzi za kocha Marcio Maximo. Enzi hizo mapenzi ya Watanzania kwa timu ya taifa ni 100%. Kuna mkasa mmoja ambao leo umenifanya nimkumbuke Cannavaro mara baada ya kumuona kwenye benchi la Stars.

Ilikua hivi mara baada ya mchezo kati ya Tanzania na Cameroon kumalizika 'Cannavaro' alifuatwa na Eto'o anayecheza klabu ya Barcelona ya Hispania akitaka wabadilishane jezi baada ya pambano hilo kumalizika ambapo Stars ilichapwa mabao 2-1 yaliyofungwa na mchezaji huyo.

Tukio hilo lilibua mjadala baada ya Ofisa Habari wa TFF kipindi hicho, Florian Kaijage kukaririwa na vyombo vya habari akisema 'Cannavaro' atakatwa sh. 20,000 kwa kitendo cha kubadilishana jezi na Eto'o.

Baada ya tukio hili ndio ikawa rasmi kwa wachezaji wa timu ya taifa kubadilishana jezi na wenzao.
 
Mwaka 2008 Taifa Stars enzi za kocha Marcio Maximo. Enzi hizo mapenzi ya Watanzania kwa timu ya taifa ni 100%. Kuna mkasa mmoja ambao leo umenifanya nimkumbuke Cannavaro mara baada ya kumuona kwenye benchi la Stars.

Ilikua hivi mara baada ya mchezo kati ya Tanzania na Cameroon kumalizika 'Cannavaro' alifuatwa na Eto'o anayecheza klabu ya Barcelona ya Hispania akitaka wabadilishane jezi baada ya pambano hilo kumalizika ambapo Stars ilichapwa mabao 2-1 yaliyofungwa na mchezaji huyo.

Tukio hilo lilibua mjadala baada ya Ofisa Habari wa TFF kipindi hicho, Florian Kaijage kukaririwa na vyombo vya habari akisema 'Cannavaro' atakatwa sh. 20,000 kwa kitendo cha kubadilishana jezi na Eto'o.

Baada ya tukio hili ndio ikawa rasmi kwa wachezaji wa timu ya taifa kubadilishana jezi na wenzao.
Tumetoka mbali sana
 
Umaskini mbaya hadi jezi za taifa hazitoshi
 
Mwaka 2008 Taifa Stars enzi za kocha Marcio Maximo. Enzi hizo mapenzi ya Watanzania kwa timu ya taifa ni 100%. Kuna mkasa mmoja ambao leo umenifanya nimkumbuke Cannavaro mara baada ya kumuona kwenye benchi la Stars.

Ilikua hivi mara baada ya mchezo kati ya Tanzania na Cameroon kumalizika 'Cannavaro' alifuatwa na Eto'o anayecheza klabu ya Barcelona ya Hispania akitaka wabadilishane jezi baada ya pambano hilo kumalizika ambapo Stars ilichapwa mabao 2-1 yaliyofungwa na mchezaji huyo.

Tukio hilo lilibua mjadala baada ya Ofisa Habari wa TFF kipindi hicho, Florian Kaijage kukaririwa na vyombo vya habari akisema 'Cannavaro' atakatwa sh. 20,000 kwa kitendo cha kubadilishana jezi na Eto'o.

Baada ya tukio hili ndio ikawa rasmi kwa wachezaji wa timu ya taifa kubadilishana jezi na wenzao.
Umenikumbusha mbali 2-1 ilikuwa Youande.
Daressalaam ilikuwa 0-0 canavaro alimkaba sana Etoo hio mechi nilikuwepo uwanjani kwa mkapa 2008.
 
Kuna yule mchezaji wa taifa stars baada ya mchezo kati ya taifa stars na brazil akahojiwa na vhombo kimoja atoe maoni yake kuhusu mchezo akaanza kusema " hawa ( brazili) wa kawaida sana, wana nini hawa wepesi sana, wanabebwa tu."

Dah jamaa alipondwa sana na wadau wa soka. Mwenye kumbukumbu aiweke hapa alikua nani yule jamaa.
 
Kuna yule mchezaji wa taifa stars baada ya mchezo kati ya taifa stars na brazil akahojiwa na vhombo kimoja atoe maoni yake kuhusu mchezo akaanza kusema " hawa ( brazili) wa kawaida sana, wana nini hawa wepesi sana, wanabebwa tu."

Dah jamaa alipondwa sana na wadau wa soka. Mwenye kumbukumbu aiweke hapa alikua nani yule jamaa.
Kwa nini bongo nihame burudan kama hizi 😂😂😂
 
Kuna yule mchezaji wa taifa stars baada ya mchezo kati ya taifa stars na brazil akahojiwa na vhombo kimoja atoe maoni yake kuhusu mchezo akaanza kusema " hawa ( brazili) wa kawaida sana, wana nini hawa wepesi sana, wanabebwa tu."

Dah jamaa alipondwa sana na wadau wa soka. Mwenye kumbukumbu aiweke hapa alikua nani yule jamaa.
Bila shaka ni Humud huyo
 
Kuna yule mchezaji wa taifa stars baada ya mchezo kati ya taifa stars na brazil akahojiwa na vhombo kimoja atoe maoni yake kuhusu mchezo akaanza kusema " hawa ( brazili) wa kawaida sana, wana nini hawa wepesi sana, wanabebwa tu."

Dah jamaa alipondwa sana na wadau wa soka. Mwenye kumbukumbu aiweke hapa alikua nani yule jamaa.

Kwenye mechi hiyo hiyo TEGETE alimfuata Maicon kumuomba jezi... Maicon akamuangalia Tegete kuanzia uu mpaka chini kisha akaivua na kumtupia Tegete! Tegete akaikotoka kwa furaha zote..akavua ya kwake ili ampe Maicon ila jamaa alikataa jezi ya Tegete..licha ya kwamba ile ilikuwa dharau kubwa ila si haba tegete alirudi na jezi mbili nyumbani siku ile
 
Kwenye mechi hiyo hiyo TEGETE alimfuata Maicon kumuomba jezi... Maicon akamuangalia Tegete kuanzia uu mpaka chini kisha akaivua na kumtupia Tegete! Tegete akaikotoka kwa furaha zote..akavua ya kwake ili ampe Maicon ila jamaa alikataa jezi ya Tegete..licha ya kwamba ile ilikuwa dharau kubwa ila si haba tegete alirudi na jezi mbili nyumbani siku ile
Dah ile mechi ilijaa vimbwanga sana. Huenda hilo tukio ndo lilimfanya jamaa yule awaponde brazil.

Kuna ile shabiki anaingia uwanjan anamfuata Káka.
 
Back
Top Bottom